Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Muundo upi wa Muungano unafaa?

  • Serikali 1

    Votes: 81 23.3%
  • Serikali 2

    Votes: 22 6.3%
  • Serikali 3

    Votes: 241 69.5%
  • Sijui

    Votes: 3 0.9%

  • Total voters
    347
  • Poll closed .
ndugu wana jamvi Nawapenda sana!! katika pitapita zangu maeneo ya mjini leonikapita kwenyekijiwe kimoja cha DRAFT nikakuta watu wengi wakicheza,kama kawaida yangu nikachokoza mada juu ya muundo wa muungano wengi walipendekeza serekali tatu wenye rais mmoja na mawaziri wakuu wawili na wachache walitaka serekali mbili wenye rais wa zanziber na rais wa jamuhuri wa muungano wa TZ baada ya mabishano ya masaa kadhaa aliibuka mzee mmoja rafiki yangu na kutoa suluhisho alisema hivii!! kwa kuwa kura ya wazi na siri zinatumika kwa wakati mmoja bungeni ikijulikana kwa jina la kura ya SIRI WAZI mzee huyu nae alipendekeza Mifumo yote miwili ya serekali mbili na serekali tatu zitumike kwa pamoja kwani CCM wanabishana na maoni ya waTZ nilicheka sana nikasema huenda bunge maalum la katiba linaweza kuja na suluhisho hilo.maana mhhhhhhhh! bunge lina vihoja hili we acha tu.
 
Baada ya miaka hamsini ya muungano ambao una serikali mbili ya muungano na ya zanzibar basi sasa ni wakati muafaka kupitia katiba mpya kurekebisha kidogo style ya serikali, kuwepo na serikali mbili lakini ziwe ya tanganyika na ya muungano hapo ndo kero zote za muungano zitaisha.

Kula like kaka!
 
Huenda sifahamu kitu hapo,, uchaguzi wa serikali.moja mbili au tatu si ilikuwa wakati wa kukusanya maoni yaliofamywa na tume ya warioba?!?! Sasa BMK si nikuboresha rasimu tu na si kuanza batilisha maoni ya waliowengi?! Nilitegemea sana kuona hili BMK kufanya uboreshaji wa yaliyomo ktk rasimu...so waboreshe hizo serikali tatu zilizopendekezwa na watz...ziwe za namna gani...na si kupenyeza misimamo yao pasipo zingatia ya watanzania..kwa kufanya hivyo inakuwa ni kudharau kazi iliyofanya na Tume ya Warioba.
 
Kumekuwa na wanaotaka serikali moja, mbili na tatu lakini hizi serikali hazitafanikiwa kama Watanzania wengi wamechoka muungano na wanataka tuwe na nchi mbili tofauti. Je leo hii tukiweka kwenye kura za maoni kama Watanzania wanataka muungano mimi naona kama Watanzania wengi watachagua muungano ufe kwani Wabara wengi wanaona wanatumiwa tu na Wanzanzibar wengi wanaona watapata faida zaidi bila muungano. Tatizo kubwa sana ni viongozi wa Zanzibar kwasababu ndiyo wanaonufaika na muungano kuliko kikundi kingine chochote na wnasingizia muungano kwa utendaji kazi wao duni.Pesa yote inaishia kuwatunza viongozi Zanzibar
 
Sawa kabisa kama hii katiba ni yawatanzania watanzania walisha toa maoni iweje sasa nashangaa na kuna wananchi ambao hawakutoa maoni yao mwanzoni na sasa wanakwenda kupangua na kuwaka yakwao,kwa maslahi yao na yavyama vyao,jamani tuiombee sana nchi yetu.
 
mimi kama mzanzibari nataka zanzibari yangu kama tanganyika munaulazima wa kuungana zipo nchi kama kongo ,Ruanda,majirani zenu Kenya. tena hao Kenya mpaka mlima kilimanjaro munashea.Zanzibar kwanza.
 
nini faida ya kuvunja muungano na nini faida ya kuuacha muungano.. ikiwa tayari wanzanzibari wameshazaa na watanganyika naikiwa muungano wa inchi utavunjwa vipi kuhusu hizi familia zilizo ungana nazo zitavunjwa...
 
Kumekuwa na wanaotaka serikali moja, mbili na tatu lakini hizi serikali hazitafanikiwa kama Watanzania wengi wamechoka muungano na wanataka tuwe na nchi mbili tofauti. Je leo hii tukiweka kwenye kura za maoni kama Watanzania wanataka muungano mimi naona kama Watanzania wengi watachagua muungano ufe kwani Wabara wengi wanaona wanatumiwa tu na Wanzanzibar wengi wanaona watapata faida zaidi bila muungano. Tatizo kubwa sana ni viongozi wa Zanzibar kwasababu ndiyo wanaonufaika na muungano kuliko kikundi kingine chochote na wnasingizia muungano kwa utendaji kazi wao duni.Pesa yote inaishia kuwatunza viongozi Zanzibar

Aswaaaaaa tusilazimishwe. binafsi muungano siutaki.
 
Serikali 2 ndo mpango mzima! Tukiendekeza 3 Serikali ya Muungano itakuwa haina hata ardhi (ardhi si suala la Muungano) na itakuwa ombaomba kwa nchi washirika kwa kuwa haina vyanzo vya mapato vya kwake!
Ardhi ya serikali ya muungano ni hipi kwa sasa?kumbuka Zanzibar wana Ardhi yao
 
Serikali moja...na kuwe mgawanyo wa mdaraka kwamba rais akitoka tz visiwan msimu huu msimu mwingine atoke tz bara...pia tuwe na bunge moja...jeshi moja, wimbo mmoja wa taifa, kwa kifupi iwe nchi moja huru bila kujali Utanganyika wala Uzanzibar....tuta step up...ni mtazamo tu
 
Daaah mm naona serikari mbili ndio nzuri

Bro #willy ishu ni kwamba ndugu zetu wa visiwani wana katiba yao ya mwaka 2010 ambayo tayari imeshapoteza maana ya muungano na kwa katiba hiyo Zanzibar inajitambulisha kama nchi yenye mipaka yake rasmi...

Na ukifuatilia katika ibara yake ya 1, 6 na 80 zinakinzana kabisa na katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na kutokana na hayo ndiyo maana inapendekezwa Serikali tatu ili na Tanganyika iwe na mamlaka yake kamili kama ilivyo zenji.

Na kama wakitaka Serikali mbili hakuna budi zenji wavunje katiba yao kwasababu wana bendera na nyimbo ya taifa piaaa...
 
Hilo ndilo swara tunayotaka ss wananchi katiba nzuri na pia wabunge malumu was Anglia upended wote na watoe mahamuzi ya pamoja na sio kununuliwa na watu baadhi!! Hilo ni mawazo yangu
 
serkal 2 ili kuepusha kuvunja muungano siku za usoni

Kwani sasa ulipo unakusaidia nini/ haujui muungano ni kwa ajili ya ajira za viongozi tu. Nipe sababu za muungano kuvunjika tunaathirika vipi. Mbayuayu alisha sema changanya na akili zako kidogo usisharadie mawazo ya watu!
 
Kuna watu wengine humu ndani sijui hata kama wanafuatilia huu mchakato mzima wa katiba kwasababu kuna mambo ya msingi sana ya kutazamwa katika Serikali mbili na Serikali tatu lakini mtu anaandika Serikali mbili or tatu au kumpinga mwingine bila ya kuwa na hoja ya msingi.

Kabla ya kuja humu ndani kuchangia hakikisha unafuatilia hata kidogo jinsi huu mchakato unavyokwenda utainjoi kinoma vinginevyo utakua bendera fuata upepo tuuuu dailyyyy
 
Back
Top Bottom