Kuondoa Ubabaishaji wa TANESCO Kuundwe Makampuni Madogo ya Kimkoa na Kikanda

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,566
41,085
Kila mmoja anajua kuwa Serikali, mashirika na makampuni yake, hawajawahi kuwa na ufanisi katika mambo karibia yote . Wanachoweza ni ulaghai, uwongo, kukamata watu, na mara nyingi kubambikia watu kesi. Lakini ukija kwenye utawala bora ni zero, uadilifu ni zero, ubunifu ni zero, biashara na uchumi.

Kwa sasa Serikali inachofanya ni kuwafukarisha watu kupitia TANESCO. TANESCO inafanya kazi zake kwa ulaghai mkubwa. Mara walisema mitambo inafanyiwa marekebisho, mara mvua hakuna, mara tunabadilisha nguzo, sahizi wanasema ni hitilafu!! Yaani umeme kutokuwepo kwa siku nzima ni hitilafu. Nchi nyingine, hii isingetajwa kama hitilafu bali janga. Na ni lazima Serikali nzima ingekuwa busy na suala hilo. Na vyombo vya habari vingekuwa live kufuatilia yote yanayoendelea.

Ukweli ni kwamba hawa watu ni waongo. Na kwa kutegemea hawa TANESCO, hata tungekuwa na mabwawa 1,0000 ya kuzalishia umeme, bado hatutaweza kupata umeme wa uhakika. Na kwenye hili, subirini litakapoanza kutumika bwawa la Nyerere kama kutakuwa na umeme wa uhakika. Hawa watu wameishiwa uelewa, maarifa, uafilifu, na hawana namna nyingine yoyote. Upeo na uwezo wao umegota.

Serikali ilishindwa kuendesha mabenki, viwanda mbalimbali, ATCL, simu, elimu, afya (mpaka sasa kwa kiasi kikubwa wabategemea hospitali za makanisa) n.k. Hivi tunategemea muujiza gani toka TANESCO iliyo chini ya Serikali, kwenye umeme?

Ni vema sasa, tukafanya kama ilivyofanyika kwenye simu. TANESCO inyang'anywe monopoly kwenye biashara ya umeme. Iwe ni kampuni tu ya kawaida itakayohitajika kutimiza sheria na sera ya nishati. Makampuni binafsi yaruhusiwe kuzalisha na kusambaza umeme kwenye maeneo yoyote watakayotaka na watakayoweza. Yanaweza kuanza na mikoa michache. Kwa kuanzia makampuni hayo yanaweza kutumia umeme na miundombinu ya TANESCO, huku, taratibu wakitengeneza miundombinu yao, na kujenga vyanzo vipya vya kuzalishia umeme. Huko mbeleni makampuni yatakuwa na uamuzi wa kununua umeme wa TANESCO au kununua kwa wazalishaji wengine. TANESCO watalipwa mapato ya ukodishaji miundombinu yao. Na yenyewe ikiwa mibovu, baadaye inaweza kuachwa.

Kunaweza kufanyika hata utaratibu mwingine, lakini kwa kuitegemea hii TANESCO, tusitegemee kwenda kokote. Kuna baadhi ya mataifa, umeme kukatika hata kwa saa moja, kunaweza kuiangusha Serikali lakini sisi kutokuwa na umeme inaonekana ni maisha ya kawaida.
 
Kila mmoja anajua kuwa Serikali, mashirika na makampuni yake, hawajawahi kuwa na ufanisi katika mambo karibia yote . Wanachoweza ni ulaghai, uwongo, kukamata watu, na mara nyingi kubambikia watu kesi. Lakini ukija kwenye utawala bora ni zero, uadilifu ni zero, ubunifu ni zero, biashara na uchumi.

Kwa sasa Serikali inachofanya ni kuwafukarisha watu kupitia TANESCO. TANESCO inafanya kazi zake kwa ulaghai mkubwa. Mara walisema mitambo inafanyiwa marekebisho, mara mvua hakuna, mara tunabadilisha nguzo, sahizi wanasema ni hitilafu!! Yaani umeme kutokuwepo kwa siku nzima ni hitilafu. Nchi nyingine, hii isingetajwa kama hitilafu bali janga. Na ni lazima Serikali nzima ingekuwa busy na suala hilo. Na vyombo vya habari vingekuwa live kufuatilia yote yanayoendelea.

Ukweli ni kwamba hawa watu ni waongo. Na kwa kutegemea hawa TANESCO, hata tungekuwa na mabwawa 1,0000 ya kuzalishia umeme, bado hatutaweza kupata umeme wa uhakika. Na kwenye hili, subirini litakapoanza kutumika bwawa la Nyerere kama kutakuwa na umeme wa uhakika. Hawa watu wameishiwa uelewa, maarifa, uafilifu, na hawana namna nyingine yoyote. Upeo na uwezo wao umegota.

Serikali ilishindwa kuendesha mabenki, viwanda mbalimbali, ATCL, simu, elimu, afya (mpaka sasa kwa kiasi kikubwa wabategemea hospitali za makanisa) n.k. Hivi tunategemea muujiza gani toka TANESCO iliyo chini ya Serikali, kwenye umeme?

Ni vema sasa, tukafanya kama ilivyofanyika kwenye simu. TANESCO inyang'anywe monopoly kwenye biashara ya umeme. Iwe ni kampuni tu ya kawaida itakayohitajika kutimiza sheria na sera ya nishati. Makampuni binafsi yaruhusiwe kuzalisha na kusambaza umeme kwenye maeneo yoyote watakayotaka na watakayoweza. Yanaweza kuanza na mikoa michache. Kwa kuanzia makampuni hayo yanaweza kutumia umeme na miundombinu ya TANESCO, huku, taratibu wakitengeneza miundombinu yao, na kujenga vyanzo vipya vya kuzalishia umeme. Huko mbeleni makampuni yatakuwa na uamuzi wa kununua umeme wa TANESCO au kununua kwa wazalishaji wengine. TANESCO watalipwa mapato ya ukodishaji miundombinu yao. Na yenyewe ikiwa mibovu, baadaye inaweza kuachwa.

Kunaweza kufanyika hata utaratibu mwingine, lakini kwa kuitegemea hii TANESCO, tusitegemee kwenda kokote. Kuna baadhi ya mataifa, umeme kukatika hata kwa saa moja, kunaweza kuiangusha Serikali lakini sisi kutokuwa na umeme inaonekana ni maisha ya kawaida.
wazo lako ni zuri sana
 
Kila mmoja anajua kuwa Serikali, mashirika na makampuni yake, hawajawahi kuwa na ufanisi katika mambo karibia yote . Wanachoweza ni ulaghai, uwongo, kukamata watu, na mara nyingi kubambikia watu kesi. Lakini ukija kwenye utawala bora ni zero, uadilifu ni zero, ubunifu ni zero, biashara na uchumi.

Kwa sasa Serikali inachofanya ni kuwafukarisha watu kupitia TANESCO. TANESCO inafanya kazi zake kwa ulaghai mkubwa. Mara walisema mitambo inafanyiwa marekebisho, mara mvua hakuna, mara tunabadilisha nguzo, sahizi wanasema ni hitilafu!! Yaani umeme kutokuwepo kwa siku nzima ni hitilafu. Nchi nyingine, hii isingetajwa kama hitilafu bali janga. Na ni lazima Serikali nzima ingekuwa busy na suala hilo. Na vyombo vya habari vingekuwa live kufuatilia yote yanayoendelea.

Ukweli ni kwamba hawa watu ni waongo. Na kwa kutegemea hawa TANESCO, hata tungekuwa na mabwawa 1,0000 ya kuzalishia umeme, bado hatutaweza kupata umeme wa uhakika. Na kwenye hili, subirini litakapoanza kutumika bwawa la Nyerere kama kutakuwa na umeme wa uhakika. Hawa watu wameishiwa uelewa, maarifa, uafilifu, na hawana namna nyingine yoyote. Upeo na uwezo wao umegota.

Serikali ilishindwa kuendesha mabenki, viwanda mbalimbali, ATCL, simu, elimu, afya (mpaka sasa kwa kiasi kikubwa wabategemea hospitali za makanisa) n.k. Hivi tunategemea muujiza gani toka TANESCO iliyo chini ya Serikali, kwenye umeme?

Ni vema sasa, tukafanya kama ilivyofanyika kwenye simu. TANESCO inyang'anywe monopoly kwenye biashara ya umeme. Iwe ni kampuni tu ya kawaida itakayohitajika kutimiza sheria na sera ya nishati. Makampuni binafsi yaruhusiwe kuzalisha na kusambaza umeme kwenye maeneo yoyote watakayotaka na watakayoweza. Yanaweza kuanza na mikoa michache. Kwa kuanzia makampuni hayo yanaweza kutumia umeme na miundombinu ya TANESCO, huku, taratibu wakitengeneza miundombinu yao, na kujenga vyanzo vipya vya kuzalishia umeme. Huko mbeleni makampuni yatakuwa na uamuzi wa kununua umeme wa TANESCO au kununua kwa wazalishaji wengine. TANESCO watalipwa mapato ya ukodishaji miundombinu yao. Na yenyewe ikiwa mibovu, baadaye inaweza kuachwa.

Kunaweza kufanyika hata utaratibu mwingine, lakini kwa kuitegemea hii TANESCO, tusitegemee kwenda kokote. Kuna baadhi ya mataifa, umeme kukatika hata kwa saa moja, kunaweza kuiangusha Serikali lakini sisi kutokuwa na umeme inaonekana ni maisha ya kawaida.
Tumefanya hvyo kwny cm,kila cku bando juu
Zenj wamempa kdg mfaransa bandar,vilio vya gharama bandarin vmeanza
Umeme c ndo tutalia kilio cha mbwa hapa
 
Tumefanya hvyo kwny cm,kila cku bando juu
Zenj wamempa kdg mfaransa bandar,vilio vya gharama bandarin vmeanza
Umeme c ndo tutalia kilio cha mbwa hapa
Angalao umeme utaupata. Fikiria kama hata hilo bando la bei juu lisingekuwepo kabisa.
 
Kila mmoja anajua kuwa Serikali, mashirika na makampuni yake, hawajawahi kuwa na ufanisi katika mambo karibia yote . Wanachoweza ni ulaghai, uwongo, kukamata watu, na mara nyingi kubambikia watu kesi. Lakini ukija kwenye utawala bora ni zero, uadilifu ni zero, ubunifu ni zero, biashara na uchumi.

Kwa sasa Serikali inachofanya ni kuwafukarisha watu kupitia TANESCO. TANESCO inafanya kazi zake kwa ulaghai mkubwa. Mara walisema mitambo inafanyiwa marekebisho, mara mvua hakuna, mara tunabadilisha nguzo, sahizi wanasema ni hitilafu!! Yaani umeme kutokuwepo kwa siku nzima ni hitilafu. Nchi nyingine, hii isingetajwa kama hitilafu bali janga. Na ni lazima Serikali nzima ingekuwa busy na suala hilo. Na vyombo vya habari vingekuwa live kufuatilia yote yanayoendelea.

Ukweli ni kwamba hawa watu ni waongo. Na kwa kutegemea hawa TANESCO, hata tungekuwa na mabwawa 1,0000 ya kuzalishia umeme, bado hatutaweza kupata umeme wa uhakika. Na kwenye hili, subirini litakapoanza kutumika bwawa la Nyerere kama kutakuwa na umeme wa uhakika. Hawa watu wameishiwa uelewa, maarifa, uafilifu, na hawana namna nyingine yoyote. Upeo na uwezo wao umegota.

Serikali ilishindwa kuendesha mabenki, viwanda mbalimbali, ATCL, simu, elimu, afya (mpaka sasa kwa kiasi kikubwa wabategemea hospitali za makanisa) n.k. Hivi tunategemea muujiza gani toka TANESCO iliyo chini ya Serikali, kwenye umeme?

Ni vema sasa, tukafanya kama ilivyofanyika kwenye simu. TANESCO inyang'anywe monopoly kwenye biashara ya umeme. Iwe ni kampuni tu ya kawaida itakayohitajika kutimiza sheria na sera ya nishati. Makampuni binafsi yaruhusiwe kuzalisha na kusambaza umeme kwenye maeneo yoyote watakayotaka na watakayoweza. Yanaweza kuanza na mikoa michache. Kwa kuanzia makampuni hayo yanaweza kutumia umeme na miundombinu ya TANESCO, huku, taratibu wakitengeneza miundombinu yao, na kujenga vyanzo vipya vya kuzalishia umeme. Huko mbeleni makampuni yatakuwa na uamuzi wa kununua umeme wa TANESCO au kununua kwa wazalishaji wengine. TANESCO watalipwa mapato ya ukodishaji miundombinu yao. Na yenyewe ikiwa mibovu, baadaye inaweza kuachwa.

Kunaweza kufanyika hata utaratibu mwingine, lakini kwa kuitegemea hii TANESCO, tusitegemee kwenda kokote. Kuna baadhi ya mataifa, umeme kukatika hata kwa saa moja, kunaweza kuiangusha Serikali lakini sisi kutokuwa na umeme inaonekana ni maisha ya kawaida.
Shida sio serikali wala TANESCO shida ni sisi wananchi hatuwajibiki kudai haki zetu hivyo shida ya kukosekana kwa umeme haiwasumbui wala kuwapa shida watendaji wa TANESCO hata viongozi serikalini

Fikiria maanadamano ya kudai umeme yangeanza tu tangu wiki ya kwanza ya katika katika hii sasa hivi wangekuwa hawajalitatua??
 
Shida sio serikali wala TANESCO shida ni sisi wananchi hatuwajibiki kudai haki zetu hivyo shida ya kukosekana kwa umeme haiwasumbui wala kuwapa shida watendaji wa TANESCO hata viongozi serikalini

Fikiria maanadamano ya kudai umeme yangeanza tu tangu wiki ya kwanza ya katika katika hii sasa hivi wangekuwa hawajalitatua??
Upo sahihi. Uingereza, mwaka 1974 kulitokea mgao wa umeme kutokana na mgomo wa wafanyakazi wa mgodi wa makaa ya mawe. Wananchi hawakusikiliza hadithi za Serikali, waliiondoa Serikali ya Conservative iliyokuwa chini ya Waziri Mkuu Edward Heath. Hiyo iliwezekana kwa sababu nchi ilikuwa na watu wenye utimamu wa akili, wanaotambua mamlaka yao. Haikuwa na watu wa ajabu ajabu, wasiojielewa kama akina Mwashambwa, Variable, au wengine wa namna yao.
 
Tanesco wanakata Umeme kweli Siku ya sikukuu Hii ni KERO
Wazo la mtoa mada ni la msingi, lakini halitekelezeki kwa sababu wakubwa wananufaika na shirika la umeme. Kuna namna ambavyo wanaweza kutwist mambo wakala cha juu. Ndio maana kuanzisha shirika binafsi la umeme inakuwa ngumu sana. Akitokea mwekezaji atapewa masharti magumu mno mpaka atheme. Lazima atashindwa masharti. Kuna wakati nilidhani serikali imezuia mashirika binafsi lakini baada ya utafiti nikabaini sheria ya kuruhusu hilo ilishatungwa. Changamoto ikawa kwenye kanuni zinazosimamia utekelezaji wa hilo zimefanywa kuwa ngumu sana kupita maelezo.
Bila kupata wawekezaji binafsi kwenye umeme tutaendelea kulia na kulalamika bila mafanikio. Tanzania nchi yangu naipenda
Ila katika hili tunahitaji mabadiliko makubwa sana ili kuhakikisha tunapata maendeleo endelevu
 
Back
Top Bottom