Elections 2010 Kura za mbunge zinabebwa kwenye sahani ya chakula je za rais?

Mungi

JF Gold Member
Sep 23, 2010
16,975
9,566
Jana nilisoma gazeti la mwananchi likidai msimamizi wa uchaguzi jimbo la segerea alikamatwa akitoka kununua chakula, alipopekuliwa alikutwa na nyara za tume ya uchaguzi, ikiwa pamoja na mihuri pamoja na makaratasi ya kura.

Sasa kama kura za mbunge zinabebwa kwenye hotpot ya wali je ya rais itakuwaje? CCM waizi wa kura, hakuna uhalali wa kura zinazoendelea kutangazwa.

Labda tukubali tu kuongozwa na viongozi tusiowachagua kwa ajili ya kuepusha vurugu. Vilevile katika mazingira kama haya, hakuna cha kuogopa, maana haki haipatikani kirahisi, mpaka itumike gharama.

Tuwasikilizie ndg zetu CHADEMA wana maoni gani kuhusu mustakbali wa nchi hii.
 
Back
Top Bottom