Mkuu Alfu Ulela,
Nijuavyo mimi ni haya; (Ila bahati nzuri tuna viongozi na members toka Chadema ambao watajibu vema zaidi).
Chadema wamekuwa na mikakati na harakati yenye kukumbatia na kuhakikisha inawafungua macho jamii na kuwafungua akili ili kuwaamsha wananchi katika masuala ambayo yanawagusa, na ni kwa namna ipi Utawala na viongozi katika utawala wana shiriki moja kwa moja katika kuathiri maisha ya jamii katika kila Nyanja ya maisha. Kuwezesha mikakati na harakati hizo kumekuwa na oparesheni zenye mlengo huwa wa kuifikia jamii ya Tanzania kila mahala nchini.
Oparesheni kwa sasa ambayo inafanya kazi ndani ya Chadema ni maarufu kwa jina la Movement for Change (M4C). Uongozi wa Chadema wamewekeana utaaratibu wa kazi ambao umegawa majukumu dhidi ya viongozi kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa na kupita Tanzania nzima.
Nje ya oparesheni hiyo ya M4C kuna oparesheni nyingine mfanano iliyo wahi pia anzishwa kwa malengo ambayo yapo karibu sawa kabisa. Hio opareshini iliyowahi fanywa ni moja maarufu kwa jina la operation Sangara.
Katika makala hii nimeweka Mh. Zitto Kabwe anaeleza na kufafanua kwa kirefu ni kwa nini oparesheni Sangara ilibuniwa.
Kwa maelezo zaidi, soma hii makala juu ya 'Operation Sangara' pengine itakusaidia.
CC.
Zitto,
Dr. Slaa,
Mikael P Aweda,
Mwita Maranya,
Molemo,
Ben Saanane