Kuna wakati mwingine viongozi wa Tanzania wanaonewa

Ramon Sanchez

JF-Expert Member
Oct 9, 2022
767
1,829
Mambo vp jamiiforums

Ninaandika mada hii sio kama ninahitaji something in return kama vile nipewe pesa au ajira serikali. Hapana. Ninaandika fikra zangu tu kama inavyoona inafaa.

Ndugu zangu, hii nchi bado ni masikini saaana ukilinganisha na nchi kama China, USA, Russia pamoja na England. Kuna baadhi ya mambo tunapaswa kuwakosoa viongozi ila kuna mengine ukijaribu kutizama katika jicho la kibinadamu, utagundua tu ya kwamba hili suala lipo nje ya uwezo wao kwa sababu ya umasikini wa nchi. Pesa haitoshi kuigawa katika familia ya Tanzania kila mmoja aridhike.

Kuna wakati tuwakosoe viongozi lakini wakati mwingine tuwe na aibu kidogo kama ambavyo katika familia unakuta wiki nzima watoto wanakula wali mara moja kwa wiki ndivyo inavyotokea katika ngazi hizi za uongozi wa juu (mishahara kuchelewa, malimbikizo ya madeni, renderers kutokulipwa kwa wakati) haya yote ni dalili ya umasikini wa nchi yetu ya Tanzania.

Kwa kiandika hayo juu simaanishi kwamba hakuna uzembe wa baadhi ya watendaji wachini pamoja na waandamizi wa serikali, hapana, uzembe upo, tuendelee kuwasema lakini sisi bado ni masikini sana.

Jenga picha nchi kama Russia. Nchi ya Russia miaka kadhaa nyuma walikuwa wanatumia internet hii ya kawaida kama ambayo Tanzania inatumia lakini wakaamua kujitoa na kuanzisha internet yao.

Unajua kwa sababu gani waliamua kufanya vile? Kwa sababu Russians are rich compared to Tanzania. Laiti kama Tanzania ingekuwa na GDP kubwa kama hizo nchi za Ulaya, basi na sisi tungeweza kuwa na internet yetu pamoja na kurusha satellite huko juu angani, lakini issue ni umasikini wa nchi.

Nepotism, kujuana pamoja na uswahiba upo na ninaomba tuendelee kukosoa lakini tukumbuke sisi ni masikini ndio maana hata baadhi ya shule za msingi hazina vyoo.

Yangu, mimi leo ni hayo tu. Tuendelee kuwakosoa viongozi lakini tukumbuke ya kwamba Tanzania sio Russia na wala sio Marekani, bali sisi ni Taifa la kipato cha chini na siku zote nchi haziwezi Kulingana.
 
Unataka internet ya Tanzania uitumie kufanya nini?
Mbona unaonekana ni member wa JF wa muda mrefu alafu unakurupuka sana?

Mtu akiwa na nia mbaya na internet ya Tanzania, anaweza akadhubutu kuandika mtandaoni??
 
huko nje ya jamii forum, watu wengi wanajua jamii forum ni ya watu wenye akili timamu tu, hawajui tu kuwa huku nako kuna wapumbavu wakubwa kama wewe....wizi wa mabilions kila mwezi bila wahusika kuwajibishwa ndo useme viongozi hao wanaonewa wanapokosolewa juu ya kushindwa kuwahudumia vyema wananchi?....hizi kauli endelea kuandika ukiwa nyuma ya keyboard, ukija kuropoka live utapoteza meno...
 
huko nje ya jamii forum, watu wengi wanajua jamii forum ni ya watu wenye akili timamu tu, hawajui tu kuwa huku nako kuna wapumbavu wakubwa kama wewe....wizi wa mabilions kila mwezi bila wahusika kuwajibishwa ndo useme viongozi hao wanaonewa wanapokosolewa juu ya kushindwa kuwahudumia vyema wananchi?....hizi kauli endelea kuandika ukiwa nyuma ya keyboard, ukija kuropoka live utapoteza meno...
Sawa boss asante kwa comment yako.
 
Mbona unaonekana ni member wa JF wa muda mrefu alafu unakurupuka sana?

Mtu akiwa na nia mbaya na internet ya Tanzania, anaweza akadhubutu kuandika mtandaoni??
Value ya internet unayoifaidi ni huduma zinazopatikana humo na wingi wa watumiaji. Utajiri wa Russia umewapelekea kuwekeza kwenye kutafuta namna ya kucontrol wanachoweza kukiona watu wao mitandaoni. Ndio unachotaka kwetu? Au motivation yako ni nini
 
Value ya internet unayoifaidi ni huduma zinazopatikana humo na wingi wa watumiaji. Utajiri wa Russia umewapelekea kuwekeza kwenye kutafuta namna ya kucontrol wanachoweza kukiona watu wao mitandaoni. Ndio unachotaka kwetu? Au motivation yako ni nini
Mkuu, ninaomba kusema tena "acha kukurupuka". Longtime members wa JF kama wewe wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa new members.

Please man up bro.
 
sijui kwanini umeamua kuitolea mfano china,us na russia!!!
hizi nchi zimeshatoka kwenye mipango ya ujenzi wa zahanati na vyumba vya madarasa,zipo mbali sana kwenye namna ya kukuza uchumi zaidi na kuboresha mazingira zaidi ya raia wake.
sisi ndio kwanza tunawaza madawati na vikokotoo.

kitu cha kwanza ukumbuke lawama,malalamiko,masimango, na nongwa kwa viongozi haipo ktk wao kushindwa kutufikisha ziliko US ama china,bali ni kuchemka kabisa kusimamia serikali zao katika hatua hii changa tuliyopo.
mende inalalamika,fungu la dawa za mahospital linasua sua,kuna panya zimebeba fungu zinajipakulia kwa nafasi bila bugdha.

nchi imekosa mtendaji wa mwisho ina msemaji tu,ambaye nayeye unakuta analalamikia aliowateua,sijui nani awawajibishe!!!!

nchi kuna wizi kila sehemu lakini wakaguzi wa hesabu wanaishia kusoma tu ripoti kisha wanakwenda likizo fupi kupumzika.

kwa mfumo huu,ili kutoboa tutauza mpaka visivyouzika kwa watu ili tuishu,kituo kinachofuata ni reli,watu wanakula hela wanatulia.
 
Mambo vp jamiiforums

Ninaandika mada hii sio kama ninahitaji something in return kama vile nipewe pesa au ajira serikali. Hapana. Ninaandika fikra zangu tu kama inavyoona inafaa.

Ndugu zangu, hii nchi bado ni masikini saaana ukilinganisha na nchi kama China, USA, Russia pamoja na England. Kuna baadhi ya mambo tunapaswa kuwakosoa viongozi ila kuna mengine ukijaribu kutizama katika jicho la kibinadamu, utagundua tu ya kwamba hili suala lipo nje ya uwezo wao kwa sababu ya umasikini wa nchi. Pesa haitoshi kuigawa katika familia ya Tanzania kila mmoja aridhike.

Kuna wakati tuwakosoe viongozi lakini wakati mwingine tuwe na aibu kidogo kama ambavyo katika familia unakuta wiki nzima watoto wanakula wali mara moja kwa wiki ndivyo inavyotokea katika ngazi hizi za uongozi wa juu (mishahara kuchelewa, malimbikizo ya madeni, renderers kutokulipwa kwa wakati) haya yote ni dalili ya umasikini wa nchi yetu ya Tanzania.

Kwa kiandika hayo juu simaanishi kwamba hakuna uzembe wa baadhi ya watendaji wachini pamoja na waandamizi wa serikali, hapana, uzembe upo, tuendelee kuwasema lakini sisi bado ni masikini sana.

Jenga picha nchi kama Russia. Nchi ya Russia miaka kadhaa nyuma walikuwa wanatumia internet hii ya kawaida kama ambayo Tanzania inatumia lakini wakaamua kujitoa na kuanzisha internet yao.

Unajua kwa sababu gani waliamua kufanya vile? Kwa sababu Russians are rich compared to Tanzania. Laiti kama Tanzania ingekuwa na GDP kubwa kama hizo nchi za Ulaya, basi na sisi tungeweza kuwa na internet yetu pamoja na kurusha satellite huko juu angani, lakini issue ni umasikini wa nchi.

Nepotism, kujuana pamoja na uswahiba upo na ninaomba tuendelee kukosoa lakini tukumbuke sisi ni masikini ndio maana hata baadhi ya shule za msingi hazina vyoo.

Yangu, mimi leo ni hayo tu. Tuendelee kuwakosoa viongozi lakini tukumbuke ya kwamba Tanzania sio Russia na wala sio Marekani, bali sisi ni Taifa la kipato cha chini na siku zote nchi haziwezi Kulingana.
Labla uliosema ni kweli LAKINI kikokotoo kinausianaje na umaskini wa nchi??

Kwa Nini wabunge wanaolipwa 12M bado wanalipwa pension yao yote baada ya miaka 5 halafu mtumishi unaemlipa 350K bado unamuwekea kikokotoo!!!! Hapa unazungumziaje??

VIONGOZI WETU NI WABINAFSI SANA.
 
Back
Top Bottom