Kupendwa raha jamani

Kupendwa raha jamani

Mjuukum

Senior Member
Joined
Nov 4, 2014
Posts
164
Reaction score
27
Unaamshwa asubuhi, Unatayarishiwa maji ya kuoga, Unaandaliwa nguo za kuvaa kwa siku hiyo, Unaandaliwa chai au brekefast kwa kizungu aaah
Unapewa maneno ya kutiwa moyo na mwandani wako, Njiani unasindikizwa kwa simu ya mwandani au sms , Ukifika job au kibaruani unaanmbiwa "kazi njema".

Unakumbushwa kula chakula cha mchana na mwandani kwa simu au sms, Jioni unapewa dondoo za stori na mwandani kabla ya kutoka ili upate hamu ya kurudi nyumbani mapema Ukifika mwandani anakupokea na kukupa pole kwa namna anavyojua yeye, Unakaa kwenye kochi anakuwashia Tv anakuwekea kipindi ukipendacho. Unaletewa chai ya kutayarisha tumbo kbla ya mlo wa usiku.

Hapo sasa ratiba inajishona yenyewe baada ya kula chakula cha jioni (dinner).

Mwasemaje wadau?
 
Unaamshwa asubuhi
Unatayarishiwa maji ya kuoga
Unaandaliwa nguo za kuvaa kwa siku hiyo
Unaandaliwa chai au brekefast kwa kizungu aaah
Unapewa maneno ya kutiwa moyo na mwandani wako
Njiani unasindikizwa kwa simu ya mwandani au sms
Ukifika job au kibaruani unaanmbiwa "kazi njema"
Unakumbushwa kula chakula cha mchana na mwandani kwa simu au sms
Jioni unapewa dondoo za stori na mwandani kabla ya kutoka ili upate hamu ya kurudi nyumbani mapema
Ukifika mwandani anakupokea na kukupa pole kwa namna anavyojua yeye
Unakaa kwenye kochi anakuwashia Tv anakuwekea kipindi ukipendacho
Unaletewa chai ya kutayarisha tumbo kbla ya mlo wa usiku



Hapo sasa ratiba inajishona yenyewe baada ya kula chakula cha jioni (dinner)

Mwasemaje wadau?
  • Yawezekana kwa miezi sita ya mwanzo wa ndoa changa
  • Sababu kuna wanandoa kwenye ndoa, wanaishi kwa mazoea tu, ilimradi siku ziende
  • Kama ingekuwa hivyo (ulivyoandika) tusingesikia ndoa kuvunjika, kufumaniana na mitafaruku ya kila aina.


 
Last edited by a moderator:
Watu wana roho za uchungu,ghubu na wivu jamani humu dunian...mtoa mada anapata raha ya ndoa/mahusiano yake,wewe unaleta stress zako hapa za ndoa chungu sijui wengine wanalia ndani ya ndoa..yaan umekaa kimaumivumaumivu tu unataka na wengine waishi kama wewe katika mahusiano yako,wewe ni wewe na wengine ni wengine..watu toka waoane mambo ni mazuri kabisa,kuna kutofautiana mtazamo ila hawajagombana hata siku moja kama wewe hadi unalala na kisu chini ya kitanda badala ya asali ya mahaba na mafuta yakuchua mwili pemben,..wewe au huyo mwenzako kwa pamoja au tofauti mliharibu mahusiano yenu,sasa unaleta hoja za maumivu yako ili wengine waogope au??wakati mwingine tuwe tunajadili na raha za mahusiano siyo maumivu tu...namna hii uadui unazidi kuongezeka katika jamii...kama unapataga maumivu tu waone wazoefu wakupe mbinu unenepe roho kwa mapenzi..ndiyo kusema MAUMIVU YA MAPENZI YANATIBIWA NA MAPENZI SIYO VINGINEVYO....kupendwa raha mtoa mada...
 
Mmh huo ni mwanzo tu na ukiona unanyenyekewa sana ujue huyo kaachika mahali so anaishi kwa wasiwasi na kuna kitu anatafuta ndio maana unafanya yote hayo huna lolote so live your life don't pretend
 
Back
Top Bottom