The Khoisan
JF-Expert Member
- Jun 5, 2007
- 15,394
- 12,978
Wabunge waikaanga TRA kuporomoka kwa uchumi Send to a friend Tuesday, 15 March 2011 20:54 0diggsdigg
Leon Bahati
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imesema matatizo ya mgawo wa umeme nchini imesababisha kupoteza Sh295 bilioni katika makadirio ya makusanyo ya Sh3,686 bilioni kwenye kipindi cha miezi minane iliyopita.
Akizungumza kwenye semina ya wabunge inayoendelea jijini Dar es Salaam jana, Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Placidus Luoga, miongoni mwa sababu zilizopelekea kushuka kwa mapato ni mgawo wa umeme.Semina hiyo ina lengo la kushauri serikali jinsi ya kukabiliana na kupanda kwa gharama za maisha, uhaba wa nishati ya umeme na njia za kubuni vyanzo vingine vya mapato.
"Katika kipindi cha Julai 2010 hadi Februari mwaka huu, makusanyo yalikuwa ni Sh3,391 bilioni wakati matarajio yalikuwa Sh3,686 bilioni. Hayo ni mafanikio ya asilimia 64 ya matarajio ya kukusanya Sh5,652.6 bilioni kwa mwaka huu wa fedha 2010/11," alisema Luoga.
Luoga alisema TRA imeweka mikakati kuhakikisha katika miezi minne iliyobaki mwaka huu wa fedha unaoishia Julai, kiwango cha makusanyo ya Sh5,652 kinafikiwa. Hata hivyo, wabunge waliishambulia TRA kwa uzembe wa masuala mbalimbali, ikiwamo kushindwa kukusanya kodi ipasavyo kwenye sekta ya madini, misamaha ya kodi na rushwa miongoni mwa wafanyakazi wake.Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Kabwe Zitto, alisema mwaka wa fedha uliopita 2009/10, serikali ilipoteza Sh630 bilioni kutokana na misamaha ya kodi.
Zitto alilalamika kuwa, hasara hiyo ilichangiwa na misamaha ya kodi kwa wawekezaji sekta ya madini.
Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Magdalena Sakaya, alisema ukwepaji mkubwa wa kodi unafanywa na wawekezaji kwa kubadilisha majina kila baada ya miaka mitatu, unafanywa kutokana na udhaifu wa sheria.
Matatizo mengine yaliyolalamikiwa na wabunge ni urasimu unaofanywa na watumishi wa TRA na kusababisha wafanyabiashara kukwepa Bandari ya Dar es Salaam, tofauti ya kodi Zanzibar na Tanzania Bara, kodi kubwa kwenye mishahara ya wafanyakazi na kushindwa kukusanya kodi kwa Wamachinga.
Lakini, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tindu Lisu, alitofautiana na wenzake akisema, lawama hizo hazipaswi kutupiwa TRA bali ni wabunge waliotunga sheria dhaifu za ukusanyaji kodi mwaka 1997.
"Kuwapo na kiwango kikubwa cha msamaha wa kodi wanaopaswa kulaumiwa ni wabunge sio TRA," alisema Lisu na kuongeza:"Kwa mfano mwaka jana sekta ya madini iliingiza Sh7.2 trilioni, lakini makusanyo ya kodi yalikuwa ni Sh283 milioni. Ukiangalia hapa utaona asilimia 94 ya utajiri wa Tanzania ulienda nje kutokana na tatizo la Bunge hili."
Mwenyekiti wa semina hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Dk Abdallah Kigoda, alisema msamaha wa kodi Kenya na Uganda ni asilimia moja wakati Tanzania inafikia asilimia mbili.
Source: Mwananchi
My take: Huwa nashangaa ninaposikia kuwa mashirika yanatumia ujanja kukwepa kodi kwa kutumia sheria dhaifu iliyopo. Sasa kama washalijuwa hilo kwa nini wasibadilishe sheria??? Hizo pesa wanazopoteza kutokana na mgao wa umeme zingeweza kununua magenarator mangapi???
Cha kushangaza, wabunge wote hawalioni hilo (pamoja na our own Brilliant Zitto) except Lissu!! Sheria na poor policy, lawama kwa TRA!!
Leon Bahati
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imesema matatizo ya mgawo wa umeme nchini imesababisha kupoteza Sh295 bilioni katika makadirio ya makusanyo ya Sh3,686 bilioni kwenye kipindi cha miezi minane iliyopita.
Akizungumza kwenye semina ya wabunge inayoendelea jijini Dar es Salaam jana, Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, Placidus Luoga, miongoni mwa sababu zilizopelekea kushuka kwa mapato ni mgawo wa umeme.Semina hiyo ina lengo la kushauri serikali jinsi ya kukabiliana na kupanda kwa gharama za maisha, uhaba wa nishati ya umeme na njia za kubuni vyanzo vingine vya mapato.
"Katika kipindi cha Julai 2010 hadi Februari mwaka huu, makusanyo yalikuwa ni Sh3,391 bilioni wakati matarajio yalikuwa Sh3,686 bilioni. Hayo ni mafanikio ya asilimia 64 ya matarajio ya kukusanya Sh5,652.6 bilioni kwa mwaka huu wa fedha 2010/11," alisema Luoga.
Luoga alisema TRA imeweka mikakati kuhakikisha katika miezi minne iliyobaki mwaka huu wa fedha unaoishia Julai, kiwango cha makusanyo ya Sh5,652 kinafikiwa. Hata hivyo, wabunge waliishambulia TRA kwa uzembe wa masuala mbalimbali, ikiwamo kushindwa kukusanya kodi ipasavyo kwenye sekta ya madini, misamaha ya kodi na rushwa miongoni mwa wafanyakazi wake.Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Kabwe Zitto, alisema mwaka wa fedha uliopita 2009/10, serikali ilipoteza Sh630 bilioni kutokana na misamaha ya kodi.
Zitto alilalamika kuwa, hasara hiyo ilichangiwa na misamaha ya kodi kwa wawekezaji sekta ya madini.
Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Magdalena Sakaya, alisema ukwepaji mkubwa wa kodi unafanywa na wawekezaji kwa kubadilisha majina kila baada ya miaka mitatu, unafanywa kutokana na udhaifu wa sheria.
Matatizo mengine yaliyolalamikiwa na wabunge ni urasimu unaofanywa na watumishi wa TRA na kusababisha wafanyabiashara kukwepa Bandari ya Dar es Salaam, tofauti ya kodi Zanzibar na Tanzania Bara, kodi kubwa kwenye mishahara ya wafanyakazi na kushindwa kukusanya kodi kwa Wamachinga.
Lakini, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tindu Lisu, alitofautiana na wenzake akisema, lawama hizo hazipaswi kutupiwa TRA bali ni wabunge waliotunga sheria dhaifu za ukusanyaji kodi mwaka 1997.
"Kuwapo na kiwango kikubwa cha msamaha wa kodi wanaopaswa kulaumiwa ni wabunge sio TRA," alisema Lisu na kuongeza:"Kwa mfano mwaka jana sekta ya madini iliingiza Sh7.2 trilioni, lakini makusanyo ya kodi yalikuwa ni Sh283 milioni. Ukiangalia hapa utaona asilimia 94 ya utajiri wa Tanzania ulienda nje kutokana na tatizo la Bunge hili."
Mwenyekiti wa semina hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Dk Abdallah Kigoda, alisema msamaha wa kodi Kenya na Uganda ni asilimia moja wakati Tanzania inafikia asilimia mbili.
Source: Mwananchi
My take: Huwa nashangaa ninaposikia kuwa mashirika yanatumia ujanja kukwepa kodi kwa kutumia sheria dhaifu iliyopo. Sasa kama washalijuwa hilo kwa nini wasibadilishe sheria??? Hizo pesa wanazopoteza kutokana na mgao wa umeme zingeweza kununua magenarator mangapi???
Cha kushangaza, wabunge wote hawalioni hilo (pamoja na our own Brilliant Zitto) except Lissu!! Sheria na poor policy, lawama kwa TRA!!