Kushiriki kila Shughuli za kidini

Kushiriki kila Shughuli za kidini

fimboyaukwaju

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2020
Posts
5,608
Reaction score
7,166
Mimi ni mwislamu na ni mkimya sana,nasali na sijioneshi kabisa na mara nyingi navaa vizuri sana napoenda kusali,mara chache sana huwa navaa kanzu,nashiriki mikutano ya waislamu wenzangu lakini sio muongeaji sana,ila michango natoa.

Sasa marehemu mama yangu ndio alikuwa muislamu lakini alinifundisha kushiriki mikutano ya dini zingine na pia kuchangia. Basi huwa naenda RC,Sabato,KKKT na madhehebu mengine ya Kikristu,mikutano ya mabaniani napo kama kuna kazi nashiriki zote na michango natoa.

Nachofurahi makanisa yote ya kikristu wananijua na wananikubali na huja kwangu mara kwa mara ama kupata ushauri au kijia michango na nafurahia kabisa,na mahusiano mazuri mno na wachungaji,mapadri,masista,na hata viongozi wa dini za wahindi.

Namshukuru sana marehemu mama ambae alikuwa kila mahali yupo.Na Mungu ananitunza sana
 
Safi sana kijana
Mungu hajawahi mtupa mja wake
Ukimtumikia Mungu hakika atakuheshimisha
 
Usitoke ulipo huko mwishoni yajayo yanafurahisha utakata tepe huko peponi mpaka.ufurahi
 
Kasome dini yako ww mzee

21:20

Mayahudi hawawi radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao. Sema: Hakika uwongofu wa Mwenyezi Mungu ndio uwongofu. Na kama ukifuata matamanio yao baada ya ujuzi ulio kwisha kujia, hutapata mlinzi wala msaidizi kwa Mwenyezi Mungu.
 
Mimi ni mwislamu na ni mkimya sana,nasali na sijioneshi kabisa na mara nyingi navaa vizuri sana napoenda kusali,mara chache sana huwa navaa kanzu,nashiriki mikutano ya waislamu wenzangu lakini sio muongeaji sana,ila michango natoa.

Sasa marehemu mama yangu ndio alikuwa muislamu lakini alinifundisha kushiriki mikutano ya dini zingine na pia kuchangia. Basi huwa naenda RC,Sabato,KKKT na madhehebu mengine ya Kikristu,mikutano ya mabaniani napo kama kuna kazi nashiriki zote na michango natoa.

Nachofurahi makanisa yote ya kikristu wananijua na wananikubali na huja kwangu mara kwa mara ama kupata ushauri au kijia michango na nafurahia kabisa,na mahusiano mazuri mno na wachungaji,mapadri,masista,na hata viongozi wa dini za wahindi.

Namshukuru sana marehemu mama ambae alikuwa kila mahali yupo.Na Mungu ananitunza sana
Waisalmu wenzio watakuita wewe kafiri mana uislamu ni dini ya kutenga na kuwachukia wasio waislma
 
Waisalmu wenzio watakuita wewe kafiri mana uislamu ni dini ya kutenga na kuwachukia wasio waislma
hapana hamuna hata muislamu atakayeniita kafir maana nina miaka zaidi ya 15 nipo hivi hivi,waislamu wananiona na hakuna anayenitulana wala kunihoji maana misingi ya dininya kiislamu siivunji.Waislamu sio watu wa hivyo kama unav yodhani wewe
 
Back
Top Bottom