Kuna watumishi wanajituma sana!

Kuna watumishi wanajituma sana!

Nikisoma shuhuda kama hizi huwa napata amani kidogo, maana kwa kweli nilisha generalise kuwa watu ishi wote wa umma ni mashetani, hasa polisi, mahakama, uhamiaji, na hospitalini , huko kote niliishia kupata si huduma baki adhabu kali iliyosababisha nijute kuzaliwa Tanzania, ila kama bado kuna watu wema hata wachache kama huyo Jose nawa ombea kwa Mungu awape mlima wa baraka, si rahisi kuwa mwema kwenye mfumo uliooza, hata kama mtoa mada ndiye Jose mwenyewe atakuwa anaiishi hadithi yake hii tamu yenye kutupa matumaini sisi tulio wahitaji, Mungu akubariki sana Jose.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Kweli kabisa mkuu, japokuwa mimi si jose
 
Mi nasema ukweli! Kuna Mama mmoja pale Baraza la Aridhi na Nyumba Tanga anajiita D. W. Mangure ndiyo Mwenyekiti pale, yule Mama ni mlaa rushwa sana,na anapenda kuendesha Magari makubwa Kama Alfadi!! Naomba Takukuru Makao makuu wamchunguze kimya kimya, hasa kwenye hukumu zake anazotoa, huwa anawa fever sana wenye pesa bila hata ya aibu! Yaani hukumu zake zinatofautiana hadi na maoni ya Wazee wa Baraza lake!!
Hawa ni kuwabainisha kama hivi ndo dawa yao, tusikae kimya
 
Habari wakuu,

Kweli nimeamiani kwenye kundi la kenge huwezi kosa na mamba. Na pia samaki mmoja akioza si kwamba wote wataoza.

Nimeongea hayo kwa kujithibitishia kwa kuona baadhi ya watumishi wa umma wanafanya kazi zao kwa umakini na kwa weledi mkubwa sana. Kweli kuna watumishi waliapa kiapo cha haki kabisa.

Nilienda almost mara tatu pale branch ya RITA manispaa karibu na uwanja wa TAIFA , nikakutana na mwamba mmoja anaitwa Jose, huyu mwamba anapiga kazi kisawa sawa yaani, yaani yuko tayari hata asile mlo wowote ule ila ahakikishe wateja wake wote wamepata huduma.

Mwamba mcheshi na akiwa kazini anapiga kazi like hakuna kesho. Jamaa hana dharau na sio mtu wa kufokea wateja kama wafanyavyo baadhi ya watumishi. Pia mwamba ana nidhamu na ni mtu makini sana.

Kuna siku jamaa alizidisha muda wake wa kazi kutoka saa 6 mpaka 12 jioni, kwa kuhudumia wateja. Huyu mwamba aliniaminisha kuwa si watumishi wote ni wahuni. Bali kuna wapiga kazi kweli kweli.

Hongera sana mwamba kama umesoma uzi huu basi big up man, soon utatoka sehemu moja na kwenda nyingine kaka
Kweli aisee. Hata mimi nilikutana na Mwl kwenye shule moja ya sekondari kule Kigoma aisee alikuwa Second Master jamaa anapiga kazi hadi nilimkubali. Alinipa moyo sana. Na ilikuwa Raha sana kufanya kazi na yule mtu. Nilishamsahau jina maana ni kitambo sana.

Mwamba Mwingine nilikutana naye NMB kule zanzibar Tawi la Malindi Tall fulani hivi ananyoa Pank amazing jamaa anapiga kazi hana mchezo.

Simjui jina pia lakini Pongezi hizi zimfikie popote alipo.

NMN Malindi Zanzibar huyu Benk Teller is amazing
 
Cha ajabu katika utumishi wa umma ukiwa mchapakazi unaonekana ni tatizo.....Tuna safari ndefu sana.
Wakati wewe uko mwaminifu ktk kazi wengine wako bize na connection na mafisadi tu. Na hapo ndio unaonekana mkorofi 😅😅
 
Mi nasema ukweli! Kuna Mama mmoja pale Baraza la Aridhi na Nyumba Tanga anajiita D. W. Mangure ndiyo Mwenyekiti pale, yule Mama ni mlaa rushwa sana,na anapenda kuendesha Magari makubwa Kama Alfadi!! Naomba Takukuru Makao makuu wamchunguze kimya kimya, hasa kwenye hukumu zake anazotoa, huwa anawa fever sana wenye pesa bila hata ya aibu! Yaani hukumu zake zinatofautiana hadi na maoni ya Wazee wa Baraza lake!!
Bora tuwe tunawachana hivyo hivyo maana Takukuru haina kazi
 
Wakati wewe uko mwaminifu ktk kazi wengine wako bize na connection na mafisadi tu. Na hapo ndio unaonekana mkorofi 😅😅
Inashusha sana morali ya kazi, 2021 ilikua ndio mwisho wangu kufanya kazi kama punda....haitakaa ijirudie labda kazi zangu binafsi ila sio za umma, nilijifunza mengi sana ukifanya kazi kwa kujitoa unakua ni tatizo.
 
Inashusha sana morali ya kazi, 2021 ilikua ndio mwisho wangu kufanya kazi kama punda....haitakaa ijirudie labda kazi zangu binafsi ila sio za umma, nilijifunza mengi sana ukifanya kazi kwa kujitoa unakua ni tatizo.
Ndiyo unless uwe mtu wao( satan company)
 
Mimi pale Chuo Cha Usimamizi wa Fedha, Ifm nilikutana na mama mmoja loan officer mnyakyusa alinisaidia sana kwa kweli, na ni mpiga kazi sawa sawa sio mtu wa kujiona wala majivuno, namshukuru sana
 
Kichefuchefu kipo Manispaa ya Kinondoni aisee, unaenda unahitaji kushughulikiwa jambo lako kupata jibu mtu hadi amalizie kutuma emoj kwanza...
 
Kichefuchefu kipo Manispaa ya Kinondoni aisee, unaenda unahitaji kushughulikiwa jambo lako kupata jibu mtu hadi amalizie kutuma emoj kwanza...
Kuna umuhimu mkubwa sana wa Mama kua mkali kwa Watoto wake ambao ndiyo Watumishi wa Umma, Mtoto ukimdekeza sana anaharibikiwa, Mama ajaribu kua mkali kidogo Kama alivyokua Marehemu Baba!!
 
Kuna dada mmoja wilaya flani mkoa wa Pwani asee dada anapiga kazi sana Mungu ambariki sana.
Mtaje kwa majina Mkuu.

Taifa linahitaji watu wa namna hii.

Siyo haya mabumunda mengine ukienda Ofisini kwao wanakuona kama umeenda kuwakera tu..

Hongera sana Jose wa Rita na Dada wa Mkoani Pwani. Mungu awabariki sana muendelee na Moyo huo wa kuhudumia Watanzania kwa nidhamu.
 
Sema Jose unatafuta cheo sana, unahisi Alex akiona hii post ndio atakupandisha? Pale pamekaa kikabila mchizi wangu, we komaa na mishe zingine ila usitarajie kutoka kupitia hiyo kazi
 
Sema Jose unatafuta cheo sana, unahisi Alex akiona hii post ndio atakupandisha? Pale pamekaa kikabila mchizi wangu, we komaa na mishe zingine ila usitarajie kutoka kupitia hiyo kazi
Unamjua jose mwenyewe pale RITA
 
hajanunua gari bado huyo..hajapata ata 20ml loan.. kwa kifupi fatilia vzuri utakuta bado yupo kwenye probational contract.
 
Back
Top Bottom