QEEN ADEMU1
Senior Member
- Dec 24, 2019
- 134
- 324
[emoji2771]Leo naomba kuuliza Wanandoa waliopo humu, hata wale ambao bado mabaharia mnakaribishwa Sana maana nyie ndio wahanga wakubwa wa hili suala. Mwanzoni munakuwa na mapenzi makubwa kwa wenza wenu lakini baadaye mambo yanaharibika.
[emoji2771]Kwanini wakati wa mwanzo wa mahusiano mnakua very romantic mpaka mnapelekea Ndoa, na baada ya Ndoa wengine hata mwaka hujaisha wameshaanza mipango ya kando na wanabadilika kabisaaa, mapenzi hakuna -- yaani "wanabakana" kwenye Ndoa zao.
[emoji2771]Hao hao Wanandoa kila mmoja akipata mchepuko nje anafanya vizuri lakini akija kwa Mume wake au Mke wake wanaishi kama wazee.
[emoji2771]Hakuna mahaba, hata jumbe tamu za maneno tu. Huwezi kuta Wanandoa wanaongea mambo ya Mapenzi, sana sana ni mambo ya Karo za shule za Watoto , Kodi ya nyumba nakadhalika. Hakuna hata Nakupenda Mpenzi, hakuna mashamsham , yalishaisha kitambo.
[emoji2771]Ndio maana Wanawake japo sio wote wanajitahidi kutafuta Makungwi na kujiunga kwenye magroup ya WhatsApp wanafundishwa namna na kumshika Mwanaume akupende, na Mwanaume naye japo sio wote yuko busy kushinda kwenye mitandao ya kijamii kutafuta company na Marafiki wa Kike.
[emoji2771]Yaani upendo umepoa kabisaa. Yale malovee hakuna kabisa kwenye Ndoa zetu. Kabla hamjaoana mlikuwa mnapeana raha mnaridhishana lakini baada ya mwaka mnabaniana unyumba au unapewa kwa masharti huku mkishindwa kuridhishana. Shida nini hapo Wanandoa[emoji780]
Wanandoa , najua wengi wapo humu na wahanga wa hili tatizo. Je, shida ni nini[emoji780]
Tunaomba Mwanaume mfunguke kero zenu na Wanawake wenzangu mfunguke kero zenu ili 2020 tujenge familia bora.
Ndoa bila usaliti, inawezekana. Karibuni[emoji779]
[emoji3590]Ndoa na IHESHIMIWE NA WATU WOTE [emoji120] NA MALAZI YAWE SAFI [emoji120] MAANA WAASHERATI NA WAZINZI MUNGU [emoji120] ATAWAHUKUMIA adhabu (Waebrania 13: 4)
Sent using i phone x
[emoji2771]Kwanini wakati wa mwanzo wa mahusiano mnakua very romantic mpaka mnapelekea Ndoa, na baada ya Ndoa wengine hata mwaka hujaisha wameshaanza mipango ya kando na wanabadilika kabisaaa, mapenzi hakuna -- yaani "wanabakana" kwenye Ndoa zao.
[emoji2771]Hao hao Wanandoa kila mmoja akipata mchepuko nje anafanya vizuri lakini akija kwa Mume wake au Mke wake wanaishi kama wazee.
[emoji2771]Hakuna mahaba, hata jumbe tamu za maneno tu. Huwezi kuta Wanandoa wanaongea mambo ya Mapenzi, sana sana ni mambo ya Karo za shule za Watoto , Kodi ya nyumba nakadhalika. Hakuna hata Nakupenda Mpenzi, hakuna mashamsham , yalishaisha kitambo.
[emoji2771]Ndio maana Wanawake japo sio wote wanajitahidi kutafuta Makungwi na kujiunga kwenye magroup ya WhatsApp wanafundishwa namna na kumshika Mwanaume akupende, na Mwanaume naye japo sio wote yuko busy kushinda kwenye mitandao ya kijamii kutafuta company na Marafiki wa Kike.
[emoji2771]Yaani upendo umepoa kabisaa. Yale malovee hakuna kabisa kwenye Ndoa zetu. Kabla hamjaoana mlikuwa mnapeana raha mnaridhishana lakini baada ya mwaka mnabaniana unyumba au unapewa kwa masharti huku mkishindwa kuridhishana. Shida nini hapo Wanandoa[emoji780]
Wanandoa , najua wengi wapo humu na wahanga wa hili tatizo. Je, shida ni nini[emoji780]
Tunaomba Mwanaume mfunguke kero zenu na Wanawake wenzangu mfunguke kero zenu ili 2020 tujenge familia bora.
Ndoa bila usaliti, inawezekana. Karibuni[emoji779]
[emoji3590]Ndoa na IHESHIMIWE NA WATU WOTE [emoji120] NA MALAZI YAWE SAFI [emoji120] MAANA WAASHERATI NA WAZINZI MUNGU [emoji120] ATAWAHUKUMIA adhabu (Waebrania 13: 4)
Sent using i phone x