Kusamehe deni la HESLB ni sawa?

Kusamehe deni la HESLB ni sawa?

ni sawa kabisa alivyosema Mgombea wetu. wadaiwa wa heslb watasamehewa madeni ili wafanye kazi kwa amani waweze kulipa kodi ya serikali na kuanza kujenga maisha yao. Ni bahati kwamba msamaha utawakumba hata akina zitto sasa unachopaswa kusema ni kuwashauri akina zitto na ridhiwani wao walipe deni hilo kwa kupeleka fedha hizo kwa jamii kama kununua madawati na vifaa tiba

ukisikia ubepari ndo huu, kumsamehe deni aliyenacho na kumkamua masikini, yaani tumsamehe zitto anaezunguka na mgombea na msururu wa wapambe, ila mamalishe akamuliwe rejesho! Bora tubaki na ccm.
 
Kwa lugha nyingine Lowassa anafanya hata waliotaka kulipa waone kumbe hakuna umuhimu wa kufanya hivyo. Ingawa Lowassa atashindwa uchaguzi huu lakini kauli zake zitazorotesha ulipaji wa mikopo.
 
ukisikia ubepari ndo huu, kumsamehe deni aliyenacho na kumkamua masikini, yaani tumsamehe zitto anaezunguka na mgombea na msururu wa wapambe, ila mamalishe akamuliwe rejesho! Bora tubaki na ccm.

mkuu watanzania ni wapumbavu pamoja na lowasa wao pamoja na kusistiza elimu kumbe hajitambui yeye mwenyewe , nadhani bodi ya mkupo ingeboreshwa zaidi kuwa taasis inayojitegemea ili kuendelea kutoa huduma ya uhakika kwa
vijukuu , na wajukuu wetu
kwa kuhakikisha madeni yanalipwa kumbe wadaiwa watasamehewa hii ni aibu kwa mgombea uraisi
 
mkuu watanzania ni wapumbavu pamoja na lowasa wao pamoja na kusistiza elimu kumbe hajitambui yeye mwenyewe , nadhani bodi ya mkupo ingeboreshwa zaidi kuwa taasis inayojitegemea ili kuendelea kutoa huduma ya uhakika kwa
vijukuu , na wajukuu wetu
kwa kuhakikisha madeni yanalipwa kumbe wadaiwa watasamehewa hii ni aibu kwa mgombea uraisi

hii elimu ya bure watoto wa mabalozi na mawaziri siwatataka wasome havard kwa gharama za serikali? Tunarudi kulekule.
 
Hii ahadi ya kufuta madeni ya wahitimu ni nzuri sana. Lowasa anatakiwa kuisemia hii kwa nguvu kubwa sana. Vijana wengi wasomi watamuunga mkono.
 
Nilitaka nianze kulipa ila baada ya hii kauli itabidi nichukue uamuzi wa ama kulipa au kutolipa baada ya uchaguzi mkuu. Hata baada ya miaka kumi ijayo endapo chadema itaingia madarakani hii itakua agenda kuu hivyo suala la kulipa ni issue. Hiyo hela bora niweke vocha m a m a e
 
Watu wamesamehewa mabilioni ya escrow we unazungumzia vimilioni vya mboga, ahsante lowasa kura ni kwako
 
Watu wamesamehewa mabilioni ya escrow we unazungumzia vimilioni vya mboga, ahsante lowasa kura ni kwako

ujinga nao ni kipaji, wenzenu wanachonga dili nyie mnakenua meno, unajua hela ngapi ilishapigwa?
 
Ni uongo mtupu, ni kitu kisichowezekana. me hapa tu nadaiwa ml 7.8 sa sijui wengine then kwa tz nzima duuh! nchi itafilisika
 
Ni uongo mtupu, ni kitu kisichowezekana. me hapa tu nadaiwa ml 7.8 sa sijui wengine then kwa tz nzima duuh! nchi itafilisika

itakuwa ulisomea udaktari, ila inauma pesa umeitumia na demu baada ya chuo demu katosa kaenda kuolewa na shefa wake, ila ww ndo unakomaa na rejesho, kwa kweli inauma sana, lowasa wapoze machungu jamani.
 
Lowasa alivyokuwa siha alisema wadaiwa wa heslb watasamehewa madeni yao.

Wadaiwa wa heslb ni watu waliosoma chuo kikuu kwa mkopo wa serikali na huanza kulipa baada ya kuhitimu kupata ajira na kuwa na kipato cha uhakika kwa maana ya ajira ya kudumu.

Unaposema watasamehewa najiuliza mtu kama mhandisi daktari meneja wa benki mbunge kama nasari zitto riz1 nao wakumbwe na msamaha huo napata mashaka sana.

Kwanini wasilipe na fedha hizo zikaelekezwa kwenye kuboresha elimu mfano ujenzi miundombinu ya kufundishia? Mabweni ya kisasa na hata kujenga vyuo vipya.

Je, kama watasamehewa hawa watu wenye ajira na vipato vya uhakika kwani wapo wanaolipwa hadi mil kumi kwa mwezi halafu tukimbizane na mamalishe waliokopa nmb dcb na saccos itakuwa sahihi kweli?

Kwanini tusifute madeni yote tuanze moja kama ndo hivyo?

Kodi ya mfanyakazi itapandishwa ambayo atailipa milele kuliko mkopo anaoumaliza akaendelea na maisha yake kalenga mbali mzee huyu lakini hakutaka kumuathiri asiyepata kazi
 
Naongezea swali: Kusamehe matajiri wakubwa kulipa kodi ni sawa? Kusamehe wezi wa mabilioni ya EPA ni sawa? Nyambafu zako,mnakera sana nyie. Sijui unafaidika nini na ccm? Au ni mtoto wa waziri?
 
Wivu ni kitu kibaya sana. Lowassa amesema Elimu itakuwa bora na bure, na wote waliokopeshwa watasamehewa madeni yao, sasa wewe unachukia nini?
Lowassa amesema ataunda serikali rafiki na maskini, akimaanisha maskini wata enjoy sana. Sasa wewe kinakuuma mini?
 
Lowasa alivyokuwa siha alisema wadaiwa wa heslb watasamehewa madeni yao.

Wadaiwa wa heslb ni watu waliosoma chuo kikuu kwa mkopo wa serikali na huanza kulipa baada ya kuhitimu kupata ajira na kuwa na kipato cha uhakika kwa maana ya ajira ya kudumu.

Unaposema watasamehewa najiuliza mtu kama mhandisi daktari meneja wa benki mbunge kama nasari zitto riz1 nao wakumbwe na msamaha huo napata mashaka sana.

Kwanini wasilipe na fedha hizo zikaelekezwa kwenye kuboresha elimu mfano ujenzi miundombinu ya kufundishia? Mabweni ya kisasa na hata kujenga vyuo vipya.

Je, kama watasamehewa hawa watu wenye ajira na vipato vya uhakika kwani wapo wanaolipwa hadi mil kumi kwa mwezi halafu tukimbizane na mamalishe waliokopa nmb dcb na saccos itakuwa sahihi kweli?

Kwanini tusifute madeni yote tuanze moja kama ndo hivyo?

Mikopo ya elimu ya juu ni kodi yako na yangu.

Kusoma bure ni haki yako na yangu.

Huyo mwenye kipato kikubwa analipa kodi kama wengine.

Ni sawa na kukopeshwa kujengewa barabara wakati ni haki yako.

Fikiria...
 
ujinga nao ni kipaji, wenzenu wanachonga dili nyie mnakenua meno, unajua hela ngapi ilishapigwa?

Vaa pajama yako ya kijani ulale bana usinletee ujinga wako mie
Lowasa mabadiliko, mabadiliko lowasaaaa
 
Wivu ni kitu kibaya sana. Lowassa amesema Elimu itakuwa bora na bure, na wote waliokopeshwa watasamehewa madeni yao, sasa wewe unachukia nini?
Lowassa amesema ataunda serikali rafiki na maskini, akimaanisha maskini wata enjoy sana. Sasa wewe kinakuuma mini?

Hawa watu ni wabinafsi sana. Mgombea wao kaahidi elimu bure mpaka form 4! Form 4 ni kitu gani kwa dunia ya leo, si ubinafsi huu!? Dunia ya leo kwa upande wa elimu, at least uwe umesomea fani fulani kwa kiwango fulani ... Sio habari ya sekondari.
 
Hivi haushangai mwanafunzi wa elimu ya juu kupewa mkopo na kampuni ya simu kupewa ruzuku, au kampuni kubwa kupewa tax holiday na mfanyakazi kutakiwa kulipa kodi. Hii ni dhambi hata kwa Mungu.
 
Hii nchi bado tuna mijitu nyoko mingi sana!! Mabilioni kiasi gani watu wamesamehewa sembuse hivi vihela vya mboga? Lowassa songa baba wewe ndo mkombozi wetu! Hivi ulishauliza ni bilioni ngapi zilisharejeshwa tangu bodi ianze kutoa mikopo kwa wanafunzi? Watu wamekaa tu wanakula pesa kama haina mwenyewe, wacha Lowassa aje wakatafute kazi ingine! Nyoko nyie!
 
Back
Top Bottom