Kupigiana simu kwa wanandoa

Kupigiana simu kwa wanandoa

beautifulonyinye

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2015
Posts
728
Reaction score
481
Habarini za asubuhi wakuu, natumai ni wazima sana. Leo nina swali kwa wanandoa au wenye mahusiano ya mbali, mimi mume wangu siyo kwamba anafanya kazi nje ya mkoa ila amesafiri kikazi kwa muda tu ana kama karibia miezi 2.

Ila mwenzangu huyu hapigi simu ni ujumbe tu, sasa mimi hicho kitendo kinaniudhi sana na akipiga kidogo utasikia dk. zimeisha, sasa najiuliza dk. zimeisha anaongea na kina nani?

Sasa swali langu kwa wanandoa hasa wenye upendo na wake/waume/wapenzi wao, wanaweza kaa hata siku 3 bila kumpigia simu mwenza wake, yaani ni kawaida au kuna shida pahala?

Naomba maoni yenu hasa kwa wanaume waliokuwa makini na wake/wapenzi wao, namaanisha wenye upendo wa Agape.
 
Sijui kuhusu yeye kama kuna shida mahala ama lah!!

Binafsi mimi ni mvivu kinoooma kupiga simu, huu ni udhaifu wangu, kuongea muda mrefu kwenye simu naona tabu,
Mke wangu yupo km 500 kutoka nilipo mimi, anajua kuwa hilo ni tatizo langu, imebidi siku hizi awe ananikumbusha fulani umewasiliana nae, umemjulia hali, haya wasiliana nae sasa hivi unipe mrejesho.

Kwake imekuwa si tatizo katika mara 20 tutakazo ongea kwenye simu basi mara 19 kapiga yeye, akiwa likizo kwa siku anaweza piga simu hata mara 5.
Nikimpigia anafurahi kuwa naanza badilika kwa ajili yake, ila nisipopiga sio kesi anajua ndio udhaifu wangu.

Kwanza ngoja nimpigie mara ya mwisho kupiga mimi ni majuzi aliponitxt nimpigie salio limeisha 😂
 
Hili jambo mie lilileta ugomvi sana.

Kimsingi mie ni mvivu sana kupiga simu. Napiga simu tu pale ambapo naona ni muhimu kwangu. Kwa mfano nikisafiri napiga simu asubuhi kuuliza wameamkaje na mipango ya siku.

Baada ya hapo nitapiga simu usiku kuwa mmeshindaje na kiujumla mambo yalikuwaje?

Hili alikuwa hapendi but alikuja kuzoea. Mie mpaka wazazi wanajua hivyo.
 
Sijui kuhusu yeye kama kuna shida mahala ama lah!!

Binafsi mimi ni mvivu kinoooma kupiga simu, huu ni udhaifu wangu, kuongea muda mrefu kwenye simu naona tabu,
Mke wangu yupo km 500 kutoka nilipo mimi, anajua kuwa hilo ni tatizo langu, imebidi siku hizi awe ananikumbusha fulani umewasiliana nae, umemjulia hali, haya wasiliana nae sasa hivi unipe mrejesho.
Kwake imekuwa si tatizo katika mara 20 tutakazo ongea kwenye simu basi mara 19 kapiga yeye, akiwa likizo kwa siku anaweza piga simu hata mara 5.
Nikimpigia anafurahi kuwa naanza badilika kwa ajili yake, ila nisipopiga sio kesi anajua ndio udhaifu wangu


Kwanza ngoja nimpigie mara ya mwisho kupiga mimi ni majuzi aliponitxt nimpigie salio limeisha
Tunafanana sana.
 
Mimi kupiga simu pia ni mvivu sana,

Kwa sababu nipo nae mbali huwa nijitahidi baadhi ya siku nikiwa narudi kutoka job napiga simu tunaongea mpaka nafika home.

Ila nikiwa home kwangu huwa siongei kabisa hata nkipigiwa na mtu mwingine huwa napatwa na uvivu wa kupokea.
 
Anakujali? anakuthamini? anakutunza kama mkewe?

If yes then chukulia kama hiyo ndo weakness yake as hujaolewa na malaika mama, akitext mjibu ukimiss kuongea nae wewe mpigie maadam hajakukataza kumpigia mana hiyo ndo ingekua mbaya!

Vinginevyo unajitafutia vidonda vya tumbo mama!
 
Swali ni kwamba je wakati hajasafiri mkoa mwingine mlikuwa na hulka ya kupigiana sim ?
 
Back
Top Bottom