Kusamehe au kuacha bora kipi

Kusamehe au kuacha bora kipi

iMind

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
3,157
Reaction score
5,268
Kutokana na uzoefu wangu wa kimaisha na JF naona kama una mchumba au mke mzuri katika mambo mengine ispokuwa ukagundua kuwa ana chepuka solution siyo kumuacha. Maana hata ukipata mwingine possibility kwamba atachepuka ni kubwa. Ila nafikiri ukimsamehe uliyenaye amaweza kutulia na kuacha tabia hiyo na mkaishi kwa amani kwani atajutia matendo yake na kujirekebisha.

Sina uhakika na hili ila nahisi mtu aliye jeruhiwa anajirekebisha. Hasa baada ya kujutia vitendo vyake.

Ushauri wangu ukimfuma mwanamke kwa mara ya kwanza mpe nafasi baada ya kuhakikisha amejutia vitendo vyake na kuahidi kuacha. Mara ya pili ikitokea fukuzia mbali. Jamii ya leo ni ya ajabu. Utaacha wangapi?

Nimejaribu kufikiri hivi kutokana na visa vinavyoletwa hapa JF lila siku. Je solution ni kuacha na kutafuta mwingime.Najaribu kufikiri tu. Nyie mnaonaje
 
Mzinifu mara moja ni mzinifu milele.

Sasa wewe samehe halafu endelea naye mpaka siku atakapokuletea gonjwa la zinaa lisilo na tiba ndo utatia akili.
 
Wanawake huwa twasamehe haraka

Ila wanaume wana mioyo migumu hapo kwenye kusamehe
 
Mpe onyo kama hatarudia tena kwa kipindi kisichopungua miezi sita basi futa kabisa kosa...na akirudia baada ya kufutiwa kosa endelea kuapply kanuni hiyo ya miezi sita sita hadi atimize miaka 60 atakuwa amestaafu kuchepuka!
 
kwa wife sawa naweza kusamehe..ila mchumba,sijui gf haina mjadala hiyo wala kujiuliza mara mbili..
 
kwa wife sawa naweza kusamehe..ila mchumba,sijui gf haina mjadala hiyo wala kujiuliza mara mbili..
Kwa nini usisamehe mchumba? Nafikiri bora usamehe. Si unajua zimwi likujualo...
 
Mzinifu mara moja ni mzinifu milele.

Sasa wewe samehe halafu endelea naye mpaka siku atakapokuletea gonjwa la zinaa lisilo na tiba ndo utatia akili.
Binafsi nilisha samehewa. Na ukweli nilibadilika baada ya kusamehewa. Fikra zangu ni kwamba mtu akisamehewa anajirekebisha especially kama kuchepuka kwake ilikuwa ni kwa kujaribu tu. Ila kama kuchepuka kwake ni kutokana na upungufu fulani kwenye uhusiano wenu basi pengine ni vyema kuzungumza na kurekebisha upungufu huo kama una rekebishika. Kama upungufu uliosababisha achepuki haurekibishiki basi ni vyema kumwaga manyanga.
 
Ikishakuwa Ni issue ya trust, basi tegemea lolote kusamehewa au kutokusamehewa. Sio kwamba watu hawataki kusamehe, Ni kwa sababu trust imevunjwa na huwezi jua uliyemsaliti alikuamini kwa kiasi gani. Ninaweza kuwish Kabisa kukusamehe ila nisiweze kukuamini tena. Na hakuna mahusiano yoyote Yale, Kama Trust Haipo. So ukienda kucheat, nenda tu at your own risk. Ukiachika usije leta za kujiliza na Kumsingizia shetani Kuwa alikupitia.
 
Najuta kutosamehe.

I moved on, miez kadhaa imepita nimepata mtu ndiyo but bado naona kuna kosa nilifanya kwa kuto kumsamahe.

Ukizingatia kuwa mimi nilichepukaga na akagundua na tukaendelea japo alikuwa na kinyongo bt hakukionesha waziwazi had alipokuja kulipiza.

Sometimes ni bora tu kusamehe
 
Back
Top Bottom