Kupata Kadi na plate number Pikipiki

Kupata Kadi na plate number Pikipiki

Lameckk

Member
Joined
Jun 5, 2024
Posts
9
Reaction score
1
WanaJamiiForums Habari zenu,

Nimenunua Pikipiki Mpya kwenye kampuni Fulani Tangia mwezi wa Tatu Hadi kufikia muda huu sijapata plate number na Kadi nikiwapigia wananiambia Chassis yangu Haionekani kwenye Mfumo wa TRA,

Naombeni Msaada wa Kisheria nn nifanye? maana pia Barabarani Traffic wananisumbua lakini pia inanijima umiliki halali wa Chombo changu.
 
Yaezakuwa pkpk yako iliingia kimagendo pasi kulipiwa Kodi,

Washtaki uone kama hawajakupa pkpk ingine
 
Yaezakuwa pkpk yako iliingia kimagendo pasi kulipiwa Kodi,

Washtaki uone kama hawajakupa pkpk ingine
Ana washitaki kwa reference ipi? Kama kadi hana bila shaka hakuna hata mkataba wa mauziano.
Hapo akijifanya mjuaji hawakawii kumgeuzia kibao kuwa jamaa kawaibia pikipiki yao. Kwa kifupi jamaa kafanya biashara kisukuma sana
 
Daah yani ulinunuaje nunuaje hio pikipiki em weka wazi weka na hio kampuni wazi kabsa ukiwa unahitaji msaada lazma uwe wazi
 
Ana washitaki kwa reference ipi? Kama kadi hana bila shaka hakuna hata mkataba wa mauziano.
Hapo akijifanya mjuaji hawakawii kumgeuzia kibao kuwa jamaa kawaibia pikipiki yao. Kwa kifupi jamaa kafanya biashara kisukuma sana
Atawashtaki sababu alipewa risiti ya EFD aliponunua.

Kama hana risiti, asitupigie kelele.
 
Kwa hawa wafanya biashara unanunua mzigo wa vifaa vya umeme risiti inasoma vitenge au vipodozi?
Pikipiki mpya ya 3m unanunuaje bila risiti na kukubali kuondoka bila kadi wala plate number?

Risiti itamsaidia kupata kadi itaposajiliwa, na ikishindikana kupata usajili, risiti itawafanya wampe pkpk ingine ambayo chasis yake itakuballi kupokea usajili kwenye mifumo.

Kununua pikipiki SI sawa na kununua kitenge..


Tusiragisishe mambo
 
Ulifanya biashara kienyeji mkuu.
Pkpk mpya nyingi tu zinauzwa bila kadi wala plate number,

Unapewa risiti ya manunuzi, inaandikwa chasis number kwenye Kibao, inawekwa nyuma ya pkpk unatembelea kwa muda ambao usajili bado kukamilika.

Unaacha tin namba na majina yako Ili washughulikie new registration kwenye mifumo tra.


Kama ambavyo gari hutembelea chasis number, pikipiki ni hivyo pia.
 
Pikipiki mpya ya 3m unanunuaje bila risiti na kukubali kuondoka bila kadi wala plate number?

Risiti itamsaidia kupata kadi itaposajiliwa, na ikishindikana kupata usajili, risiti itawafanya wampe pkpk ingine ambayo chasis yake itakuballi kupokea usajili kwenye mifumo.

Kununua pikipiki SI sawa na kununua kitenge..


Tusiragisishe mambo
Mkuu kama imeshindikana kupewa kadi ambapo ni zoezi la siku moja tu kuhamisha umiliki kutoka kampuni muuzaji kwenda kwa mteja mnunuzi.
Sitarajii kama huyo muuzaji atakuwa muadilifu kutoa risiti ya EFD yenye thamani ya Million 3+ tena inayosoma bidhaa halisi iliyouzwa na sio risiti ya kutembelea asisumbuliwe na askari.
 
Mkuu kama imeshindikana kupewa kadi ambapo ni zoezi la siku moja tu kuhamisha umiliki kutoka kampuni muuzaji kwenda kwa mteja mnunuzi.
Sitarajii kama huyo muuzaji atakuwa muadilifu kutoa risiti ya EFD yenye thamani ya Million 3+ tena inayosoma bidhaa halisi iliyouzwa na sio risiti ya kutembelea asisumbuliwe na askari.
Hapo ni hivi,

Yaweza kuwa ni kweli mfumo ulisumbua kusajili au kufuta taarifa za chasis husika,

Hapo busara wauzaji ni kummsaidia apate pkpk ingine ambayo itapata usajili ndani ya wiki, wao washughulikie tatizo.
 
WanaJamiiForums Habari zenu,

Nimenunua Pikipiki Mpya kwenye kampuni Fulani Tangia mwezi wa Tatu Hadi kufikia muda huu sijapata plate number na Kadi nikiwapigia wananiambia Chassis yangu Haionekani kwenye Mfumo wa TRA,

Naombeni Msaada wa Kisheria nn nifanye? maana pia Barabarani Traffic wananisumbua lakini pia inanijima umiliki halali wa Chombo changu.
Hadithi za new member zinanifurahisha sana ......... Kwahyo Wew unamiliki chombo au unamiliki pikipiki?????
 
Ana washitaki kwa reference ipi? Kama kadi hana bila shaka hakuna hata mkataba wa mauziano.
Hapo akijifanya mjuaji hawakawii kumgeuzia kibao kuwa jamaa kawaibia pikipiki yao. Kwa kifupi jamaa kafanya biashara kisukuma san
and
Ana washitaki kwa reference ipi? Kama kadi hana bila shaka hakuna hata mkataba wa mauziano.
Hapo akijifanya mjuaji hawakawii kumgeuzia kibao kuwa jamaa kawaibia pikipiki yao
Ana washitaki kwa reference ipi? Kama kadi hana bila shaka hakuna hata mkataba wa mauziano.
Hapo akijifanya mjuaji hawakawii kumgeuzia kibao kuwa jamaa kawaibia pikipiki yao. Kwa kifupi jamaa kafanya biashara kis
Mkuu kama imeshindikana kupewa kadi ambapo ni zoezi la siku moja tu kuhamisha umiliki kutoka kampuni muuzaji kwenda kwa mteja mnunuzi.
Sitarajii kama huyo muuzaji atakuwa muadilifu kutoa risiti ya EFD yenye thamani ya Million 3+ tena inayosoma bidhaa halisi iliyouzwa na sio risiti ya kutembelea asisumbuliwe na askari.
Nilipewa Risiti Tuu wadau
 
Hadithi za new member zinanifurahisha sana ......... Kwahyo Wew unamiliki chombo au unamiliki pikipiki?????
Waliniuzia wakanipa Risiti ya EFD Tuu wakaniambia Plate Namba na Kadi nitapata Baada ya wiki moja
 
Mkuu kama imeshindikana kupewa kadi ambapo ni zoezi la siku moja tu kuhamisha umiliki kutoka kampuni muuzaji kwenda kwa mteja mnunuzi.
Sitarajii kama huyo muuzaji atakuwa muadilifu kutoa risiti ya EFD yenye thamani ya Million 3+ tena inayosoma bidhaa halisi iliyouzwa na sio risiti ya kutembelea asisumbuliwe na askari.
Risiti Ninayo Mkuu plate Namba na Kadi Ndo waliniambia watanipa Baada ya wiki moja
 
Pkpk mpya nyingi tu zinauzwa bila kadi wala plate number,

Unapewa risiti ya manunuzi, inaandikwa chasis number kwenye Kibao, inawekwa nyuma ya pkpk unatembelea kwa muda ambao usajili bado kukamilika.

Unaacha tin namba na majina yako Ili washughulikie new registration kwenye mifumo tra.


Kama ambavyo gari hutembelea chasis number, pikipiki ni hivyo pia.
Na Mimi pia Nilifanya hivyo hivyo Niko na Risiti ya EFD Tuu
 
Back
Top Bottom