Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 40,556
- 63,025
Mawasiliano ni kitu cha muhimu sana.Lakini si vizuri kwa masaa 24 kila mtu anayekutafuta awe anakupata kwenye mawasiliano.Ile hali ya mtu yeyote kukupata masaa 24 tunaita ni u-'cheap labour'.Yaani wewe unajiweka cheap katika maisha yako.Anayetakiwa kukupata wewe masaa 24 ni mke/mume,watoto,wazazi wako.Kuhusu marafiki,mabosi zako kazini n.k wanatakiwa wawe na limit kwenye muda...mfano mwisho wa mawasiliano yao uwe ni baada ya kutoka kazini n.k.Baada ya hapo simu /laini inakuwa off...hii itakupa heshima na kila mtu atakuona wa thamani.Si sifa bosi wako kukupigia muda anaotaka..mfano saa nne usiku au usiku wa manane...ukiona hivyo ujue wamekuona wewe ni 'cheap'. Unaweza kuwa na mtandao/laini kwa ajili ya kazi,marafiki,familia..Ni mtazamo wangu.....