Kuoa! Ili iweje?


VYOTE UTABISHA: Lakini subiri uanze kuoza ukiwa bado hai,ndio hivyo viswali vyako utajijibu mwenyew,ukija tena kuomba ushaur hapa jf nasisi tutakuuliza unakula pipi[ARV] ili iweje?
 
Inatakiwa atoe strong reson sio kumpiga vijembe tu na kumkandia,huenda ana maana sana nyuma ya pazia kutokana na sentesi yake ya kuoa ili iweje
 
Kibaolojia umekua, ila kitabia, kifikira, kimatendo, kimtazamo na kijamii bado mtoto. Na haya yanajipambanua kutokana na andiko lako linalokuonyesha kuwa unafikiri ndoa ni ngono, mke kukuzalia watoto, mke kukufuliwa nguo, soksi, mke kukufagilia nyumba na upuuzi mwingine unaofanana na huo. Yaani unachukulia ndoa ni mkusanyiko shughuli ambazo unafanyiwa na mwanamke. Are you serious? Ndoa ni zaidi za tamaa ya ngono, ndoa ni mapenzi na mapenzi ni zaidi ya ngono. ndoa ni kusaidiana majukumu na sio kusaidiwa kama unavyowaza wewe. ndoa ni taasisi takatifu, tofauti na unavyofikri wewe. ndoa malezi ya watoto kama mkijaliwa kupata watoto na ujenzi wa familia iliyo imara. Ndoa ni hali ya kujisikia mume na mke wapo mwili mmoja. Na mengine mengi yanayofanana na haya. Nakushauri ujiongeze.
 
We nani kakwambia wazazi wake walioana?
 
Kama huelewi umuhimu wa kuoa bora usioe tu
 
Hiyo ni laana unamuhitaji YESU akuweke huru maana umefungwa na pepo la ngono hata hujitambui
 
Mkuu, hoja zako ni nzuri, ila unapoingiza suala la Mungu unakuwa hauko sawa, sio watu wote wanaamini katika hizi dini zinazozungumzia Mungu achilia mbali hilo ulilosema ni kusudi lake, hebu toa hoja ambazo zitamgusa kila mtu, bila kujali ni muumini wa dini ama la.

Hadi hapa hakuna aliyetoa hoja yenye mashiko, wengi wanazungumzia kupikiwa, kufuliwa na kadhalika, vitu ambavyo mfanyakazi wa kawaida tu anaweza kufanya, wengine wanasema ili kupata mtoto na kuuguzwa ukiugua, vitu vinavyowezekana tu bila ndoa, swali linabaki, kwa nini mtu aoe?

Binafsi nakaribia 40 na sijawahi kufikiria kuoa, msiniponde, nipeni hoja kwa nini nioe, labda mnaweza kunishawishi nianze kutafuta mchumba.
 
Huyu bado mtoto mdogo mhurumieni tu akikua atajua ujinga aliokuwa akifikiria.
 

Sawa mkuu
 
Umekula maharage ya wapi wewe mpaka usione umuhimu wa kuishi na mke na watoto? HAKIKA HUWEZI KUJUA UTAMU WA ASALI MPAKA UONJE.
 

Ili ujipangie malengo, unadhani kila siku utakuwa kijana? Kuna siku wasichana watakukimbia na utabaki peke yako na hapo ndiyo utaiona hiyo 'nipo nipo' kama inafanya kazi.
 
halafu nawewe unajiita mwanaume....
 
kuna watu wa kuwashauri lakini sio mleta mada.........AMEVURUGWA
 

una akili kubwa sana mkuu, hongera
 
Watu wengine hata wazazi wao wasingeoana ili wasiwepo duniani maana ni matatizo kuliko miaka 50 ya CCM

mkuu sio kila mtoto ni zao la ndoa, waombe radhi wote waliozaliwa nje ya ndoa
 
Hiyo ni laana unamuhitaji YESU akuweke huru maana umefungwa na pepo la ngono hata hujitambui

ambae hajawahi kufanya ngono na awe wa kwanza kunyoosha kidole juu
 
Huyu bado mtoto mdogo mhurumieni tu akikua atajua ujinga aliokuwa akifikiria.

mzee wa funny umemsikia Mjuni Lwambo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…