Kusafiri kwenda Ghana kunahitaji Visa?

Kusafiri kwenda Ghana kunahitaji Visa?

MamaZion

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2023
Posts
248
Reaction score
280
Habari waungwana, kama kichwa cha habari kisemavyo.

Je, kuna uhitaji wa mimi Mtanzania kuwa na Visa iwapo nataka kwenda Ghana? Naelewa kuwa hatuna ubalozi hapa nchini ila sijui nchi zetu zina makubaliano gani.
 
Habari waungwana, kama kichwa cha habari kisemavyo.

Je, kuna uhitaji wa mimi Mtanzania kuwa na Visa iwapo nataka kwenda Ghana? Naelewa kuwa hatuna ubalozi hapa nchini ila sijui nchi zetu zina makubaliano gani.
Huhitaji VISA, ni passport yako tu mkuu. Kama utahitaji tips zaidi nicheki, nina connections zangu huko.
 
Aisee Ghana kuna malaria sana.. ukikaa vibaya unaweza kula malaria mara 2 ndani ya mwezi mmoja.
 
Habari waungwana, kama kichwa cha habari kisemavyo.

Je, kuna uhitaji wa mimi Mtanzania kuwa na Visa iwapo nataka kwenda Ghana? Naelewa kuwa hatuna ubalozi hapa nchini ila sijui nchi zetu zina makubaliano gani.
Hapana,visa utagongewa hapohapo ukitua fhana mimi nimesafiri wiki iliyopita sikudaiwa visa
 
Asante sana. Nilisoma mtandaoni kuwa wanahitaji kuona bank statement yako isije ikawa unataka kuzamia. Je ni kweli inabidi niandae hiyo kitu?
 
Asante sana. Nilisoma mtandaoni kuwa wanahitaji kuona bank statement yako isije ikawa unataka kuzamia. Je ni kweli inabidi niandae hiyo kitu?
Hakuna atakaekuuliza mambo ya bank statement mkuu. Cha msingi uwe tu na barua ya mwaliko either kutoka kwa ofisi ambayo imekualika Ghana (kwa mkutano au kikao, etc), au uwe na barua ya mwaliko kutoka kwa mtu alieko Ghana ambae anakualika umtembelee, na pia uwe na return ticket. Tena hivyo vitu pale Airport ya kwetu ndo watakusumbua kukuulizia uwaonyeshe. Ukifika huku watu wao wa immigration hawana shida na Watanzania kabisa, mimi nilivyotua Accra watu wao wa immigration waliniuliza umekuja kufanya nini huku, nikajibu kiutani nimekuja huku nioe mwanamke wa Ghana maana ni wazuri sana, nawapenda. Jamaa akacheka vibaya sana, akagonga passport yangu mhuri, tena kanipa full 60 days!!
 
Back
Top Bottom