ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Wakuu'
salamu mbele siku zote.
Nina jamaa yangu ni askari, na huwa anachukuliwa kwenda kusindikiza milipuko kwa ajili ya hawa wezi wanaoharibu mazingira yetu wakitafuta dhahabu sehem mbalimbali za nchi yetu.
Kwa mjibu wa sheria ya milipuko, hairuhusu milipuko hiyo kusafirishwa bila kuwa na kibali cha afisa madini wa eneo husika, lakini pia bila kuwa na police escort.
Kinachonisikitisha, ni malipo wanayopewa baada wakati wakisindikiza. ikumbukwe kuwa, askari wetu hawa, wanalazimika kusindikiza milipuko hiyo kisheria, lakini pia kwao inakuwa ni sherehe kwani akisafiri kwa siku wanapewa 50,000/tsh.
Mimi naamini inawezekana kiwango kinachotambuliwa kimataifa ni kikubwa kuliko wanacholipwa hawa askari wetu, kusindikiza milipuko, ni sawa na kutembea na kifo mkononi.
Mwenye kujua kiasi hasa anachotakiwa kulipwa askari wetu anijulishe niwataarifu hawa masoja wetu wanaohangaika kulisaka tonge, kwani mishahara yao hailingani na majukum waliyopewa na sheria zetu.
nawasilisha
salamu mbele siku zote.
Nina jamaa yangu ni askari, na huwa anachukuliwa kwenda kusindikiza milipuko kwa ajili ya hawa wezi wanaoharibu mazingira yetu wakitafuta dhahabu sehem mbalimbali za nchi yetu.
Kwa mjibu wa sheria ya milipuko, hairuhusu milipuko hiyo kusafirishwa bila kuwa na kibali cha afisa madini wa eneo husika, lakini pia bila kuwa na police escort.
Kinachonisikitisha, ni malipo wanayopewa baada wakati wakisindikiza. ikumbukwe kuwa, askari wetu hawa, wanalazimika kusindikiza milipuko hiyo kisheria, lakini pia kwao inakuwa ni sherehe kwani akisafiri kwa siku wanapewa 50,000/tsh.
Mimi naamini inawezekana kiwango kinachotambuliwa kimataifa ni kikubwa kuliko wanacholipwa hawa askari wetu, kusindikiza milipuko, ni sawa na kutembea na kifo mkononi.
Mwenye kujua kiasi hasa anachotakiwa kulipwa askari wetu anijulishe niwataarifu hawa masoja wetu wanaohangaika kulisaka tonge, kwani mishahara yao hailingani na majukum waliyopewa na sheria zetu.
nawasilisha