WanaJF,
Hivi punde nimetoka kwenye nyumba ya ibada kufanya sala, lakini kama ilivyo ada, tumefanya mawaidha hapa na kubwa zaidi lilikuwa ni suala la maadili kwa viongozi.
Katika mawaidha hayo, shekhe wetu alionyesha masikitiko makubwa sana kwa kitendo kilichofanywa na baadhi ya viongozi wa UKAWA kufuatia hatua za viongozi hao kuwapiga wake zao mabusu wakiwa katika hadhara.
Katika kukazia hoja zake, shekhe alimtaja Lowassa kuwa kinara wa michezo ya kubusu wanawake hadharani na pia alitolea mfano wa siku ya jana kuwa Lowassa alimbusu mkewe hadharani huku taifa zima likishuhudia!
Aidha, shekhe wetu alieleza kuwa, matendo ya kupigana mabusu hadharani hufanywa na watu walevi na wasio na maadili mema. Shekhe aliongeza kuwa, mtu yeyote mwenye akili timamu kamwe hawezi kufanya mambo hayo mbele ya hadhara kwani atatambua kuwa kuna watoto hivyo sio vyema kwao kuona mabusu.
Tukio hili kama linavyoonekana hapo juu sio la kimaadili na hakika halipaswi kufanywa mbele ya jamii ya Kitanzania.
Pia shekhe hakusita kugusia juu ya watu wanao jihusisha na ukahaba ambao nao wanajiweka karibu na viongozi wa umma...hapa binafsi nilipata picha kuwa atakuwa anawazungumzia aunt Ezekiel na Wolper.
Hivi punde nimetoka kwenye nyumba ya ibada kufanya sala, lakini kama ilivyo ada, tumefanya mawaidha hapa na kubwa zaidi lilikuwa ni suala la maadili kwa viongozi.
Katika mawaidha hayo, shekhe wetu alionyesha masikitiko makubwa sana kwa kitendo kilichofanywa na baadhi ya viongozi wa UKAWA kufuatia hatua za viongozi hao kuwapiga wake zao mabusu wakiwa katika hadhara.
Katika kukazia hoja zake, shekhe alimtaja Lowassa kuwa kinara wa michezo ya kubusu wanawake hadharani na pia alitolea mfano wa siku ya jana kuwa Lowassa alimbusu mkewe hadharani huku taifa zima likishuhudia!
Aidha, shekhe wetu alieleza kuwa, matendo ya kupigana mabusu hadharani hufanywa na watu walevi na wasio na maadili mema. Shekhe aliongeza kuwa, mtu yeyote mwenye akili timamu kamwe hawezi kufanya mambo hayo mbele ya hadhara kwani atatambua kuwa kuna watoto hivyo sio vyema kwao kuona mabusu.
Tukio hili kama linavyoonekana hapo juu sio la kimaadili na hakika halipaswi kufanywa mbele ya jamii ya Kitanzania.
Pia shekhe hakusita kugusia juu ya watu wanao jihusisha na ukahaba ambao nao wanajiweka karibu na viongozi wa umma...hapa binafsi nilipata picha kuwa atakuwa anawazungumzia aunt Ezekiel na Wolper.