Kuna shida kwenye Jeshi letu

Kuna shida kwenye Jeshi letu

Pamoja na yanayoendelea nchi, nikili kuwa kwenye jeshi letu kuna shida kubwa sana.
Nimekuwa nikijiuliza sana, je tuna jeshi kweli, tuna polisi wenye weledi, au ni vibwengo tu? Unaambiwa kuua na unatii tu.

Kwa mtazamo wa kimataifa, amri inayokwenda kinyume na sheria haipaswi kutekelezwa. Kwa hiyo, si kosa kukataa amri ya mkuu kama amri hiyo ni haramu au inavunja misingi ya utu. Askari au polisi wana wajibu wa kufikiri, kuchuja, na kulinda raia, si kutekeleza kila kitu.

Swali kubwa linabaki: tatizo linaanzia wapi? Je, ni kwenye mchakato wa uajiri (recruitment) ambapo watu wasio na uwezo wa kufikiri kwa kina wanachukuliwa (Machawa) na kuingizwa kwee jeshi letu? Au ni mfumo wa mafunzo na uongozi unaowafinyanga watu kuwa watendaji bila akili zao?

Kwa hali ilivyo, inaonekana kabisa kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vimejaa vilaza, watu wasiokuwa na maadili ya kazi wala uwezo wa kubeba majukumu makubwa ya kulinda raia. Ndiyo maana swali hili linaumiza kichwa: je, ni kosa kukataa amri ya mkuu inayokwenda kinyume na sheria? .
Tukubali kwamba, nchi inahitaji reformation kubwa sana, karibu katia kila taasisi.

Kuendelea kuwepo kwa Samia madarakani,ndio ucheleweshaji wa mabadiriko hayo, na nchi yetu itaendelea kuteseka sana. Miezi michache inayokuja, Tanzania itakuwa hali ngumu sana. Kumbuka haya maneno.

Watanzania, hii hali sio shwari, achana na wanaojitoa akili zao, huku wakitumia mgongo wa dini, kwamba watu wanamkataa Samia kisa dini yake, ni sababu za kipuuzi, na ni wapumbavu.

Watanzania wote ni ndugu, haijalishi wewe ni Mkristo au muislam, au kabila lolote, tuwapuuze hawa mapumbavu wanaotaka kuwatenga watanzania.

Hii ndiyo aina ya Polisi wa Tanzania.
 
Kwenye hili wewe sema tu, ila mama haondoki kwasababu mtu hataki awepo. Samia yupo, nawe kafanye kazi ya kukupatia maisha, vinginevyo utajikuta una njaa na umaskini wa kutisha.

Haya maandishi yanaonesha wewe ndo kilaza usiyejua nini vyombo vya ulinzi vinafanya. Ulitarajia wakuache uibe, uharibu mali za umma na za watu binafsi na uwaue wao wana wa ulinzi halafu wakuchekee? Waswahili huwa tunasena "ukicha mwana kulia, mwisho utalia wewe. Mkuu lia na uume meno baadae ukajifunze.
Kwa kifupi tu, wewe ni moja ya uzao wa laani tulionao Tanzania. Nitakujibu vizuri nikipata time. Jaribu kuficha upumbavu wako. Kimya pia ni Hekima.
 
Majeshi msikate tamaa kwa nyuzi kama hizi zilizozo za ovyo! Kama raia waliamua kufanya uasi dhidi ya wenzao , dhidi ya mali za uma nk. Hawa watu walitarajia ninyi muwachekee ili watimize lengo la kuchoma SGR,bunge nk?
Katika nchi hii hamtaachwa mfanikiwe. Nguvu ni Ile ile mzidi kujichanganya.
 
Kwa kifupi tu, wewe ni moja ya uzao wa laani tulionao Tanzania. Nitakujibu vizuri nikipata time. Jaribu kuficha upumbavu wako. Kimya pia ni Hekima.
Huenda uzai wa laana unatoka kwenye ukoo wako hapa Tanzania, ikitokea kwamba nawe ni Mtanzania. Ni kweli kimya ni hekima. Ungeanza wewe kukaa kimya haya yasingekuwepo.

Mimi nangojea kwa hamu majibu yako 'mazuri'. Kama unadhani unaweza kusema halafu watu wakanyamaza, sema.
 
Kwa sasa EA kuna jeshi moja tu imara na lenye weledi, nalo ni RDF. Waliobaki huwezi walinganisha hata na M23 ambayo ina oganaizesheni nzuri, mafunzo ya hali ya juu pamoja na zana za kisasa.
Unadhani RDF wanaweza kwenda kinyume na Maagizo ya Mr. Slim hata kama ni haramu?
 
Kwenye hili wewe sema tu, ila mama haondoki kwasababu mtu hataki awepo. Samia yupo, nawe kafanye kazi ya kukupatia maisha, vinginevyo utajikuta una njaa na umaskini wa kutisha.

Haya maandishi yanaonesha wewe ndo kilaza usiyejua nini vyombo vya ulinzi vinafanya. Ulitarajia wakuache uibe, uharibu mali za umma na za watu binafsi na uwaue wao wana wa ulinzi halafu wakuchekee? Waswahili huwa tunasena "ukicha mwana kulia, mwisho utalia wewe. Mkuu lia na uume meno baadae ukajifunze.

Hongereni kwa hii👆🏾 kazi askari wa Samia.
 
Nivitie shime Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama, mliposhikilia kazeni hapo hapo, watu wameshaanza kutoa milio huku baada ya kuvuruga mipango yao. Uzuri kwenye hizo Taasisi hamjaingia kwa kupigiwa kura, ajenda yenu ni moja tu kuhakikisha Ulinzi na Usalama wa Tanzania utakaotupeleka katika nchi yenye amani na umoja. Nawasilisha.
Wanafanya ULINZI na USALAMA wa kitu gani???

Hizo ni MILITIA za wahuni tu
 
Majeshi msikate tamaa kwa nyuzi kama hizi zilizozo za ovyo! Kama raia waliamua kufanya uasi dhidi ya wenzao , dhidi ya mali za uma nk. Hawa watu walitarajia ninyi muwachekee ili watimize lengo la kuchoma SGR,bunge nk?
Katika nchi hii hamtaachwa mfanikiwe. Nguvu ni Ile ile mzidi kujichanganya.

Naona mmemuadhibu kijana kwa kutaka kuchoma SGR na Bunge, kwenye hili mlikuwa makini haswa.
 
Ukishakosa siasa safi kwenye Taifa, Hakuna Sector itabaki Salama, Sio dini, kikimo, Elimu, Jeshi wala Familia.

Woote hao wanarishwa Sera na Sheria zinazotokana na quality ya siasa kwenye jamii
 
We nani kakwambia polisi anaeshambuliwa na mawe huwa anasubiri kuambiwa amri ya kuua? Ukimshambulia kwa mawe hana haja ya kusubiri kupewa amri na yoyote atajipa amri mwenyewe, na ukifanya uhalifu akaja kukudhibiti ukatumia nguvu dhidi yake hivyo hivyo atajipa amri ya kutumia nguvu ikiwezekana kukuua.

Kwahiyo hamna mtu anaewapa amri nenda kavunje duka la mtu na kuharibu mali ya mtu wakukute alafu utajua kuna mtu anawapa amri au wanajiamrisha wenyewe.
 
We nani kakwambia polisi anaeshambuliwa na mawe huwa anasubiri kuambiwa amri ya kuua? Ukimshambulia kwa mawe hana haja ya kusubiri kupewa amri na yoyote atajipa amri mwenyewe, na ukifanya uhalifu akaja kukudhibiti ukatumia nguvu dhidi yake hivyo hivyo atajipa amri ya kutumia nguvu ikiwezekana kukuua.

Kwahiyo hamna mtu anaewapa amri nenda kavunje duka la mtu na kuharibu mali ya mtu wakukute alafu utajua kuna mtu anawapa amri au wanajiamrisha wenyewe.
Unaweza soma tena ulichoandika na kujisikiliza mwenyewe?
 
Back
Top Bottom