Kuna ulazima gani wa kusema hivi!?

Kuna ulazima gani wa kusema hivi!?

funduku

Senior Member
Joined
May 2, 2013
Posts
131
Reaction score
36
Matumaini yangu mpo wazima, Ishu ni kwamba mimi binafsi nafikili kuna baadhi ya vitu au maneno si yalazima kuyataja ktk sentensi au kauli. kwa mfano uta sikia mtu anasema "Ngoja kwanza nikaoge maji". na wakati neno 'maji' halikua la lazima kulitaja kama ungesema "ngoja kwanza nikaoge" ungeeleweka bila ya kutaja neno maji, maneno mengine utasikia eti mtu anasema, naenda kunya mavi au naenda kukojoa mkojo, na wakati angesema kua naenda kunya au kukojoa tayari ingefahamika bila ya kutaja mavi au mkojo. Asenteni sana naomba kuwasilisha. maneno mengine yanayofanana na hayo ongezea wewe hapo chini ambayo watu hupenda kuyatamka.
 
1. Ninaimba wimbo
2. Ninatembea kwa miguu
3. Ninaomba maombi mvua inyeshe.
 
Hawafanyi kosa wanaosema hivyo ila wanafanya ujalizaji usio na sababu kwakuwa maana inakuwa imeshaeleweka.
 
Mleta mada uko sahihi. Naongezea mifano hii ya harakaharaka:
Amejifungua mtoto
Ameuwawa na kufa.
Ameoa mke
 
Mkuu siku hizi watu wanaoga vitu vingi sana si maji tu :smile-big:
 
Mmmh Mara nyingine utumie tafsida ndugu hasahasa hilo neno kuny* mav*
 
Back
Top Bottom