Magu
Senior Member
- Jun 13, 2011
- 156
- 56
Wana JF nawaombeni msaada wenu, kuna rafiki yangu kaja kuomba ushauri kwangu, kiasi sijampa ushauri unaotakiwa mana nimechanganyikiwa na mimi pia. Huyu jamaa yangu anadai kuwa anapotaka kufanya mapenzi na mke wake wa ndoa anapoteza hamu na anashindwa kabisa kutekeleza wajibu huo mhimu ktk ndoa. Lakini baada ya tatizo kuonekana linakuwa kubwa akaamua kujaribu nje ya ndoa kama je pia itashindikana? Kule nje anaweza piga hata 3 hadi 4 kwa siku, ila anapokuja nyumbani mchezo ni ule ule!!! Kinachompa mashaka si kuwa uko nje ana mwanamke wa permanent ambaye anaweza kumhisi kumfanyia mambo ya kinyamwezi 'limbwata' ili kuvuruga ile ndoa ahamie kwake. Anapotaka kupeleka hisia kwa mke kuwa labda ndo anafanya mambo hayo ili asi function pia haiji akilini mana haoni sababu! Je nimshauri nini huyu rafiki yangu? Naombenini msaada ndg zangu