Katika uchaguzi mkuu uliopita kura yangu niliigawa kama ifuatavyo: Kura ya urais nilimpa mgombea wa CUF, Ibrahimu Lipumba kwa kuwa ninaamini ni bora kuliko wote. Kwa upande wa Ubunge nilimpa mgombea wa CCM ambaye ninaamini ni chagua bora kabisa na kwa upande wa udiwani nilimpa mgombea wa CDM ambaye kwa ujumla ni ni bora yawezekana kuliko diwani yeyote niliyepata kumwona. Binafsi nilikuwa sichagui chama kwa kuwa ninaamini uadilifu wa mtu hautokani na imani yake katika chama, uadilifu wa mtu ni mtu mwenyewe na roho yake.