Kwa kebehi za hawa watu hata kama ningekuwa mimi ndo raisi ningeongoza milele ili kuwakomoa tu...tindo nitaendelea kutofautiana na wewe, siyo kwa hoja, ila kwa mtazamo wako chanya na uliojaa chuki dhidi ya Rais Magufuli, Serikali na Chama Tawala.
Hakuna hata mara moja umejadili kwa hoja zaidi ya kebehi na kejeli. Niamini ndiyo kiwango chako cha kushiriki majadiliano?
Isitoshe sijapata kusoma mada yako yoyote yenye kuleta mjadala kuhusu upande wa wanasiasa unaowawikilisha humu JF, ili tikashirikishana kupanua uelewa wa uwezo wa upande huo kuongoza nchi.
Nikirejea kwenye majibu yako:
Wasema kwamba:
1) Ni kama anavyojifanya anakienzi kiswahili, ukweli ni kuwa lugha ya kiingereza inampiga chenga, najiuliza kujua kiingereza ni msingi wa nini?
2) Sio kwamba hataki demokrasia, ukweli ni kuwa haiwezi[/[], je, demokrasia kwako maana yake ni nini na inatekekezwaje?
Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo ben saa nane ndio mungu wenu? Mnatujazia server hapa,, ben saa nane ben saa kumiSawa mwambie ben saanane yuko wapi na PhD yake feki bado anaitumia?
Sent using Jamii Forums mobile app
Nashukuru umerudi, nilijua kwa kile nilichokuambia jana ungerudi, na huu utetezi wako umejikita kwenye kile nilichokuambia jana. Kwangu mtu yoyote asiyeheshimu mifumo ya demokrasia hata afanye zuri gani hawezi kupata sifa toka kwangu. Hata akifanya jambo jema huwezi kuniona namsifia sana sana nitakaa kimya. Ninajua uko biased hivyo sitegemei uone mchango wangu wowote wa maana, hilo sio kosa langu ni juu ya udhaifu wako.
1. Kiingereza ni moja kati ya lugha zetu 2 kuu za Taifa. Yeye ameonyesha hataki kutumia kiingereza bali anakienzi kiswahili. Je kuchomeka maneno ya kiingereza kwenye hotuba zake kuna mantiki gani kama lengo ni kukienzi kiswahili?
2. Demokrasia yetu iko mpaka ndani ya katiba na vyama vya siasa vipo kisheria, inakuwaje azuie kazi halali za vyama vya siasa nchi nzima huku chama chake kikifanya kwa uwazi na kificho?
Suala la uchaguzi, ni dhahiri chaguzi zetu hasa toka awamu yake hii, box la kura haliheshimiwi na yote haya ni kutokana na mitazamo yake dhidi ya demokrasia.
Naamini uliyoyaandika hayawakilishi imani yako ila yanasukumwa na mtazamo wa upande wa pili.
Nikushangae tu wewe unayetukuza lugha ya Kiingereza wakati kuna jitihada za kukuza na kukieneza Kiswahili, lugha ya Taifa. Kwa hilo ni dhahiri una wajibu wa kujitambua, kujiamini na kuchukua hatua stahiki.
Kuhusu demokrasia, amini una tafsiri potofu na ni kwa sababu ya mtazamo wako hasi kuhusu Rais na Serikali.
Demokrasia haipimwi kwa kiwango gani wanasiasa wanapanda majukwaani.
Demokrasia ni utawala wa wengi kupitia wawakilishi waliochaguliwa kwa utaratibu uliokubalika. Kwa nchi yetu uwakilishi unaanzia mtaa/kitongoji hadi Taifa. Na wawakilishi wanawajibika, siyo kupanda majukwaani bali kushiriki vikao vilivyoainishwa kwenye Katiba ya JMT, kusikiliza, kupokea na kuwakilisha yatokanayo kwenye vikao vya juu vya maamuzi.
Uchaguzi hauwezi kuhesabika kutokuwa huru pale tu mshindani anapokosa kuchaguliwa na hatimaye kuilaumu Tume ya Uchaguzi. Na isitoshe mazingira ya kuandaa, kusimamia upigaji kura, kuhesabu na hatimaye matokeo kutangazwa yote huwa huru. Palipo na dosari katika mchakato mzima wa uchaguzi, mahakama ziko wazi kusikiliza malalamiko au madai ya aina hiyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekutekenya kidogo tu lakini ulivyo ' Nyali ' angalia jinsi unavyotokwa na ' Mapovu ' namna hii. Pole sana hadi nakuonea huruma.
[/QUOTE
Kama wewe nilivyokujambisha ukaanza misifa ya kuduwanzi mara sijui mwanaume wa mara, sijui uduwanzi gani.
K
So what is the point here?Kwa yoyote mwenye kufuatilia mienendo ya kisiasa na kiserikali atakubaliana na mimi kwamba Magufuli siyo mpenzi kihivyo wa demokrasia. Hili siyo tusi wala lawama, ni mtazamo wangu kuhusu mtazamo wake! Na hata yeye mwenyewe anasemaga mara kwa mara kwamba demokrasia inatuchelewesha!
Siku baada ya siku ameonekana kuegemea upande wa taasisi ya jeshi hadi kufikia kusuggest timu ya taifa itoke Jeshini. Hizi siyo kauli ya kubeza, anaamini kabisa kuwa ndiyo suluhisho la matatizo yetu yote. Huu ni mtazamo wake ambao unajadilika (kama tutaruhusiwa kujadili!)
Katika tafakari yangu namuona pia kama ni mtu ambaye hata madaraka aliyonayo angependa ayapate kwa njia nyingine ukizingatia kama nilivyotangulia kusema, siyo mfuasi mkubwa sana wa mfumo wa demokrasia.
Nakumbuka 2015 siku ya mwisho ya kampeni kule Mwanza, Kikwete alionekana kama anampandisha mori achangamke (tafuta clip wakati Kikwete anampa nafasi ya kuongea). Toka hapo amekuwa na miaka 5 ya kujizatiti kufikia ndoto yake ya kupata madaraka na kuongoza kwa mfumo alio comfortable nao zaidi.
Huwa siyo rahisi kumshinda Raisi aliye madarakani katika uchaguzi (incumbent President) hata awe ameboronga kivipi. Ni kazi ngumu sana hata kwenye nchi zenye demokrasia iliyokomaa. Nikitumia maneno ya kiingereza ambayo sidhani kama naweza kupata tafsiri sahihi naweza kusema 'the election is his to lose'.
Sitashangaa mwakani akiwatuma wengine wakafanye kampeni huku tukaambiwa yeye ana majukumu muhimu zaidi.
Baada ya hapo chacha!
Sio kwamba hataki demokrasia, ukweli ni kuwa haiwezi. Ni kama anavyojifanya anakienzi kiswahili, ukweli ni kuwa lugha ya kiingereza inampiga chenga kuiongea kwa ufasaha. Hata sasa analitumia jeshi kwakuwa jeshi pia linadhani lina wajibu wa kuhakikisha rais aliyeko madarakani ana haki ya kushinda uchaguzi yeye na chama chake. Hiyo 2020 analitegemea jeshi na vikundi vya kihalifu kuhakikisha anatangazwa mshindi kwani hana uwezo wa kushinda kwa ushawishi.
Unafikiri atakuwepo ?
Amefanya kampeni tangu alipoingia madarakani kila siku yuko live kwenye tv hata kwa matukio ya kawaida. Pia.ikumbukww nec ni mali yake binafsiKwa yoyote mwenye kufuatilia mienendo ya kisiasa na kiserikali atakubaliana na mimi kwamba Magufuli siyo mpenzi kihivyo wa demokrasia. Hili siyo tusi wala lawama, ni mtazamo wangu kuhusu mtazamo wake! Na hata yeye mwenyewe anasemaga mara kwa mara kwamba demokrasia inatuchelewesha!
Siku baada ya siku ameonekana kuegemea upande wa taasisi ya jeshi hadi kufikia kusuggest timu ya taifa itoke Jeshini. Hizi siyo kauli ya kubeza, anaamini kabisa kuwa ndiyo suluhisho la matatizo yetu yote. Huu ni mtazamo wake ambao unajadilika (kama tutaruhusiwa kujadili!)
Katika tafakari yangu namuona pia kama ni mtu ambaye hata madaraka aliyonayo angependa ayapate kwa njia nyingine ukizingatia kama nilivyotangulia kusema, siyo mfuasi mkubwa sana wa mfumo wa demokrasia.
Nakumbuka 2015 siku ya mwisho ya kampeni kule Mwanza, Kikwete alionekana kama anampandisha mori achangamke (tafuta clip wakati Kikwete anampa nafasi ya kuongea). Toka hapo amekuwa na miaka 5 ya kujizatiti kufikia ndoto yake ya kupata madaraka na kuongoza kwa mfumo alio comfortable nao zaidi.
Huwa siyo rahisi kumshinda Raisi aliye madarakani katika uchaguzi (incumbent President) hata awe ameboronga kivipi. Ni kazi ngumu sana hata kwenye nchi zenye demokrasia iliyokomaa. Nikitumia maneno ya kiingereza ambayo sidhani kama naweza kupata tafsiri sahihi naweza kusema 'the election is his to lose'.
Sitashangaa mwakani akiwatuma wengine wakafanye kampeni huku tukaambiwa yeye ana majukumu muhimu zaidi.
Baada ya hapo chacha!