Kuna wimbi kubwa la watu wanaozaliwa mjini hawana ukaribu na vijiji vyao na watoto wao hawajui asili yao

R-K-O

JF-Expert Member
Jun 27, 2023
482
2,138
Ni vema sana kutembelea kijijini kwenu mara kwa mara kuendeleza ukaribu na sehemu yako ya asili, likizo ya wiki mbili si mbaya mara moja kila mwaka,

Kuna wimbi kubwa kwa watu mijini hawana ukaribu kabisa na sehemu zao za asili, Unakuta mtu alipelekwa huko kijijini mara mbili tu akiwa mdogo na ndio imetoka hio, hapo kwa kawaida hakuna ukaribu wowote maana hata watu aliowakuta udogoni washapitia mabadiliko mengi.

Wengine ndio kabisa hata kwao huko hawakujui, wapo mijini tu.

Hii hali ni mbaya sana, watoto kila mwaka inabidi wazoeshwe kupajua asili yao ilipo nao waendeleze utamaduni huu kwa vizazi vijavyo visisahau asili yao.

Hii huwa inaleta hata kiu ya kupaendeleza kwenu, mnaishi mjini nyumba nzuri ila kijijini kwenu nyumba inatia aibu, hii inaleta hasira ya kutaka kupaendeleza kwenu

Mnaishi mjini sehemu nzuri ila kijijini kuna nyumba mbili tu nzuri za maprofesa ambao hawajasahau kwao, hii ni aibu, hapa mkianza utamaduni wa kurudi kwenu nyumba nzuri zitazidi.
 
Haya ni moja ya madhara ya maendeleo ya dunia na watu kuhamahama.

Baba mmakonde kaenda Morogoro kakutana na Manka wamefunga ndoa na kuzaa watoto Morogoro ambao nao wanakwenda kutafuta maisha Mbeya, wanakutana na Mhaya Mbeya wanaoana.

Miaka ijayo hata Makabira na dini vitapotea.
 
Watu wanapaswa wawe wema na wachapakazi popote walipo,kwa wale waliopata bahati ya kufahamu vijiji vyao na wanatembelea mara kwa mara ni jambo jema,ama wale ambao hawakupata fursa hiyo ni vema kupambana hapo hapo na kuwalea watoto wao vema.
 
Hata mtoto nae kuna siku atakuwa mkubwa, anaenda kuwa mgeni wan ani akitaka kwenda kijijini ?

Matokeo yake ndio unakuta kuna watu wana maendeleo wanataka kuendeleza kwao ila hawajui pa kuanzia,
Aende kijijini akafanye nini wakati yeye amezaliwa mjini? Pengine bibi na babu wameshakufa zamani hata akienda anakuwa mgeni kabisa.

Kama ameamua kusaidia asaidie tu lakini siyo lazima kuwa awe 'mwanakijiji'.
 
Aende kijijini akafanye nini wakati yeye amezaliwa mjini? Pengine bibi na babu wameshakufa zamani hata akienda anakuwa mgeni kabisa.

Kama ameamua kusaidia asaidie tu lakini siyo lazima kuwa awe 'mwanakijiji'.
Kama mtu anaenda kijijini tangu mdogo anaanza kupazoea na kuzoeana na ndugu zake wa huko, hii ni sababu tosha ya kwenda kijininj kwao mara kwa mara
 
Tatzo uchawi umezidi vijijini
Unajua tusidanganyane hapa sehemu kubwa sana ya jamii saizi inafanya maendeleo hata kijijini tu! Na hizo ni dhana tu ambazo uhalisia wake ni mdogo sana kwa sasa! Na kwa sehemu kubwa watu mpaka vijijini wanajenga nyumba nzuri tu ila kwa vile wengi wamejificha mjini wanaamini kubwa maisha ni town lakini uhalisia unawez kujikuta watu kijijini wananyumba nzuri kuliko hata wanaokaa mjini!
Na kuwapeleka watoto kijijini ni jambo jema hususani katika kuwafanya wajue maisha tofauti na ya mjini na hii itawasaidia sana katika maisha yao maana wanaweza kuajiriwa au kujiajiri katika maeneo tofauti na mjini!
Kwa kifupi toafauti ya maisha ya mjini na kijijini kwa sasa ni ndogo sana kutokana na mfumo wa maisha ulivyobadilika!
 
Haya ni moja ya madhara ya maendeleo ya dunia na watu kuhamahama.

Baba mmakonde kaenda Morogoro kakutana na Manka wamefunga ndoa na kuzaa watoto Morogoro ambao nao wanakwenda kutafuta maisha Mbeya, wanakutana na Mhaya Mbeya wanaoana.

Miaka ijayo hata Makabira na dini vitapotea.
Mkuu, makabila yameanza kutoweka taratibu tena kistarabu. Huko Ulaya Dini nazo zinaanza.
 
Kuna watu humu wakishushwa na gari stand ya wilaya ili wafike kwao itabidi wasubirie gari la mkaa
sasa mtu kama huyu akiwaza hilo balaa anaona ajifariji tu eti mimi born town.
Born town wakati ukikata moto mzoga unapelekwa kule kule.
 
Ni vema sana kutembelea kijijini kwenu mara kwa mara kuendeleza ukaribu na sehemu yako ya asili, likizo ya wiki mbili si mbaya mara moja kila mwaka,

Kuna wimbi kubwa kwa watu mijini hawana ukaribu kabisa na sehemu zao za asili, Unakuta mtu alipelekwa huko kijijini mara mbili tu akiwa mdogo na ndio imetoka hio, hapo kwa kawaida hakuna ukaribu wowote maana hata watu aliowakuta udogoni washapitia mabadiliko mengi.

Wengine ndio kabisa hata kwao huko hawakujui, wapo mijini tu.

Hii hali ni mbaya sana, watoto kila mwaka inabidi wazoeshwe kupajua asili yao ilipo nao waendeleze utamaduni huu kwa vizazi vijavyo visisahau asili yao.

Hii huwa inaleta hata kiu ya kupaendeleza kwenu, mnaishi mjini nyumba nzuri ila kijijini kwenu nyumba inatia aibu, hii inaleta hasira ya kutaka kupaendeleza kwenu

Mnaishi mjini sehemu nzuri ila kijijini kuna nyumba mbili tu nzuri za maprofesa ambao hawajasahau kwao, hii ni aibu, hapa mkianza utamaduni wa kurudi kwenu nyumba nzuri zitazidi.
Wengi vijiji vilisambaratika kwa ujumla walikwisha hama.
 
Kosa la Nani sasa? Mfano mimi mama yangu (Marehemu) alizaliwa na kukulia Shinyanga mjini mtaa wa viwandani! Mama yake (Bibi) na baba yake (babu) washafariki hpo nyumbani hakunaga mtu tena nyumba iliyokuwepo imepangishwa ndugu wote wako sehemu tofauti tofauti. Upande wa baba baba yangu alizaliwa na kukulia Misungwi wazazi wake (babu na bibi) washafariki hakuna hata ndugu baba wadogo na wakubwa au mashangazi wanaoishi huko nyumba zipo zimepangishwa kwa wanafunzi wa chuo cha kilimo ukiriguru… wazazi wangu walikutana Arusha nmezaliwa na kukulia Arusha ingawa kijijini tulikuwa tunaenda. Kwa upande wa mke wangu Mama yake alizaliwa Songwe Mbeya Ila alikuja kutafta Arusha, baada ya maeneo Yao kuchukuliwa kupisha upanuzi wa uwanja walilipwa na kila mtu kuhamia kwake (bibi yake) alihamishia makazi Arusha, upande wa baba yake nae hawako kijijin kila mtu alishaondoka Bariadi na wako mijini kutafuta. Sasa watoto wangu wataenda kijijin wapi?? Bibi mzaa baba (mama yangu) kazikwa Arusha baba yangu (babu Yao) anaishi Moshono Arusha. Kwa upande wa mama Yao bibi mzaa mama (Mama mkwe) amezikwa Arusha baba mkwe (babu Yao) anaishi Njiro Arusha. Sasa unafkir I hao wanangu wataenda kijijin wapi? Hamna kijiji cha kwenda kusalimia na wao utwalaumu?? Saa nyngne ni nature inaamua hamna namna
 
Kosa la Nani sasa? Mfano mimi mama yangu (Marehemu) alizaliwa na kukulia Shinyanga mjini mtaa wa viwandani! Mama yake (Bibi) na baba yake (babu) washafariki hpo nyumbani hakunaga mtu tena nyumba iliyokuwepo imepangishwa ndugu wote wako sehemu tofauti tofauti. Upande wa baba baba yangu alizaliwa na kukulia Misungwi wazazi wake (babu na bibi) washafariki hakuna hata ndugu baba wadogo na wakubwa au mashangazi wanaoishi huko nyumba zipo zimepangishwa kwa wanafunzi wa chuo cha kilimo ukiriguru… wazazi wangu walikutana Arusha nmezaliwa na kukulia Arusha ingawa kijijini tulikuwa tunaenda. Kwa upande wa mke wangu Mama yake alizaliwa Songwe Mbeya Ila alikuja kutafta Arusha, baada ya maeneo Yao kuchukuliwa kupisha upanuzi wa uwanja walilipwa na kila mtu kuhamia kwake (bibi yake) alihamishia makazi Arusha, upande wa baba yake nae hawako kijijin kila mtu alishaondoka Bariadi na wako mijini kutafuta. Sasa watoto wangu wataenda kijijin wapi?? Bibi mzaa baba (mama yangu) kazikwa Arusha baba yangu (babu Yao) anaishi Moshono Arusha. Kwa upande wa mama Yao bibi mzaa mama (Mama mkwe) amezikwa Arusha baba mkwe (babu Yao) anaishi Njiro Arusha. Sasa unafkir I hao wanangu wataenda kijijin wapi? Hamna kijiji cha kwenda kusalimia na wao utwalaumu?? Saa nyngne ni nature inaamua hamna namna
Wapeleke njiro na moshono tu hao watoto napo vijijini
 
Ni vema sana kutembelea kijijini kwenu mara kwa mara kuendeleza ukaribu na sehemu yako ya asili, likizo ya wiki mbili si mbaya mara moja kila mwaka,

Kuna wimbi kubwa kwa watu mijini hawana ukaribu kabisa na sehemu zao za asili, Unakuta mtu alipelekwa huko kijijini mara mbili tu akiwa mdogo na ndio imetoka hio, hapo kwa kawaida hakuna ukaribu wowote maana hata watu aliowakuta udogoni washapitia mabadiliko mengi.

Wengine ndio kabisa hata kwao huko hawakujui, wapo mijini tu.

Hii hali ni mbaya sana, watoto kila mwaka inabidi wazoeshwe kupajua asili yao ilipo nao waendeleze utamaduni huu kwa vizazi vijavyo visisahau asili yao.

Hii huwa inaleta hata kiu ya kupaendeleza kwenu, mnaishi mjini nyumba nzuri ila kijijini kwenu nyumba inatia aibu, hii inaleta hasira ya kutaka kupaendeleza kwenu

Mnaishi mjini sehemu nzuri ila kijijini kuna nyumba mbili tu nzuri za maprofesa ambao hawajasahau kwao, hii ni aibu, hapa mkianza utamaduni wa kurudi kwenu nyumba nzuri zitazidi.
Mkuu kuijua asili so what next..!?
Mambo hoyo yashaa pitwa na wakati kiongozi.
 
Back
Top Bottom