Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 42,451
- 50,183
Habari wana Jf,
Dada yangu ana mwanae alikuwa anasoma shule ya private hapo Daresalaam maeneo Ya Tegeta , sasa kuna kipindi alisimamishwa anadaiwa ada kiasi cha 320,000.
Ña yeye kwakuwa uchumi wake umeyumba akahamua amuhamishie mwanae shule ya serikali darasa la nne, sasa amejaribu kufuatilia uhamisho kule ktk shule ya private,, uhamisho upo tayari Mwl mkuu alishaufuatilia,
Lakini wamegoma kumpa mpka alipe deni lao, na Kuna kipindi kirefu mtoto walimsimamisha akawa asomi, kibaya zaidi na kule shule Ya serikali mtoto amerudishwa mpaka aende na uhamisho,
Amejaribu kuwaomba kule shule ya private ikibidi waandikishiane, bado wamegoma wao wanataka pesa ndio watoe uhamisho,
Ivi ni hatua gani anaweza akachukua, maana nahisi ana adhibiwa mtoto Kwa kosa lisilomuhusu,,
Hilo eneo halina Afisa elimu wa kusaidia kumaliza utata ili mtoto aendelee kupata haki yake ya msingi