Kushuka kwa purchasing power, Je kundi la high income group wanaathirika? Village Supermarket ya high class wa Mbezi Beach Shamo Tower yafungwa!

Na nilishangaa sana Kuona Ujenzi wake hasa Kipindi hiki wakati hali ya Kiuchumi Tanzania ( hasa Kibiashara ) si nzuri. Na ukitaka ulione vyema hilo Jengo pita wakati wa Usiku utaliona linapendeza lakini ndani yake hakuna Wapangaji kabisa. Ninachojua Wafanyabiashara Wakubwa na Wasomi huwa kabla ya Kuanzisha Biashara yoyote / Mradi wowote ule huwa wanatakiwa pia kufanya anticipation hasa ya Business Environment kwa wakati / kipindi husika na hata kwa baadae ili usiingie Hasara isiyokuwaa ya lazima.

Na wala tusifiche hapa hali ya Uchumi kwa Tanzania kwa sasa ni mbaya na Watanzania wengi wapo ICU hasa Kimaisha na kama Mheshimiwa Rais asipoambiwa ukweli na Wasaidizi wake ambao wao Wachache wanafaidika nae huku wakiwa wanamsifia na kumdanganya kuwa hali ni Shwari kuna Siku hawa hawa Watanzania waliopo ICU Kimaisha wanaweza Kuamua kufanya Jambo ambalo pengine linaweza Kuifanya Tanzania irejee ule mfano wa French Revolution ya 1789.

Rais apunguze Miradi mingi ambayo inachukua Pesa nyingi na Kuharibu Mzunguko wa Pesa kwa Wananchi, ahakikishe Watu wa TRA wanakuwa ni Chachu ya Kuboresha Biashara za Watu kwa kuwatoza Kodi Rafiki, Benki nazo ziweze Kutoa Mikopo ya Riba nafuu kwa Wananchi ili basi Watanzania baadhi wakianzisha Miradi yao zile Pesa ziweze Kuzunguka vyema miongoni mwao ila mkazo mkubwa pia uwekwe katika Sekta ya Kilimo hasa kwa kuwapa Nafuu Wakulima katika Bei za Mbolea na hata Vifaa vya Kilimo na kama haitoshi hata Masoko yao yawe wazi na Kasi ya Uwekezaji nchini iwe ya haraka ili hili Kundi Kubwa la Wasomi wasio na Ajira ( Kazi ) sasa waweze angalau Kuajirika huko.

Wakimaliza hilo warudi tena katika Mfumo mzima wa Elimu yetu Tanzania na yenyewe ibadilishwe na kuwa ya Research Based na siyo ile ya Kikoloni ya Content Based ambayo imezalisha Wasomi wengi wenye Uwezo wa Vyeti tu ( Theory ) ila 85% yao ukija katika Practical ni Watupu kabisa kiasi cha kuwafanya wengi wao wasiwe Competent na kuwa mojawapo ya sababu ya wengi wao / wetu kutoajirika. Masomo ya Biashara, Matangazo, Ubunifu, Sayansi, Utafiti na Ujasiriamali ndiyo yanatakiwa yapewe mno Kipaumbele kwa sasa nchini Tanzania na zile Fani zingine nazo hasa za Masomo ya Sanaa ( Arts ) nao Mitaala yao inatakiwa iboreshwe zaidi ili kuweze Kuendana na Mazingira ya sasa ya Kidunia ambayo yametaliwa na Teknolojia na Ubunifu zaidi.

Rais aambiwe huu Ukweli tafadhali na aupokee kwa mikono miwili na siyo aununie kwa kutuona tunaomwambia labda tunamchukia wakati kumbe yawezekana Sisi tulio mbali nae na ambao 24/7 tupo Mitaani na katika Jamii husika na huenda wengine tukawa ni Wahanga wa haya Maisha magumu ya sasa ndiyo tunampenda na ndiyo maana tunachukua muda wetu huu kumuandikia mambo kama haya ambayo kamwe kwa aina wa Viongozi wake wengi Wanafiki aliowateua na anaowaamini hawawezi Kumuambia ng'o.
Mkuu assumption za kiuchumi zilizofanywa awamu ya 4 zinagoma kabisa awamu hii
Mfano kwenye real estate
 
Tumenunua ndege mpya tumejenga fly over na uwanja wa ndege std gauge na bwawa lakuzalisha umeme la Nyerere daraja lakigamboni haya ndio majibu yasiku hizi kama enzi zile kwenye historia sekondari yale majibu yanyambari cheap labour,high population,good climate etc 🤣🤣🤣🤣
 
True
Bora angeanza na ile ya umeme..ile kweli itamgusa kila mtanzania..ni wazo nampongeza sana

Ndege i think ts okay..japo hata for national prestige tu

Reli ingekuja walau baada ya umeme wa kutosha kuwa ready

Serikali kuhama wasnt an emergency+ni costful na ni ishu ya watu wachache

Deni la taifa watanzania mtalinywaa km sio kulioga
Katika miradi yote mradi utakaotutia umaskini vizazi na vizazi ni huo wa Stiglers Gorge. Bila kuzingatia sababu za WWF kuhusu kuvuruga ecosystems na world heritage site kuna sababu 3 za nguvu kwa nini Stiglers Gorge ni wastage of money; (1) Maji yapatayo 36% yaliyokuwapo mwaka 1980 wakati feasibility study ilifanyika sasa hivi hayapo (2) Umeme wa kutegemea maji siyo wa kuaminika kwenye karne hii kutokana na mabadiliko ya tabia nchi (3) Hata Mtera na Kihansi zilipojengwa miaka ya 1980s na 1990s tuliambiwa zingekuwa ni suluhisho la umeme lakini zimeahindwa.

Reli ya SGR shida yake kubwa ni mizigo, kule ilikoelekea hakuna mzigo mkubwa wa kuweza kulipa gharama za ujenzi. Rwanda peke yake na mzigo wa ruti hiyo haiko economically visible. Labda kama na Eastern DRC kwenye jimbo la Goma nako kungekuwa na network ya SGR.
 
Katika miradi yote mradi utakaotutia umaskini vizazi na vizazi ni huo wa Stiglers Gorge. Bila kuzingatia sababu za WWF kuhusu kuvuruga ecosystems na world heritage site kuna sababu 3 za nguvu kwa nini Stiglers Gorge ni wastage of money; (1) Maji yapatayo 36% yaliyokuwapo mwaka 1980 wakati feasibility study ilifanyika sasa hivi hayapo (2) Umeme wa kutegemea maji siyo wa kuaminika kwenye karne hii kutokana na mabadiliko ya tabia nchi (3) Hata Mtera na Kihansi zilipojengwa miaka ya 1980s na 1990s tuliambiwa zingekuwa ni suluhisho la umeme lakini zimeahindwa.

Reli ya SGR shida yake kubwa ni mizigo, kule ilikoelekea hakuna mzigo mkubwa wa kuweza kulipa gharama za ujenzi. Rwanda peke yake na mzigo wa ruti hiyo haiko economically visible. Labda kama na Eastern DRC kwenye jimbo la Goma nako kungekuwa na network ya SGR.
36% reduction for abt 40 years
So roughly another 80 years ili yawe yameisha..ila global warming haitotuacha salama

Vizazi vijavyo watajiju..watafte mbinu zao maybe umeme wa solar na upepo unatufaa...Hasa solar

SGR wamejengewa watumishi wa umma wa dodoma ama..?.maybe kutoa mizigo kati kuja coastal regions

Yafaa kutafakari kwa marefu na mapana sana
 
Bwana Paschal ndio nini hiki umeandika?

Ni kwamba unauliza na unataka ujue ni kwanini hizo shopping centers zimefungwa au shida ni kujua muathirika wa hii low purchasing power aliyosababisha huyu bwana mkubwa?
 
Funguka mkuu japo kiduchu,tupone wengi.

Mkuu mada inahusishwa na purchasing power. Yangu ilikatika ghafla bin vuu. Kwa hiyo tangu miaka 2 iliyopita sikuwahi kutia mguu wangu mle kufanya "shopping", kwa mangi na magengeni niko "popular" sana 🤣. Sasa kwa nini ilikatika, ni siri yangu ila siyo siri tena kwa wengi waliokumbwa na hali kama yangu... hope umenisoma!
 
Mkuu mada inahusishwa na purchasing power. Yangu ilikatika ghafla bin vuu. Kwa hiyo tangu miaka 2 iliyopita sikuwahi kutia mguu wangu mle kufanya "shopping", kwa mangi na magengeni niko "popular" sana 🤣. Sasa kwa nini ilikatika, ni siri yangu ila siyo siri tena kwa wengi waliokumbwa na hali kama yangu... hope umenisoma!
Mhh hadi wewee ulikua mpiga dili?.
 
Watanzania hatuna ubunifu na mipango ya biashara mizuri.

Halafu kila mtu ana duka hilohilo au biashara hiyohiyo hilo ni kosa la kiufundi kwenye biashara yoyote.

Ukifanya hivyo unawafanya wateja kuwa na nguvu ya kwenda duka moja tu kati ya matano ya mtaa mmoja, na kisha mwaanza kushikana uchawi.

Kila mtu ataka kufanya biashara ya aina moja hiyo haiwezekani.
Mkuu huo ubunifu tumeukosa tu awamu hii??
 
Mkuu huo ubunifu tumeukosa tu awamu hii??
Hata awamu zilizopita hakukuwa na ubunifu,tofauti ni kwamba haukuwa unahitajika sana sababu ulifunikwa na uhalifu, hewa hewa nyingi, madawa ya kulevya nk kwa sasa ubunifu unahitajika sababu ile mianya ya uhalifu iliyofanya ubunifu kuonekana si lolote si chochote umezibitiwa, kama ni pesa utaipata kwa kutumia maarifa (kufikiri kitu tofauti siyo mazoea)..
 
Nisingependa kuongelea serikali ya nchi yangu vibaya, so i shall stick to issue ya supermarkets kupwaya maana nimeona kuna changamoto kidogo tokea hata kwa wa kajamba nani. Mimi huwa napita Karume kufanya shopping ya mavazi na vitu vya kawaida vya majumbani mara kwa mara, mwezi uliopita nilitaka kuongeza pair ya kiatu cha mtumba nikashuka Ilala, chakushangaza nikuwa viatu vizuri kupata ni kwa mbinde sana na maeneo yamefungwa baadhi.

Sasa kwa upande wangu sidhani kama uchumi umebana sana na hata vijana wenzangu wa sokoni waliniambia kuwa hamna shida sana, issue nikaja kusanuka kuwa kwa awamu hii watu wanafuatilia sana vitu online more than moving places. Na hawa wanaofanya online tradings wakiwa hawana ofisi maalum wanaumiza sana hawa wafanyabiashara wa kawaida na pia kama issue ya mitumba ni kuwa wanaenda kuchukua bidhaa nzuri karibia zote kwa bei nafuu nakuja kupandisha bei zao wenyewe wanazotaka. Kwahiyo kuna ka system kamebadilisha upepo wa market sana hapa bongo ila watu hawaoni kwa undani wake. Kwa mfano kama hiyo supermarket walikuwa wanauza vitu vya bei ya gharama kubwa na pia kufika eneo husika ili uweze lazima uchukue mda na resources zingine basi siku hizi kuna wakulima wengi wanalima na kufanya packaging na kusambaza mazao kwa bei poa sana hata kwa delivery bure sometimes, bado wafanyabiashara wa mavazi, vyombo vya ndani n.k. Na ndio maana nikienda Karume au kwenye maeneo yetu ya kajamba nani utakosa vitu vizuri kwani vimeshapitiwa na hili kundi la online users, kwahiyo hali ni tete sishangai kufungwa kwa Village Supermarket, Shoprite walifikia pabaya pia wakaondoka pale Mlimani na Tz kwa ujumla, Nakumatt zilipotea pia kule Kenya naona zimekuja huku Tz ila zinasuasua, Mr. Price ilipitia issue za namna hii japo haikuwa awamu hii ya tano. Kwahiyo mfumo wa huduma na uendeshaji ndio unaoharibu mienendo ya kibiashara worldwide. I'm a tech junkie kwahiyo najua fika ninachoeleza. Huko South Africa tunakoona kuna uchumi wa kutisha ndio big chain supermarkets kama Pick n Pay, Spar zina suffer bigtime, fanya research.

Ukitaka kujua technology inavyosumbua dunia ya leo, fuatilia how e-commerce inakuwa kwa kasi, kama Jumia, Ali Express (Ali Baba) etc. Ukiingia youtube au kufanya research ya Amazon ambapo sub-branch yake ya AmazonGo inavyoelekea kuipiku Walmart miaka ya usoni au kuipa threat katika retail market utaelewa kuwa haya masoko ya mitindo wa zamani yanaelekea ukingoni kufa kama hayata adapt technology zilizopo na zinazokuja baadae.

NB: E-Commerce is the power house of Market Economy today, whether you like it or not. Serikali yetu kuona wanaanzisha mambo ya E-Government nakadhalika ni kuwa hamna namna hapa lazima twende sawa. Watu wanashangaa kuona VunjaBei, Frank Knows, Usiendee Kariakoo, Kelvin KB wanauza kama wako Kariakoo kumbe wanatumia online platforms to emphasize e-commerce na wanatanua wigo like wildfire huko Kariakoo, Posta wanafunga maduka. Issue sio purchasing power maana kama vijana hawa wanapanuka kwa mauzo na utambulisho basi tujue kuwa utamaduni ndio umebadilika na sisi wengi wetu bado hatuja amka kifikra.
 
Middle class Tanzania imeporomoka au haipo kabisa, most likely tumebaki na working class , yaani tumebaki kuwaona ambao wanaishi kwa living wages kama ndio middle class. Hata ile village ya seaclif village inasuasua, yule jamaa wa Shoppers ana-survive sababu yale majengo ni ya kwake.
Mada nzuri na yenye ukweli,unapoona kuna dalili za working class to stuggle to make end meets elewa kuna tatizo,uchumi wetu unakuwa kwenye makaratasi na kwenye hutuba za wanasiasa wetu ila hali halisi on the ground inaongea tofauti,angalia social services zetu zote zinayumba,kuanzia Elimu,Afya,etc etc na bado tunaongopewa kuwa uchumi unakuwa wakati sio,angalia inflation yetu na rate exchange yetu bado inaonyesha uncertainty kubwa na market inachukia kunapoonekana dalili kama hizi,njia ambazo serikali yangu inaweza kuzifanya ni pamoja na serikali kuonyesha confidence kwa wawekazaji,ruhusu uchumi huria na hapa serikali ikitayarisha na kulinda mazingira bora ya uwekezaji;wenzetu wa hapo Nigeria baada ya kuona middle class yao inayumba(kuyumba kwa hawa kunaweza kukaiangusha serikali iliyo madarakani)imelazimisha mabenki yote kutoa mikopo kwa raia wake ili kutengeneza faida na kama watashindwa warudishe pesa central bank zikae bila ya kuzalisha faida ,kwa hiyo mabenki haya kwa sasa yanatoa zaidi ya 60% ya deposit zao kusaidia middle class kujinasua maana hawa ndio wenye idadi kubwa ya wanunuzi wa bidhaa na wenye uwezo wa kusukuma maendeleo ya nchi.
 
Watanzania hatuna ubunifu na mipango ya biashara mizuri.

Halafu kila mtu ana duka hilohilo au biashara hiyohiyo hilo ni kosa la kiufundi kwenye biashara yoyote.

Ukifanya hivyo unawafanya wateja kuwa na nguvu ya kwenda duka moja tu kati ya matano ya mtaa mmoja, na kisha mwaanza kushikana uchawi.

Kila mtu ataka kufanya biashara ya aina moja hiyo haiwezekani.
Wrong, ingekuwa hivyo kariakoo hisingeshamiri huko nyuma. BTW kuna brand nyingi zilishindwa kustawi bongo lakini zilipo relocate to neighboring countries zili- flourish. Mfano Game walianzia Tanzania wakaenda Kampala na recently Nairobi , cha kushangaza bongo wamebaki na outlet moja ilhali Nairobi wanafungua outlet ya tatu. Mfano mwingine ni Shoprite, walifunga bongo wakaenda fungua Nairobi.
 
Hata awamu zilizopita hakukuwa na ubunifu,tofauti ni kwamba haukuwa unahitajika sana sababu ulifunikwa na uhalifu, hewa hewa nyingi, madawa ya kulevya nk kwa sasa ubunifu unahitajika sababu ile mianya ya uhalifu iliyofanya ubunifu kuonekana si lolote si chochote umezibitiwa, kama ni pesa utaipata kwa kutumia maarifa (kufikiri kitu tofauti siyo mazoea)..
Dah hii sababu mbona hata Magu alikuja kuikana mpaka akaita wafanya biashara kuongea nao kujua tatizo ni nin?Ile swaga kwamba wapiga deal ndio wanaolalamika haina mashiko tena maana wamejua wafanya biashara halali na haramu wote wanataabika awamu hii!Huo ndio ukweli,hata mabank yanasema uwezo wa watu kukopa na kuweza kurudisha mikopo umeshuka sana!
Huo ndio ukweli!
 
Back
Top Bottom