Kuna wanadamu na wanadamu viumbe vipya. Hawa wanadamu viumbe vipya ni akina nani hasa?

Urban86

JF-Expert Member
Jan 26, 2014
276
127
MWAMINI NI #KIUMBE_KIPYA

Je unajua nini kilitokea katika kuokolewa kwako?

Je! Unafahamu umekuwa nini mara baada ya kuwa na imani katika kufa kuzikwa na kufufuka kwa Kristo ili wewe uhesabiwe haki?

Wewe umekuwa #Kiumbe #kipya!

2Wakorintho 5:17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

Wagalatia 6:15 Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya.

Neno “kiumbe kipya” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “kainos ktisis” ambalo lina maana ya mtu mpya, kiumbe kipya (new specie, a new person,), yote pamoja katika Kristo.

Upya huu siyo habari ya kitu cha zamani au kikuukuu kilichofanyiwa marekebisho, hapana! Ni upya ambao haukuwapo, kitu ambacho hakina historia, hakikuwahi kuwepo (A real brand new thing). Ndiyo sababu mahali pengine jambo hili linaitwa uzao mpya, a new birth.

Upya huu ni kwa sababu upo ndani ya Kristo, kwa Imani katika Kristo; imani katika Injili. Upya huu sio badiliko la tabia, upya huu ni habari ya asili yako mpya katika Kristo.

Mwamini, kwa utambulisho pamoja na Kristo (identification with Christ) alizikwa pamoja na Kristo, alifufuka pamoja naye na ana maisha mapya.

Warumi 6:4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.[5] Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake; [6] mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena; [7] kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi. [8] Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye;

Wakolosai 3:1 Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu.

Kwa hio katika mind ya Mungu, Kristo alipokufa, ulikufa naye (utu wako wa kale/dhambi, au asili yako ya dhambi) ilikufa pamoja naye. Na Kristo alipofufuka ulifufuka pamoja naye, ukawa na utu mpya, ukawa umezaliwa kiumbe kipya. Huku ndiko kubatizwa katika Kristo, kuzamishwa kabisa ndani ya utu wa Kristo na kutambulishwa pamoja na huo kiasi unakua kitu kimoja (roho moja) na YEYE! (to be totally immersed and identified with Christ)

Kwa hiyo mwamini ndani ya Kristo hana historia ya nyuma, ndani ya Kristo hapana hata kumbukumbu ya dhambi na makosa kabla hajaamini. Ni kama mtoto mchanga aliyezaliwa- hana historia ya nyuma, ni mpya!

Ni makosa mwamini kusimama mbele ya kusanyiko akishuhudia maisha yake ya nyuma, jinsi alivyokua mchawi, mzinzi, mlevi, mwizi, muuaji… hayo ni mambo ya mtu aliyekufa, unaletaje habari za wafu katikati ya walio hai? Ushuhuda wa mwamini siyo huo, ushuhuda wake ni juu ya kazi ya Kristo na matokeo au impact yake kwake. Ndiyo sababu mwandishi wa Waebrania anasema tuyashike sana maungamo yetu, haya maungamo si juu ya tabia zetu kabla hatujaamini bali ni juu ya kazi aliyoimaliza Kristo kwa ajili yetu na matokeo yake.

Tunakiri na kushuhudia vile tulivyo ndani ya Kristo;
uzao mteule, taifa takatifu, haki, hekima, utakatifu, ukombozi, ukuhani wa kifalme, wenye masamaha ya milele, walio keti naye, wenyeji wa mbinguni, kanisa la wazaliwa wa kwanza, watu wa milki ya Mungu, wenye baraka zote katika ulimwengu wa roho, wenye kukaliwa na Roho wa Mungu, wenye maisha na uzima wa Mungu ndani yetu, wenye mamlaka dhidi ya falme zote na mamlaka, wamoja na Kristo, nuru, hekalu la Mungu, chumvi ya ulimwengu, utukufu wa Mungu, washindi, wateule, wenye pendo la Mungu, walioshirikishwa tabia ya kiungu, na kadhalika.. (hivyo ndivyo tulivyo katika Kristo, hayo ndiyo maungamo yetu)

Yes! Ndivyo ilivyo, Mwamini ni kazi ya Mungu:

Waefeso 2:10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Neno ni kazi yake ina maana ya kuwa mwamini ni kazi ya mikono yake (kito -masterpiece). Hii inaelezea ukamilifu wa mwamini, yeye ni uumbaji wa Mungu mwenyewe.

Si uumbaji wake, siyo jitihada zake, ni kazi ya Mungu, ametokana na Mungu, mtu mkamilifu, mtu kutoka/aliyezaliwa juu. Si wa udongo, si wa ulimwengu, amezaliwa mbinguni.
Usikubali mtu kukwambia kuwa utakuja kuwa kiumbe kipya siku ukiwa na tabia bora, wewe ni kiumbe kipya leo! Maandiko yanasema “umekuwa” siyo “utakuwa”

Hivyo ishi katika ufahamu wa kweli hii, huku ukibadili ufahamu na nia yako kwa neno la Mungu ili uchukue sura ya mtu wako wa ndani aliye mpya na mkamilifu. Kadri unavyokua katika kweli ya wewe ni nani katika Kristo, utakuwa ukibadilika katika mwenendo wako wa nje siku hadi siku.

Ndiyo sababu Paulo anasema; “bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia (ufahamu) zenu..”

Baada ya kuokolewa, umekwisha kuwa kiumbe kipya, kazi iliyopo ni kugeuzwa kwa ufahamu wako ili ufanane na mfano wa ule utu mpya ulio umbwa na matokeo yake ni ukuaji wako kiroho, ni tunda la roho, ni maisha yenye kuidhihirisha haki uliyo nayo tayari. Hivyo, Jifunze Kristo, Jifunze Neno la Mungu.

Usionewe!

Wewe ni Kiumbe kipya! Mwana wa Mungu kabisa!

Unajua nakupenda.

Felician Makarios
30 July 2019

Kainos Creation
 
MWAMINI NI #KIUMBE_KIPYA

Je unajua nini kilitokea katika kuokolewa kwako?

Je! Unafahamu umekuwa nini mara baada ya kuwa na imani katika kufa kuzikwa na kufufuka kwa Kristo ili wewe uhesabiwe haki?

Wewe umekuwa #Kiumbe #kipya!

2Wakorintho 5:17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

Wagalatia 6:15 Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya.

Neno “kiumbe kipya” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “kainos ktisis” ambalo lina maana ya mtu mpya, kiumbe kipya (new specie, a new person,), yote pamoja katika Kristo.

Upya huu siyo habari ya kitu cha zamani au kikuukuu kilichofanyiwa marekebisho, hapana! Ni upya ambao haukuwapo, kitu ambacho hakina historia, hakikuwahi kuwepo (A real brand new thing). Ndiyo sababu mahali pengine jambo hili linaitwa uzao mpya, a new birth.

Upya huu ni kwa sababu upo ndani ya Kristo, kwa Imani katika Kristo; imani katika Injili. Upya huu sio badiliko la tabia, upya huu ni habari ya asili yako mpya katika Kristo.

Mwamini, kwa utambulisho pamoja na Kristo (identification with Christ) alizikwa pamoja na Kristo, alifufuka pamoja naye na ana maisha mapya.

Warumi 6:4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.[5] Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake; [6] mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena; [7] kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi. [8] Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye;

Wakolosai 3:1 Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu.

Kwa hio katika mind ya Mungu, Kristo alipokufa, ulikufa naye (utu wako wa kale/dhambi, au asili yako ya dhambi) ilikufa pamoja naye. Na Kristo alipofufuka ulifufuka pamoja naye, ukawa na utu mpya, ukawa umezaliwa kiumbe kipya. Huku ndiko kubatizwa katika Kristo, kuzamishwa kabisa ndani ya utu wa Kristo na kutambulishwa pamoja na huo kiasi unakua kitu kimoja (roho moja) na YEYE! (to be totally immersed and identified with Christ)

Kwa hiyo mwamini ndani ya Kristo hana historia ya nyuma, ndani ya Kristo hapana hata kumbukumbu ya dhambi na makosa kabla hajaamini. Ni kama mtoto mchanga aliyezaliwa- hana historia ya nyuma, ni mpya!

Ni makosa mwamini kusimama mbele ya kusanyiko akishuhudia maisha yake ya nyuma, jinsi alivyokua mchawi, mzinzi, mlevi, mwizi, muuaji… hayo ni mambo ya mtu aliyekufa, unaletaje habari za wafu katikati ya walio hai? Ushuhuda wa mwamini siyo huo, ushuhuda wake ni juu ya kazi ya Kristo na matokeo au impact yake kwake. Ndiyo sababu mwandishi wa Waebrania anasema tuyashike sana maungamo yetu, haya maungamo si juu ya tabia zetu kabla hatujaamini bali ni juu ya kazi aliyoimaliza Kristo kwa ajili yetu na matokeo yake.

Tunakiri na kushuhudia vile tulivyo ndani ya Kristo;
uzao mteule, taifa takatifu, haki, hekima, utakatifu, ukombozi, ukuhani wa kifalme, wenye masamaha ya milele, walio keti naye, wenyeji wa mbinguni, kanisa la wazaliwa wa kwanza, watu wa milki ya Mungu, wenye baraka zote katika ulimwengu wa roho, wenye kukaliwa na Roho wa Mungu, wenye maisha na uzima wa Mungu ndani yetu, wenye mamlaka dhidi ya falme zote na mamlaka, wamoja na Kristo, nuru, hekalu la Mungu, chumvi ya ulimwengu, utukufu wa Mungu, washindi, wateule, wenye pendo la Mungu, walioshirikishwa tabia ya kiungu, na kadhalika.. (hivyo ndivyo tulivyo katika Kristo, hayo ndiyo maungamo yetu)

Yes! Ndivyo ilivyo, Mwamini ni kazi ya Mungu:

Waefeso 2:10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Neno ni kazi yake ina maana ya kuwa mwamini ni kazi ya mikono yake (kito -masterpiece). Hii inaelezea ukamilifu wa mwamini, yeye ni uumbaji wa Mungu mwenyewe.

Si uumbaji wake, siyo jitihada zake, ni kazi ya Mungu, ametokana na Mungu, mtu mkamilifu, mtu kutoka/aliyezaliwa juu. Si wa udongo, si wa ulimwengu, amezaliwa mbinguni.
Usikubali mtu kukwambia kuwa utakuja kuwa kiumbe kipya siku ukiwa na tabia bora, wewe ni kiumbe kipya leo! Maandiko yanasema “umekuwa” siyo “utakuwa”

Hivyo ishi katika ufahamu wa kweli hii, huku ukibadili ufahamu na nia yako kwa neno la Mungu ili uchukue sura ya mtu wako wa ndani aliye mpya na mkamilifu. Kadri unavyokua katika kweli ya wewe ni nani katika Kristo, utakuwa ukibadilika katika mwenendo wako wa nje siku hadi siku.

Ndiyo sababu Paulo anasema; “bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia (ufahamu) zenu..”

Baada ya kuokolewa, umekwisha kuwa kiumbe kipya, kazi iliyopo ni kugeuzwa kwa ufahamu wako ili ufanane na mfano wa ule utu mpya ulio umbwa na matokeo yake ni ukuaji wako kiroho, ni tunda la roho, ni maisha yenye kuidhihirisha haki uliyo nayo tayari. Hivyo, Jifunze Kristo, Jifunze Neno la Mungu.

Usionewe!

Wewe ni Kiumbe kipya! Mwana wa Mungu kabisa!

Unajua nakupenda.

Felician Makarios
30 July 2019

Kainos Creation
Haaaa. Viumbe wapya ni wana ccccm.mm
 
MWAMINI NI #KIUMBE_KIPYA

Je unajua nini kilitokea katika kuokolewa kwako?

Je! Unafahamu umekuwa nini mara baada ya kuwa na imani katika kufa kuzikwa na kufufuka kwa Kristo ili wewe uhesabiwe haki?

Wewe umekuwa #Kiumbe #kipya!

2Wakorintho 5:17 Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

Wagalatia 6:15 Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya.

Neno “kiumbe kipya” limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “kainos ktisis” ambalo lina maana ya mtu mpya, kiumbe kipya (new specie, a new person,), yote pamoja katika Kristo.

Upya huu siyo habari ya kitu cha zamani au kikuukuu kilichofanyiwa marekebisho, hapana! Ni upya ambao haukuwapo, kitu ambacho hakina historia, hakikuwahi kuwepo (A real brand new thing). Ndiyo sababu mahali pengine jambo hili linaitwa uzao mpya, a new birth.

Upya huu ni kwa sababu upo ndani ya Kristo, kwa Imani katika Kristo; imani katika Injili. Upya huu sio badiliko la tabia, upya huu ni habari ya asili yako mpya katika Kristo.

Mwamini, kwa utambulisho pamoja na Kristo (identification with Christ) alizikwa pamoja na Kristo, alifufuka pamoja naye na ana maisha mapya.

Warumi 6:4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.[5] Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake; [6] mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena; [7] kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi. [8] Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye;

Wakolosai 3:1 Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu.

Kwa hio katika mind ya Mungu, Kristo alipokufa, ulikufa naye (utu wako wa kale/dhambi, au asili yako ya dhambi) ilikufa pamoja naye. Na Kristo alipofufuka ulifufuka pamoja naye, ukawa na utu mpya, ukawa umezaliwa kiumbe kipya. Huku ndiko kubatizwa katika Kristo, kuzamishwa kabisa ndani ya utu wa Kristo na kutambulishwa pamoja na huo kiasi unakua kitu kimoja (roho moja) na YEYE! (to be totally immersed and identified with Christ)

Kwa hiyo mwamini ndani ya Kristo hana historia ya nyuma, ndani ya Kristo hapana hata kumbukumbu ya dhambi na makosa kabla hajaamini. Ni kama mtoto mchanga aliyezaliwa- hana historia ya nyuma, ni mpya!

Ni makosa mwamini kusimama mbele ya kusanyiko akishuhudia maisha yake ya nyuma, jinsi alivyokua mchawi, mzinzi, mlevi, mwizi, muuaji… hayo ni mambo ya mtu aliyekufa, unaletaje habari za wafu katikati ya walio hai? Ushuhuda wa mwamini siyo huo, ushuhuda wake ni juu ya kazi ya Kristo na matokeo au impact yake kwake. Ndiyo sababu mwandishi wa Waebrania anasema tuyashike sana maungamo yetu, haya maungamo si juu ya tabia zetu kabla hatujaamini bali ni juu ya kazi aliyoimaliza Kristo kwa ajili yetu na matokeo yake.

Tunakiri na kushuhudia vile tulivyo ndani ya Kristo;
uzao mteule, taifa takatifu, haki, hekima, utakatifu, ukombozi, ukuhani wa kifalme, wenye masamaha ya milele, walio keti naye, wenyeji wa mbinguni, kanisa la wazaliwa wa kwanza, watu wa milki ya Mungu, wenye baraka zote katika ulimwengu wa roho, wenye kukaliwa na Roho wa Mungu, wenye maisha na uzima wa Mungu ndani yetu, wenye mamlaka dhidi ya falme zote na mamlaka, wamoja na Kristo, nuru, hekalu la Mungu, chumvi ya ulimwengu, utukufu wa Mungu, washindi, wateule, wenye pendo la Mungu, walioshirikishwa tabia ya kiungu, na kadhalika.. (hivyo ndivyo tulivyo katika Kristo, hayo ndiyo maungamo yetu)

Yes! Ndivyo ilivyo, Mwamini ni kazi ya Mungu:

Waefeso 2:10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Neno ni kazi yake ina maana ya kuwa mwamini ni kazi ya mikono yake (kito -masterpiece). Hii inaelezea ukamilifu wa mwamini, yeye ni uumbaji wa Mungu mwenyewe.

Si uumbaji wake, siyo jitihada zake, ni kazi ya Mungu, ametokana na Mungu, mtu mkamilifu, mtu kutoka/aliyezaliwa juu. Si wa udongo, si wa ulimwengu, amezaliwa mbinguni.
Usikubali mtu kukwambia kuwa utakuja kuwa kiumbe kipya siku ukiwa na tabia bora, wewe ni kiumbe kipya leo! Maandiko yanasema “umekuwa” siyo “utakuwa”

Hivyo ishi katika ufahamu wa kweli hii, huku ukibadili ufahamu na nia yako kwa neno la Mungu ili uchukue sura ya mtu wako wa ndani aliye mpya na mkamilifu. Kadri unavyokua katika kweli ya wewe ni nani katika Kristo, utakuwa ukibadilika katika mwenendo wako wa nje siku hadi siku.

Ndiyo sababu Paulo anasema; “bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia (ufahamu) zenu..”

Baada ya kuokolewa, umekwisha kuwa kiumbe kipya, kazi iliyopo ni kugeuzwa kwa ufahamu wako ili ufanane na mfano wa ule utu mpya ulio umbwa na matokeo yake ni ukuaji wako kiroho, ni tunda la roho, ni maisha yenye kuidhihirisha haki uliyo nayo tayari. Hivyo, Jifunze Kristo, Jifunze Neno la Mungu.

Usionewe!

Wewe ni Kiumbe kipya! Mwana wa Mungu kabisa!

Unajua nakupenda.

Felician Makarios
30 July 2019

Kainos Creation

Kwanini watu huanguka tena baada ya kuwa viumbe vipya huwa Mbwa au kama nguruwe kwa kurudia matapashi
 
Kwanini watu huanguka tena baada ya kuwa viumbe vipya huwa Mbwa au kama nguruwe kwa kurudia matapashi
Mstari unaojaribu kuurejea katika muktadha wake mwandishi alipotumia neno "nguruwe au mbwa" hajukuwa anamzunguzia mwamini ambaye ni kiumbe kipya. Bali alikuwa anamrejelea asiyeamini. Mbwa kurudia matapishi yake ina maana asili yake toka mwanzo alikuwa ni mbwa ndio maana akarudi kwenye asili yake. Hivyo hivyo na nguruwe kurudi katika tope.

Mwamini kwa asili ni mwana wa Mungu na ataendelea kubaki mwana wa Mungu. Asili yake mpya ya uwana wa Mungu haiwezi kupotea kwamwe kuwa kitu kingine kisicho asili yake.

Kuelewa zaidi utambulisho huu mpya wa mwamini sikiliza somo linaitwa "Utambulisho wa Mwamini sehemu ya 1 hadi ya 4" katika channel ya Telegram ya "KainosMedia"
 
UMEKOMBOLEWA? INA MAANA GANI KUKOMBOLEWA?

Na Pastor Felician Makarios

Wakati mwingi tunaimba tumekombolewa na Yesu halafu hatukai katika kina cha maana ya maneno hayo. Tunaimba au kutamka tu kama kasuku.

Imekua kawaida katika jamii ya Kikristo, kusema tu maneno ya kidini hata kama hatuamini tunachosema au hatuelewi tunachosema.

Neno "ukombozi" linarejea gharama iliyolipwa, hiyo gharama ni thamani ya mtu.

1Timotheo 2:5 Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; 6 ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.

Neno "ukombozi" limetafsiriwa kutoka katika neno la kigiriki 'lutron' linalomaanisha gharama iliyolipwa.

Kwa hiyo Paulo anasema Yesu alijitoa kua gharama inayolipwa

Mathayo 26:28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

Damu ya Yesu (maisha ya Yesu) ndiyo gharama iliyolipwa kwaajili ya dhambi.

Tazama hapa,

Luka 22:20 Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]
Hapa tena,

Warumi 3:23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 25 ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa.

Damu ya Yesu ndiyo gharama iliyolipwa, ni bure, na ni katika Kristo. Hakuna gharama nyingine inayohitajika kwa ajili ya ukombozi.

Angalia hapa, nani aliyenunua;

Matendo 20:28 Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.

Hapa tena;

Wagalatia 3:13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;

Kwa kifo chake, alitukomboa kutoka katika dhambi.

Ni kazi ya Kristo, siyo kazi yetu. Ni yeye mwenye kufanya ukombozi.

Angalia hapa;

Tito 2:14 ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.

Tumekombolewa na maasi yote, tumesafishwa kuwa miliki yake na ndipo tuna juhudi katika kutenda mema.

Si kwa matendo ya haki tuliyotenda;

Tito 3:4 Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa,alituokoa; 5 si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu; 6 ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu; 7 ili tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, kama lilivyo tumaini letu.

Gharama ililipwa kwa niaba yetu.

1Wakorintho 6:19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; 20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

Hapa tena;

1Wakorintho 7:23 Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu.

Hivyo, tulinunuliwa kwa gharama iliyolipwa, kwahiyo ukombozi wetu ni katika Kristo.
Hivyo tunao ukombozi, siyo tutakua na ukombozi; ni sasa, tunamiliki ukombozi.

Waefeso 1:7 Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.
Neema maana yake ni kwamba ilitolewa bure, na msamaha wa dhambi unapatikana kwa sababu ya wingi wa neema yake.

Wakolosai 1:12 mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru. 13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; 14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

Katika ukombozi, tuna masamaha ya dhambi. Mungu hakuomba badiliko la moyo kutoka kwetu kabla hajatusamehe; ilitolewa kwetu kwa msingi wa kile ambacho Kristo amefanya.

Hapahitaji kujitutumua, ni kazi yake. Ni neema yake kwetu.

Waebrania 9:11 Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu, 12 wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele.

Alipata ukombozi wa milele kwaajili yetu kwa damu yake! Huku ndiko kuachiliwa kabisa kutoka kwenye dhambi.

Mwamini hayupo tena katika dhambi, ameachiliwa kabisa, amekombolewa milele.
Kumbuka kwamba Wokovu una msingi katika kweli tatu; kifo cha Yesu, kuzikwa kwake, ufufuo wa Yesu katika mwili na kwasababu hiyo kupaa kwake.

1Wakorintho 15:17 Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.

Maana kuwepo kwa dhambi kunategemea kutofufuka kwa Yesu. Ikiwa alifufuka basi imani yetu siyo bure na tayari tuna msamaha wa dhambi, hatumo dhambini tena.

Ufufuo wa Yesu ni ushahidi kwamba gharama imelipwa kwaajili ya dhambi. Ufufuo wa Yesu unathibitisha kazi ya ukombozi. Inaweka muhuri wa mwisho kabisa na inatoa uhakika wa wokovu wa milele kwa mwamini.

Angalia hapa;

Waebrania 5:9 naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;

Wanaomtii katika matumizi ya mwandishi wa Waebrania inarejea “wanaomwamini”. Kuamini ndiko kutii.

Wokovu huo, unaitwa wa milele. na Kristo ndiye anayeutunza. UKOMBOZI WA MILELE
Siyo wewe unayetunza, hapana. Ni mkombozi anayetunza ukombozi wa aliyekombolewa.
Angalia mstari huu.

Waebrania 7:22 basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi...., 25 Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

Mwandishi anasema anaweza kuwaokoa kabisa, ni muhimu kuzingatia hili

Neno kabisa ni neno milele katika andiko hilo. Hiyo inamaanisha kwamba Yesu anaokoa milele kwa sababu amefufuka na yu hai hivi leo. Yaani Yesu haokoi kwa mwaka mmoja, hapana, anaokoa kwa milele.

1Yohana 2:1 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, 2 naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.

Yeye ndiye mtetezi wetu mbele za Baba. Hivyo, hatuhukumiwi kwa dhambi tena.

Uwepo wake mbele za Baba siku zote ndiyo utetezi wetu na ndiyo hakikisho la usalama wa kile tumepokea katika Yeye, kwa kua yuko hai milele na sisi tuko hai milele. Dhambi haina nguvu tena, tuna huduma yake ya ukuhani kwa ajili yetu milele.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

Mwamini yuko huru kutoka katika hukumu. Hakuna ina maana ya hakuna, usiweke “lakini”, hiyo inatoka kwa adui.

Waebrania 8:8 Maana, awalaumupo, asema Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, Nami nitawatimizia nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda agano jipya; 9 Halitakuwa kama agano lile nililoagana na baba zao, Katika siku ile nilipowashika mikono yao niwatoe katika nchi ya Misri. Kwa sababu hawakudumu katika agano langu, Mimi nami sikuwajali asema Bwana. 10 Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu. 11 Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao. 12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena.

Hakuna kumbukumbu ya dhambi katika wokovu, Mungu hashikilii dhambi kwa mwamini.

Angalia hapa tena;

Waebrania 10:17 Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.
Wewe kwa nini unakumbuka dhambi zako? Yeye hakumbuki tena.

Unyenyekevu ni kukubali kile Mungu anasema kwako, hakumbuki! Usitake kuanza kukumbusha!

Katika uzao mpya, tuna zawadi ya kutokuwa na hukumu.

Waebrania 10:12 Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu; 13 tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake. 14 Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.

Chote ambacho Kristo amefanya, amekifanya milele na ameketi mkono wa kuumne wa Mungu.

Yesu hakufanya kazi ya siku mbili au ya kujirudia rudia.

Waebrania 13:5 Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.

Tazama sentensi, "sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa", inaonyesha kujitoa. Ni maneno ya uhakika (absolute words), ni ahadi yake na kujifunga kwake HATAKUACHA KAMWE!

Isitokee wakati wowote ukajiskia au kuona umeachwa, hawezi kukuacha kwa sababu yeyote ile. Kuwepo kwake pamoja na wewe kunategemea alichofanya Kristo na sio unachotenda wewe.

Waebrania 12:22 Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi, 23 mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika,
Umefika hauko safarini kuelekea. Wokovu wako au ukombozi wako ni halisi leo.

Waebrania 9:11 Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu, 12 wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele.

Gharama aliyolipa ni mara moja na milele. Halipi kila siku, hakusamehi kila siku. Umelipiwa milele, umesamehewe milele. Unyenyekevu ni kukubali neno lake. Acha kubishana naye, anasema amepata ukombozi wa milele.
Waebrania 9:15 Na kwa sababu hii ni mjumbe wa agano jipya, ili, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele.

Millele ni kinyume cha “ya muda tu”. Inamaanisha milele, kinachodumu. Wale waliomwamini Kristo wamepokea urithi wa milele kwa dhabihu ya Yesu ya mara moja kwa milele.

Utakua na maana sana ukikubaliana na neno lake ukaachana na stori za mtaani.

1Wathesalonike 5:23 Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo. 24 Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.

Haya hayakuwa maombi kwakuwa Paulo hakuwa anaomba kwasababu hatuombi kwaajili ya utakaso, ni kazi ya Mungu. Lakini Paulo alikua anasisitiza uaminifu wa Mungu hapa, anatuweka wakamilifu, watakatifu na salama. Anafanya hivyo kwa sababu YEYE NI MWAMINIFU.

Katika Injili nne, Bwana wetu Yesu alifundisha kweli iyo hiyo.

Yohana 5:24 Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.

Mwamini hatahukumiwa. Amevuka mautini au hukumuni na ameingia uzimani.

Huu ndiyo uzima wa milele; kupita kutoka kifo cha kiroho kuingia uzimani, hii ilifanyika katika ufufuo, katika ukombozi. Ni kazi ya uhakika.

Yohana 10:28 Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.

Yesu anatoa senstensi ya uhakika na ya kibabe hapa "hakuna mtu". Hivyo hakuna kitu, ikiwamo shetani kinaweza kutuchukua mbali kutoka katika wokovu wetu. Hii ni Jumla na kamili kiasi kwamba kila mwamini anapaswa authibitishe ufahamu wake. Mwamini amesalimishwa milele katika Kristo.

Hakuna hatari ya kupotea ama kupoteza wokovu wako. Ni yeye aliyeapa kua hutapokonywa.

Acha ushamba jubali hii, huwezi kupokonyoka hata ungetaka. Yuko na wewe milele.

Mathayo 28:20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.

Yuko pamoja nasi hata mwisho wa dahari sio mwisho wa mwaka.

Jina la mwamini limeandikwa mbinguni.
Luka 10:20 Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.

Sisi ni raia wa ufalme wa Mungu.

Waefeso 2:19 Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu.

Sisi ni washirika kabisa wa familia ya Mungu. Sisi ni raia wa mbinguni. Sio kwamba tunajipendekeza, ndivyo ametufanya.
Wafilipi 3:20 Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;

Neno, "wenyeji" limetafsiriwa kutoka katika neno la kigiriki linalomaanisha uraia.

Hivyo wokovu wetu umepewa usalama wa milele, na hapa ndipo anaposimama mwamini, huu ndiyo uhakika wake. Huu ndiyo uhalisia wa ukombozi wetu. Simama hapo hapo, ndipo ulipo.

1Petro 1:18 Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; 19 bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.

Umekombolewa kwa bei ya thamani, usianze kujiona wa bei rahisi. Usianze kutumikishwa na utoaji wa vitu vya hovyo ili kupata kupatanishwa na Mungu au vipawa na baraka za Mungu.

Ufunuo 5:9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,
Hivyo, ukombozi wa mwamini ni katika damu ya Kristo, ni katika utu wa Yesu.

Na katika huo, tunastarehe!

Tuna amani, hakuna mashaka.

Unajisikiaje?

Fanya nijue.

Pastor Makarios
FB_IMG_1689593090177.jpg
utajiri-wa-mwamini-toleo--selar.co-648b24da9c0e2.jpg


Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 
#WOKOVU vs #MWENENDO

Wokovu ni kazi ya Mungu mwenyewe; matendo mema yanachipuka kutokana na wokovu, na kazi za mwamini au kazi za mkristo sio wokovu.

Wokovu sio malipo kwa kutenda mema; wokovu ni kwa Imani katika Kristo Yesu pekee. Panapotumika neno “ujira/thawabu” katika maandiko ni kwaajili ya kazi/matendo ama mwenendo katika mwili wa Kristo! ujira huu si wokovu bali ni ujira kwa ajili ya huduma, maisha ya Ukristo na mwenendo hudumani, kwa kuleta nafsi kwa Yesu, kwa kukuza waamini (kufanya wafuasi/wanafunzi).

Kwahiyo, Luka 9:24-27, Yesu alikua anamaanisha ujira na si wokovu.

Hebu tusome hapa;

Luka 14:25-35 Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia, [26] Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [27] Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [28] Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? [29] Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, [30] wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza. [31] Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini? [32] Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali. [33] Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. [34] Chumvi ni kitu chema; lakini chumvi ikiwa imeharibika, itiwe nini ikolee? [35] Haiifai nchi wala jaa; watu huitupa nje. Mwenye masikio ya kusikilia, na asikie.

Katika mazingira hayo, mstari wa 26, Yesu anatumia hyperbole kueleza kuwa upendeleo/kipaumbele ni kumweka Kristo katika nafasi ya kwanza.

Huu sio wokovu bali ni wito kwa kuwa wakfu, wakfu kwa ajili ya Mungu na kazi ya huduma.

#Wokovu una matendo yake, lakini MATENDO SI WOKOVU

1. Yesu anawaita wanafunzi wake (Mathayo 4:18-22, Luka 5:1- 11, Yohana 1:35-51)

2. Aliwaita, wakamfuata, sasa akawapa majukumu/kazi (Mathayo 10:1-15, Marko 6:7-11, Luka 9:1-5)

3. Sasa anawaita au anawataka katika kujitoa zaidi (deeper commitment)

#WOKOVU UNAPATIKANA #MARA MOJA TU, KUKUA KIROHO NA KUTAKASWA NI #ENDELEVU (kitu kinachoendelea kila siku).

KUNA WAAMINI WASIOZAA MATUNDA

Wakristo wenye matendo/ mwenendo mbaya

Hebu tazama hapa;

1Wakorintho 3:1 Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. [2] Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, [3] kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? [4] Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?

Mstari wa 1

Neno “rohoni” linamaanisha vitu ambavyo vinahusiana na Roho.

Hakuweza kuzungumza nao kama watu wa rohoni bali kama watu wa mwilini. Hii inamaanisha kuwa watu aliokua anawaandikia walikaua ni watu wa “rohoni” yaani walikua ni wa Roho; walikuwa wamepokea Roho ambayo ni ya Mungu.

1Wakorintho 2:10 Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. [11] Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. [12] Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. [13] Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. [14] Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. [15] Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu. [16] Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.

Walikua wa “rohoni” kwasababu Roho anakaa ndani yao.

1Wakorintho 3:16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

1Wakorintho 6:11 Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

1Wakorintho 6:19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; [20] maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

Watu hawa wameoshwa, wametakaswa, wamehesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu, wao ni hekalu la Mungu, wana Roho Mtakatifu ndani yao. Hivyo ni wa “rohoni” kwa kuzaliwa, lakini hakuweza kuzungumza nao kwa namna ya “rohoni” bali kama watu wa mwilini kama watoto wachanga katika Kristo.

Neno “mwilini” (carnal- KJV) limetafsiriwa kutoka neno la Kigiriki “sarkinos” –ya/wa mwilini. (Of the flesh)

Mwamini sio wa mwilini lakini ni wa Roho. Matumizi ya neno “wa mwilini” kwa mwamini ni kuelezea matendo/mwenendo mbaya. Matumizi ya neno “wa mwilini” ni matumizi ya lugha yanayoonesha hali tofauti na uhalisia (an oxymoron); ni kuonyesha au kuelekezea tabia yao ambayo imekua tofauti na asili yao (ya rohoni).

Yaani wao ni wa rohoni, lakini matendo yao ni ya mwilini, wanaenenda kama watu wa kawaida, kama watu wasio na Roho.

Chunguza mwenendo wao

1Wakorintho 1:10 Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja. [11] Kwa maana, ndugu zangu, nimearifiwa habari zenu na wale walio wa nyumbani mwa Kloe, ya kwamba iko fitina kwenu.

1Wakorintho 3:3 kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?

1Wakorintho 5:1 Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.

1Wakorintho 6:1 Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? [2] Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo?

1. Kulikua na mashindano/mizozo (contentions) hawakua wanazungumza kitu kimoja (hawakuwa na kauli moja), kulikua na kutokuelewana baina yao

2. Kulikua na migongano/ugomvi, wivu, kutengana baina yao

3. Mwamini alimchukua mke wa babaye

4. Walikwenda katika mahakama za wasioamini ili kuamua mambo yanayowahusu waamini

5. Hawakuenenda katika upendo, hawakuwa wanawajali wengine (walio waamini) katika mambo waliyokuwa wanafanya.

Ni wazi kuwa, hawakuwa wanaennenda kama watu wa rohoni, walikua kama watu wa mwilini. Kwa hiyo matendo/mwenendo wao ulikua mbaya licha ya kuwa wameokolewa (wamepata wokovu).

#Katika waraka huo huo Paulo #aliwasifia baadhi ya waamini wenye mwenendo #mzuri;

1Wakorintho 6:15 Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa Stefana kwamba ni malimbuko ya Akaya, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumu watakatifu); [16] watiini watu kama hawa, na kila mtu afanyaye kazi pamoja nao, na kujitaabisha. [17] Nami nafurahi kwa sababu ya kuja kwao Stefana na Fortunato na Akaiko; maana hawa wamenikirimia kwa wingi yale niliyopungukiwa kwenu. [18] Maana wameniburudisha roho yangu, na roho zenu pia; basi wajueni sana watu kama hao.

Anawataja wale waliokuwa katika nyumba ya Stefana na jinsi ambavyo walijitoa kwaajili ya kuwahudumia watakatifu.

Anawataja Fortunato na Akaiko jinsi walivyomkirimia (Paulo) na watakatifu wengine

MWENENDO SIO WOKOVU, LAKINI MATENDO AU MWENENDO UNA UJIRA WAKE na pia ujira wake sio vitu (material).

Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

#Matendo/mwenendo mzuri una shina katika asili yetu; tunaenenda katika mwenendo mwema si ili tuokolewe,tunaenenda na kutembea katika hayo kwasababu tumeumbwa na Mungu kufanya matendo mema.

TUENDELEE KUTENDA MEMA NA KUWA NA MWENENDO MZURI BILA KUSAHAU KUWA MWENENDO SIO WOKOVU!

Pst Felician Makarios

Sent from my Infinix X6816 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom