Kupiga Chafya

fungamesa

Senior Member
Feb 20, 2009
129
13
Jamani naomba msaada. Maana huwa napiga chafya sana kila ninapohisi kunusa vumbi, mtu akivuta sigara moshi tu ukipita mbele yangu, pia kama natafuta nguo kabatini, nikipulizia pafyumu n.k. Chafya hiyo huambatana na mafua mepesi. Naomba mwenye kujua dawa yake nifanyaje maana hospitali huwa napewa piliton, chengachenga n.k bila mafanikio.
 
Jamani naomba msaada. Maana huwa napiga chafya sana kila ninapohisi kunusa vumbi, mtu akivuta sigara moshi tu ukipita mbele yangu, pia kama natafuta nguo kabatini, nikipulizia pafyumu n.k. Chafya hiyo huambatana na mafua mepesi. Naomba mwenye kujua dawa yake nifanyaje maana hospitali huwa napewa piliton, chengachenga n.k bila mafanikio.

Ni dhahiri wewe una allergy na kemikali (allergen) nyingi tu, hilo hutokea kwa watu wengi sana (mimi mmojawapo). Kemikali hizo husababisha mwasho kwenye njia ya hewa na mwili wako kureact kwa kutoa vichocheo (sana sana Histamine) kadhaa ambavyo ndivyo vinavyofanya upate mafua mepesi kama maji!

Dawa kubwa na ya hakika kwa allergy ni kuepuka hizo allergen zinazokusababishia hali hiyo, lakini hili si rahisi hivyo. Unaweza pia ukatumia dawa za jamii ya Anti-Histamine ambazo zinazuia kichocheo cha Histamine kisifanye kazi na kukusababishia muwasho na mafua, Piriton ni moja ya dawa hizo...except Piriton ina sedating effect hivyo inalaza laza (drowsiness), ni vyema kuitumia usiku kama huna kazi za kufanya. Dawa nzuri ni jamii ya Loratadine (Claritine, Clarityn, Claritin) lakini ni effective ukimeza pindi tu umekuwa exposed kwa hizo allergen, au kabla ya kuanza kazi za ndani ambazo unaexpect utakuna na hizo allergen...Pole!
 
Pole mkuu, Nichukuwe fursa hii kumshukuru dr.RIWA kwa kueleza kwa uzuri kabisa kuhusu aleji/mzio, ameelezea pia kuhusu histamine na akataja dawa zinazoweza kuidhibiti hiyo histamine (anti-histamine). Kwanza niseme tu anti-histamine ni dawa zenye madhara hasi mengi zaidi mwilini kuliko hata hiyo aleji yenyewe. Kusema ukweli ni vigumu sana kuitibu aleji/mzio kwa sayansi za hospitalini.

MAJI HUKINGA NA KUPONYA MZIO (Allergy):


Mzio/allergy, Ni kitendo cha mwili kupungukiwa maji wakati histamini inapozarishwa kupita wastani ili kuhimiza unywaji wa maji na ugawanywaji wa kiasi kidogo cha maji kipatikanacho mwilini.


Histamini ni kihisio cha kwanza (primary sensor) cha ubongo kinachozarishwa ili kujishughurisha na ugawanywaji wa maji kwa viungo mhimu wakati kunapokuwa na upungufu wa maji mwilini.


Inajihusisha na kazi ya ugawanywaji wa kiasi kidogo kinachopatikana cha maji (maji ya mgawo) wakati wa upungufu wa maji mwilini (Unintentional chronic dehydration).


Histamini katika lugha rahisi:


Histamini ni kemikali ambayo miili yetu huitoa inapohitaji msaada kusawazisha upungufu wa vitu mhimu sana mwilini kama maji, chumvi au potasiamu. Histamini na wasaidizi wake wengine watano (5 buddies) watasaidia kuusawazisha upya mwili ambao upo nje ya usawa.


Kwa hakika Histamini ni kitu kizuri ambacho huokoa maisha yetu kwa mujibu wa dr. Batmanghelidj. Bonyeza hapa kusoma yote: http://maajabuyamaji.net/maajabu/mzioaleji/
 
Jamani naomba msaada. Maana huwa napiga chafya sana kila ninapohisi kunusa vumbi, mtu akivuta sigara moshi tu ukipita mbele yangu, pia kama natafuta nguo kabatini, nikipulizia pafyumu n.k. Chafya hiyo huambatana na mafua mepesi. Naomba mwenye kujua dawa yake nifanyaje maana hospitali huwa napewa piliton, chengachenga n.k bila mafanikio.
yani we acha mimi ni hivyo hivyo nimemaliza hospitali zote lakini wapi kuna hospitali hapo magomeni nilienda wanashughulika na mambo ya allergy and wanaku hakikishia unapona kbs lkn wapi wanataka ukienda pale ni kazi kununua midawa kwa midawa na masharti ya vyakula, mi ilinianza i think nilivo kuwa 13 kitu kama icho,bibi yangu kaniambia hili tatizo linaitwa KAMBAKU,kuna dawa yake au nenda kwa wamasai ulizia mavumba ya kambaku unakoroga na chai kidogo afu unakuywa kama pua zimebana unanusa unapiga chafya zizibuke, lakini nisikukatishe tamaa once ukiacha or ukisahau kunywa mafua yako palepale, the only way i cope with it nimejifunza kuishi nayo nimeacha kupulizia perfum na body spary,sabuni natumia ya punda ile ya blue na white, nikiwa nafanya usafi au natafuta nguo kabatini i hold my breath au najifunga kitambaa afu sasa mimi nakaa karibu na barabra so vumbi ndani ni lazima kabla ya kulala kun'guta kitanda mafua yakicharuka kula machugwa as much as you can mi ata 7 nakula na kabla ya kulala meza panadol, dah yani tabu tunayo pata watu hawajui tu wanaona kaa mafua ya kawaida wakati same times maskio yanaziba, ukiinama kichwa kinauma, maeneo ya nyusi kunauma, milago ya pua inauma mwili wote unaskia homa, yani siku nzima unakuwa huna raha, ila bibi yangu kaniambia ukitaka yapone ni kwenda kwa mganga sijui akupikie chungu afu unajifukiza naskia unapewa mashrti ya vitu ambovo usile for like a week then unapona kabisaa,sasa sijui kama ni kweli
 
Back
Top Bottom