Mzee wa Twitter
JF-Expert Member
- Nov 5, 2023
- 1,283
- 2,043
Hii nchi ina viongozi wa ajabu sana. CAG yupo kwa mujibu wa Katiba kuwepo na kuondolewa kwake lazima kufuate Katiba japo kuna kiongozi tuliwahi kumpata kwa bahati mbaya kiongozi huyo alikuwa hatekelezi baadhi ya majukumu kwa mujibu wa Katiba na mwisho akatuondolea CAG bila kufuata utaratibu uliowekwa na Katiba.
Ripoti yake CAG ya mwaka uliopita ilipelekwa Bungeni lakini pamoja na Ubadhilifu wote uliotwaja kwenye ile ripoti hakuna aliyechukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufikishwa Mahakamani.
Juzi CAG katoa tena ripoti nayo imesheheni ubadhilifu wa Mali za Umma wahusika wametajwa ngoja tusubiri Bunge au Serikali kama itawashughulikia.
USHAURI
Kama Bunge na Serikali zinaona ripoti za CAG hazitekelezeki basi Cheo cha CAG na Ofisi yake VISIWEPO kuliko kuendelea kumtumia CAG huku ripoti yake hazifanyiwi kazi.
Cheo cha CAG kifutwe!
Ripoti yake CAG ya mwaka uliopita ilipelekwa Bungeni lakini pamoja na Ubadhilifu wote uliotwaja kwenye ile ripoti hakuna aliyechukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kufikishwa Mahakamani.
Juzi CAG katoa tena ripoti nayo imesheheni ubadhilifu wa Mali za Umma wahusika wametajwa ngoja tusubiri Bunge au Serikali kama itawashughulikia.
USHAURI
Kama Bunge na Serikali zinaona ripoti za CAG hazitekelezeki basi Cheo cha CAG na Ofisi yake VISIWEPO kuliko kuendelea kumtumia CAG huku ripoti yake hazifanyiwi kazi.
Cheo cha CAG kifutwe!