DOKEZO Kuna usafirishaji wa Mabinti wadogo kwenye Mabasi kuja Dar es salaam ili watumikishwe kwa kazi za ndani. Serikali ilitazame hili

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

lufungulo k

JF-Expert Member
Apr 19, 2012
2,550
1,987
Jana nimesafiri toka Gairo kuja Dar, kwa usafiri wa bus (jina kapuni) katika usafiri ule niligundua usafirishaji wa mabinti wa rika mbalimbali kuja mjini kwa ajili ya kazi za uyaya.

Wengine ilitilisha hadi huruma maana ni wadogo mno, mpaka kuzusha mijadala ndani ya bus hilo. Alijitokeza mama mmoja yeye alimuomba namba mmoja wa binti mdogo ambaye alikuwa akipelekwa kuanza ajira mpya na kuahidi kumpigia huyo mama aliyekuwa ajenti wa hivyo vibinti.

Wale wafanyakazi wa bus nao wanamchango wao mkubwa katika hili, wao hukabidhiwa na madalali walioko chimbo ambao huwafikisha mabinti hao na kuwakabidhi kwa makondakta na kuwapa namba za simu za wale watakao wapokea.

Ni zoezi linalofanywa kwa ustadi mkubwa, kila anapokaribia kushusha mtu, simu zinapigwa mapema na kumkuta anayepokea tayari kituoni.

Mwisho pale Mbezi Magufuli Terminal ndo utasikia tangazo la kondakta. Binti anayetegemea kupokelewa asishuke kwenye bus.

Ushauri: Mabinti hawa wasipandishwe kwenye mabus, bila kuwa na barua za watendaji zenye kuonesha jina, umri , wake, wazazi wake, namba za simu, nida na zikieleza anakwenda wapi? Kufanya nn? Ili kuokoa wale mabinti wadogo kiumri kuzolewa na janga hili.

Tunapiga vita, ushoga, wizi, ubakaji, ufisadi na maovu mengi yafananayo na hayo na kuacha janga hili ni unafiki. Na wanafiki mshahara wao ni motoni.
 
Wengine wanaondoka kwa baraka za wazazi ili kuokoa hali mbaya za familia zao.

Unakuta kabinti kamemaliza darasa la saba bado kadogo na kamefeli. kazi ngumu za pale nyumbani hakawezi. wazazi wanatoa baraka kaende mjini kakafanye kazi za uyaya ambao wao wanadhani ni rahisi kuliko kilimo.

Nilishakutana na hili kama sio nadhani ni maeneo ya Shinyanga, kabinti kalikuwa kanaenda Mwanza.
 
Mleta mada wewe unatakaje?
Unajua maisha anayoishi huko kijijini?
Maisha huko ni magumu na hakuna future nzuri.
Labda tuwaombe hao wanao waajiri wawe wanawaendeleza hawa watoto kielimu kwa kuwa umri unawaruhusu. Ila kwa ugumu wa maisha wanayoishi huko kijiji waacheni tu waje kujaribu maisha mijini.
 
Ingizo jipya mjini.. Baada ya miaka miwili mitatu
Baadhi watakuwa marehemu
Baadhi watakuwa wamepitia ubakwaji
Baadhi watakuwa wamerudi nyumbani na watoto
Baadhi watakuwa wameolewa
Baadhi watakuwa wameambukizwa magonjwa
Baadhi watakuwa ma bar maid
Baadhi watakuwa wadangaji
Baadhi watakuwa kwenye madawa ya kulevya
Baadhi watakuwa na mafanikio
Baadhi bado watakuwa wanafanya kazi za ndani nknk
 
Ustawi wa jamii wamekaa tu ofisini wanasubiria umbeya wanaume kwenda kushtakiwa kwenye dawati.wanapotoka wanajua,wanapotumikishwa mjini wanawaona.vitoto miaka 12 kweli vinatumikishwa,wewe umeona,wao hawalioni hili?Na umepamba tu habari kuwa ni kazi za ndani,ila wengi ni kwenye bar na madanguro.
 
Ustawi wa jamii wamekaa tu ofisini wanasubiria umbeya wanaume kwenda kushtakiwa kwenye dawati.wanapotoka wanajua,wanapotumikishwa mjini wanawaona.vitoto miaka 12 kweli vinatumikishwa,wewe umeona,wao hawalioni hili?Na umepamba tu habari kuwa ni kazi za ndani,ila wengi ni kwenye bar na madanguro.
Kweli ustawi wa jamii ndio very concerned kwa hili nadhani wao ndio walitakiwa kuwajibika kushulikia suala hili maana limekithiri sasa
 
Kuna sheria nyingi zinahitaji maboresho mimi Huwa nahitaji nyumbani Kwa gu Binti wa kazi awe 18yrs and above lakini Kuna mtu nilimtuma akaniletea katoto ka miaka 17,lakini Sasa amefikisha umri wa miaka 20,kanapiga job vizuri,mabinti wengi unasikia wameawa au kunyanyasa watoto ni wenye umri mdogo ambao ni miaka 12-17,ukikaa na sampuli za hivyo vitoto tegemea watakuulia mtoto siku moja
 
Jana nimesafiri toka Gairo kuja Dar, kwa usafiri wa bus (jina kapuni) katika usafiri ule niligundua usafirishaji wa mabinti wa rika mbalimbali kuja mjini kwa ajili ya kazi za uyaya.

Wengine ilitilisha hadi huruma maana ni wadogo mno, mpaka kuzusha mijadala ndani ya bus hilo. Alijitokeza mama mmoja yeye alimuomba namba mmoja wa binti mdogo ambaye alikuwa akipelekwa kuanza ajira mpya na kuahidi kumpigia huyo mama aliyekuwa ajenti wa hivyo vibinti.
Kwani hii imeanza leo na jana, mbona iko miaka mingi tu?

Hivi wafanyakazi wa nyumbani walioko mijini miaka nenda rudi si wanatokea vijijini? Madamu hakuna ajira kwa vijana hii itaendelea tu.
 
Sijui kama kuna uhaba wa madawati na vyumba vya madarasa huko Kigoma maana watoto wenye umri wa kuwa shule wanasafirishwa kwa fujo kwenda kuchunga mikoa ya jirani hasa Shinyanga na Tabora.
 
Jana nimesafiri toka Gairo kuja Dar, kwa usafiri wa bus (jina kapuni) katika usafiri ule niligundua usafirishaji wa mabinti wa rika mbalimbali kuja mjini kwa ajili ya kazi za uyaya.

Wengine ilitilisha hadi huruma maana ni wadogo mno, mpaka kuzusha mijadala ndani ya bus hilo. Alijitokeza mama mmoja yeye alimuomba namba mmoja wa binti mdogo ambaye alikuwa akipelekwa kuanza ajira mpya na kuahidi kumpigia huyo mama aliyekuwa ajenti wa hivyo vibinti.

Wale wafanyakazi wa bus nao wanamchango wao mkubwa katika hili, wao hukabidhiwa na madalali walioko chimbo ambao huwafikisha mabinti hao na kuwakabidhi kwa makondakta na kuwapa namba za simu za wale watakao wapokea.

Ni zoezi linalofanywa kwa ustadi mkubwa, kila anapokaribia kushusha mtu, simu zinapigwa mapema na kumkuta anayepokea tayari kituoni.

Mwisho pale Mbezi Magufuli Terminal ndo utasikia tangazo la kondakta. Binti anayetegemea kupokelewa asishuke kwenye bus.

Ushauri: Mabinti hawa wasipandishwe kwenye mabus, bila kuwa na barua za watendaji zenye kuonesha jina, umri , wake, wazazi wake, namba za simu, nida na zikieleza anakwenda wapi? Kufanya nn? Ili kuokoa wale mabinti wadogo kiumri kuzolewa na janga hili.

Tunapiga vita, ushoga, wizi, ubakaji, ufisadi na maovu mengi yafananayo na hayo na kuacha janga hili ni unafiki. Na wanafiki mshahara wao ni motoni.

CCM watakwambia hii nayo ni ajira kama wanayo rumbana nayo na yule nabii
 
Wengine wanaondoka kwa baraka za wazazi ili kuokoa hali mbaya za familia zao.

Unakuta kabinti kamemaliza darasa la saba bado kadogo na kamefeli. kazi ngumu za pale nyumbani hakawezi. wazazi wanatoa baraka kaende mjini kakafanye kazi za uyaya ambao wao wanadhani ni rahisi kuliko kilimo.

Nilishakutana na hili kama sio nadhani ni maeneo ya Shinyanga, kabinti kalikuwa kanaenda Mwanza.
Sio wengine, ni wote wanatoka huko kwa ridhaa ya wazazi kutokana na hali ngumu. Sasa kama kuna mikataba inasainiwa au ni maongezi ya simu tu, hapo haijulikani.
 
Ili kuwasaidia wape mtaji wape pesa
Wanashida ndio mana wanapambana kuwatetea wasiajiliwe ni ukatili mkubwa na wivu kupindukia
Ewe mtoa mada
 
Back
Top Bottom