Kupima DNA liwe suala la lazima

Ngao ya Sponji

JF-Expert Member
Jul 26, 2018
341
541
Kwa Dunia ilipofikia Sasa Swala la KUPIMA DNA linapaswa liwe ni swala la Lazima Ili Kumlimda Baba, Mama na Mtoto kwa Ujumla.

Usipojua uhalali wa uhusiano wa Damu katika familia Yako inakuweka hatarini kupoteza kizazi Chako na pengine wewe ndio unaweza ukawa Mtu mwa mwisho katika kizazi Chako Kuishi maana utakua huna mtoto wa kuendeleza Damu Yako ya Asili.

Kila mtoto au Kila Mzazi anapswa kuwa na hakika Juu ya Uhalali wa Zao lake au Damu yake katika familia, na Inapaswa kisheria kumchukulia Hatua Kali Kwa yoyote atayepotosha Taarifa za Uzazi na kupelekea Familia kuishi na zao lisilokua la kwao

Ni mara chache sana hutokea Kwa Mwanamke bila kujua/kutofahamu ukweli Juu ya baba halisi wa mtoto na Hivyo kupelekea Naye kuongezwa kwenye kundi hili la waathiriwa wa Tatizo Hili.

Takwimu zinaonyesha Baba na mtoto ndio waathirika wakubwa wa janga hili la kubebeshwa damu zisizo za kwao Huku Mwanamke akiendelea kuinjoy ilihali akijua Hilo ni kosa mbele ya Sheria lakini pia mbele za Mungu.

Kwanini nasema DNA ni lazima?

Kuna Kesi nyingi sana za watoto kubadilishwa mahospitalini, Kwa sababu Moja au nyingine Kwa watu walio na nia ovu, kabla ya Wazazi kuondoka na mtoto wao Nyumbani ni lazima apimwe DNA kuhakikisha uhalali huo.

Lakini pia Kuhakikisha kwamba mtoto huyo ni Mali Halali ya Baba. kila Mtu abebe msalaba wake, Kama Mwanamke alipewa Mimba tofauti na Mwanaume aliyenaye basi Mwanaume huyo ahusike katika kulea mtoto wake, Gharama zote ziwe Juu yake isipokua Kwa MAKUBALIANO MAALUMU TU.

DNA IWE NI LAZIMA ILI KULINDA HESHIMA YA BABA NA FAMILIA KWA UJUMLA.
 
Kwani wewe una umuhinu gani sana wa zaidi mpaka iwe lazima kizazi chako wewe tu ndiyo kiendelee?

Na hata kama wewe unaona hilo ni jambo la muhimu sana, kwa nini unafikiri kila mtu anaona hilo ni jambo la muhimu hivyo hivyo?

Hujasikia India kuna mtoto kawashitaki wazazi wake kwa kuwahoji kwa nini wamemzaa kwenye dunia hii yenye matatizo mengi bila yeye kuridhia?

Kama unaona heshima ya baba inalindwa kwa DNA, kitu ambacho mnyama yeyote anaweza kutimiza, wewe una tofauti gani na mnyama?
 
Kwani wewe una umuhinu gani sana wa zaidi mpaka iwe lazima kizazi chako wewe tu ndiyo kiendelee?

Na hata kama wewe unaona hilo ni jambo la muhimu sana, kwa nini unafikiri kila mtu anaona hilo ni jambo la muhimu hivyo hivyo?

Hujasikia India kuna mtoto kawashitaki wazazi wake kwa kuwahoji kwa nini wamemzaa kwenye dunia hii yenye matatizo mengi bila yeye kuridhia?

Kama unaona heshima ya baba inalindwa kwa DNA, kitu ambacho mnyama yeyote anaweza kutimiza, wewe una tofauti gani na mnyama?
Kwanza kukujibu hoja zako nianze Kwa kusema Binadamu Kiasili ni Mnyama, kinachotutofautisha ni features. Kila Mnyama ana Kila kitu ambacho Binadamu anacho utofauti ni katika ufanyaji kazi na Muonekano.

Pili sijasema kizazi changu ni Muhimu kuliko Cha Mtu yoyote Bali nimeongea Kwa Ujumla. Kuna haja Gani ya kwenda Kujamiiana Kwa mrengo wa kutafuta mtoto halafu Mwisho wa siku ukapewa mtoto ambaye si wako? Muda na Nguvu zote hizo ni Bora ungeziwekeza Pengine. Umetumia Gharama za kuhudumia Mimba, Kutoa Ushauri na kuumia kisaikolojia for what??? Kama umeamua kupoteza Mali zote Hizi kutafuta mtoto ni Lazima Mwisho wa Siku Uhakikishe Unatumia Kipimo Cha DNA kujiridhiaha na Matokeo ya Kazi yako.
 
Naunga mkono hoja! Ila Kuna kabila fulani lenye hasira za chapchap, akigundua mtoto sio wake ni shughuli, ndio maana kuna ulazima wa kudanganya ili kulinda usalama wa mama na mtoto. Huo niite "uwongo mtakatifu". Kwa sasa tuendelee na kujiliwaza na kausemi "kitanda hakizai haramu"
 
Nashauri itumike DNA Pori ambayo haina gharama!

Chukua ungo wa zamani uweke juani kisha mchukue mtoto mchanga muweke kwenye ungo kama unamuanika akiangalia juu!
Baba mwenye shaka na mtoto amfunike na kivuli chake kisha amuite mtoto kwa jina la bibi yake mzaa baba!
Mtoto kama damu yako ATATABASAMU! Kama sio damu yako ATAKUFA!
NB!; KAMA UNA MASHAKA MTOTO SIO WAKO USIJARIBU!
 
Nashauri itumike DNA Pori ambayo haina gharama!

Chukua ungo wa zamani uweke juani kisha mchukue mtoto mchanga muweke kwenye ungo kama unamuanika akiangalia juu!
Baba mwenye shaka na mtoto amfunike na kivuli chake kisha amuite mtoto kwa jina la bibi yake mzaa baba!
Mtoto kama damu yako ATATABASAMU! Kama sio damu yako ATAKUFA!
NB!; KAMA UNA MASHAKA MTOTO SIO WAKO USIJARIBU!
Tusifike Huko Mkuu, Uhai ulindwe Kwa Gharama yoyote Ile lakini Damu zijulikane na mwenye uhalali apewe kilicho chake.
 
Kwanza kukujibu hoja zako nianze Kwa kusema Binadamu Kiasili ni Mnyama, kinachotutofautisha ni features. Kila Mnyama ana Kila kitu ambacho Binadamu anacho utofauti ni katika ufanyaji kazi na Muonekano.

Pili sijasema kizazi changu ni Muhimu kuliko Cha Mtu yoyote Bali nimeongea Kwa Ujumla. Kuna haja Gani ya kwenda Kujamiiana Kwa mrengo wa kutafuta mtoto halafu Mwisho wa siku ukapewa mtoto ambaye si wako? Muda na Nguvu zote hizo ni Bora ungeziwekeza Pengine. Umetumia Gharama za kuhudumia Mimba, Kutoa Ushauri na kuumia kisaikolojia for what??? Kama umeamua kupoteza Mali zote Hizi kutafuta mtoto ni Lazima Mwisho wa Siku Uhakikishe Unatumia Kipimo Cha DNA kujiridhiaha na Matokeo ya Kazi yako.
Mkuu,

Kwa nini unajiona wewe ndiye mwenye maoni sahihi mpaka ulazimishe wengine kupima DNA, wakati wengine hawaamini hivyo, wanaamini undugu ni kufaana, si kufanana?

Kwa maoni yako ya DNA hayo, ina maana watu wasilee watoto wa kufikia? Wasifanye adoption? Wasisaidie watu wasio wa DNA yao?

Kasome "Lady Chatterley's Lover", uone mtu anavyotafuta kuendeleza jina la ukoo wake hata pale aliposhindwa kupata mrithi wa kibaiolojia, tena kwa mume kumbembeleza mke aende kufanya mambo na mwanamme mwingine.

Unaelewa huko Ugiriki kushakuwa na jamii ya watu ambao watoto na wake walikuwa ni wa pamoja?

Yani kama mimi na wewe ni vijana wa kiume wa rika moja, basi wanawake wote wa rika moja ni wake zetu na watoto wote wa rika la kuwa watoto zetu ni watoto zetu, hakuna ubinafsi wa kusema huyu mke wangu na huyu mtoto wangu.

Yani baba ukirudi mjini unaingia nyumba yoyote ambayo haina baba, unamkuta mwanamke ni mke wako, unawakuta watoto ni watoto wako. Ukiondoka akija mwenzako naye vilevile. Mnapokezana majukumu tu.

Na watu waliishi poa tu.

Unaelewa hilo? Au haya ni kati ya yale mambo ambayo hujui kama Watanzania wengi kwa uvivu wa kusoma?
 
Kwa Dunia ilipofikia Sasa Swala la KUPIMA DNA linapaswa liwe ni swala la Lazima Ili Kumlimda Baba, Mama na Mtoto kwa Ujumla.

Usipojua uhalali wa uhusiano wa Damu katika familia Yako inakuweka hatarini kupoteza kizazi Chako na pengine wewe ndio unaweza ukawa Mtu mwa mwisho katika kizazi Chako Kuishi maana utakua huna mtoto wa kuendeleza Damu Yako ya Asili.

Kila mtoto au Kila Mzazi anapswa kuwa na hakika Juu ya Uhalali wa Zao lake au Damu yake katika familia, na Inapaswa kisheria kumchukulia Hatua Kali Kwa yoyote atayepotosha Taarifa za Uzazi na kupelekea Familia kuishi na zao lisilokua la kwao

Ni mara chache sana hutokea Kwa Mwanamke bila kujua/kutofahamu ukweli Juu ya baba halisi wa mtoto na Hivyo kupelekea Naye kuongezwa kwenye kundi hili la waathiriwa wa Tatizo Hili.

Takwimu zinaonyesha Baba na mtoto ndio waathirika wakubwa wa janga hili la kubebeshwa damu zisizo za kwao Huku Mwanamke akiendelea kuinjoy ilihali akijua Hilo ni kosa mbele ya Sheria lakini pia mbele za Mungu.

Kwanini nasema DNA ni lazima?

Kuna Kesi nyingi sana za watoto kubadilishwa mahospitalini, Kwa sababu Moja au nyingine Kwa watu walio na nia ovu, kabla ya Wazazi kuondoka na mtoto wao Nyumbani ni lazima apimwe DNA kuhakikisha uhalali huo.

Lakini pia Kuhakikisha kwamba mtoto huyo ni Mali Halali ya Baba. kila Mtu abebe msalaba wake, Kama Mwanamke alipewa Mimba tofauti na Mwanaume aliyenaye basi Mwanaume huyo ahusike katika kulea mtoto wake, Gharama zote ziwe Juu yake isipokua Kwa MAKUBALIANO MAALUMU TU.

DNA IWE NI LAZIMA ILI KULINDA HESHIMA YA BABA NA FAMILIA KWA UJUMLA.
Naunga mkono hoja, na uzuri kwa sasa DNA inapimwa kwa laki 1 tu
 
Mkuu,

Kwa nini unajiona wewe ndiye mwenye maoni sahihi?

Unaelewa huko Ugiriki kushakuwa na jamii ya watu ambao watoto na wake walikuwa ni wa pamoja?

Yani kama mimi na wewe ni vijana wa kiume wa rika moja, basi wanawake wote wa rika moja ni wake zetu na watoto wote wa rika la kuwa watoto zetu ni watoto zetu, hakuna ubinafsi wa kusema huyu mke wangu na huyu mtoto wangu.

Na watu waliishi poa tu.

Unaelewa hilo? Aau haya ni kati ya yale mambo ambayo hujui kama Watanzania wengi kwa uvivu wa kusoma?
Mkuu huo ni mfano usio na mashiko, Ugiriki na Tanzania ni jamii mbili tofauti kabisa, tuna taratibu na Tamaduni mbili zisizoingiliana kabisa. Huko hata Mtoto kumkaripia mzazi na kumshtaki Kwa kosa la kumchapa ni Haki.

Sisi tuna Utaratibu wetu, na Hiki nilichoongea ni Moja ya Utaratibu wetu kama Watanzania.
 
Mkuu huo ni mfano usio na mashiko, Ugiriki na Tanzania ni jamii mbili tofauti kabisa, tuna taratibu na Tamaduni mbili zisizoingiliana kabisa. Huko hata Mtoto kumkaripia mzazi na kumshtaki Kwa kosa la kumchapa ni Haki.

Sisi tuna Utaratibu wetu, na Hiki nilichoongea ni Moja ya Utaratibu wetu kama Watanzania.
Sawa inawezekana tuna utaratibu wetu, lakini hakuna aliyekupa wewe cheo cha kulazimisha DNA test.

Ndiyo maana hiyo habari itabaki kuwa njozi na stories za kijiweni na JF tu.

Haitekelezeki.

Halafu wabongo ni watu wa njia za panya always, hata ukilazimisha DNA utapigwa humohumo kwenye DNA test feki!
 
Tusifike Huko Mkuu
emoji23.png
, Uhai ulindwe Kwa Gharama yoyote Ile lakini Damu zijulikane na mwenye uhalali apewe kilicho chake.
T
Tusifike Huko Mkuu, Uhai ulindwe Kwa Gharama yoyote Ile lakini Damu zijulikane na mwenye uhalali apewe kilicho chake.
Tumeacha mila na desturi za wazee wetu sasa tunalia lia!
Tulikuwa na jando
na mkole ilikuwa shule tosha
 
Back
Top Bottom