Haya mambo yalianza zamani. Miaka ya 1990 nilipata scholarship ya serikali (Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia ikiongozwa na Ben Mkapa wakati huo). Ukitoa viongozi wa juu wa Wizara, wengine wengi wao walikuwa Wazanzibari. Kuna jamaa akiitwa Fitawi na mwingine Shaban. Wala rushwa wakubwa sana. Basi majina ya scholarship yalipotoka, jina langu lilikuwemo. Nikafurahi lakini pia nikawa nashangaa kuwepo bila kutoa rushwa. Ilikuwa ya kwenda kusoma udaktari Urusi. Wakati wa kuondoka, jina langu lilikwisha tolewa. Nilijaribu kwenda kumwona Mkurugenzi wa Elimu ya Juu lakini haikusaidia. Kila niliyemwona, alikuwa anawatetea akina Shabani na Fitawi. Nikagundua kuwa hii ni kesi ya tumbili... Nikaishia kusoma Tanzania. Lakini baadaye nilimshukuru Mungu sana kwa kusoma Tanzania. Tanzania ni miaka 5 tu nikawa nimemaliza. Waliokwenda Urusi walichukuwa miaka 7-8 kumaliza. Waliporudi, walinikuta mimi tayari ni chief wao. Kwa hiyo nami naweza kupigiwa simu siku moja ili nihesabiwe kama niliyesoma Urusi. Mpaka leo ninayo barua ya Wizara ya kwenda kusoma Urusi.