Kuna msichana ananipenda

Kuna msichana ananipenda

davon

Member
Joined
Dec 8, 2012
Posts
14
Reaction score
2
Kuna msichana anainipenda kweli na kila siku haachi kuniambia kuwa ananipenda na anataka nimuoe ila ukweli ni kwamba simpendi kama anavyo nipenda yeye na sina mpango wa kumuoa na nimekuwa kwenye mahusiano nae kwa takribani mwaka nimejaribu kuwa na furaha nikiwa nae ila sina furaha... Naogopa kumuacha kwani naona nitakuwa nime muumiza sana
 
Na wewe unakaa nae wa nini sasa kama humpendi
Bora kuwa wazi umwambie kabisa kuwa aangalie ustaarabu mwingine kuliko kumpotezea muda wake
 
Foolish! unataka uchakachue hadi ukishatosheka ndo umuache, kama siyo hivyo mwambie mapemaaaa.
 
suala labda ni pengine hujawa tayari kuoa kwa sasa. Kama uko tayari basi inawezekana unaye ambaye unadhani unampenda. Tatizo linakuja kwamba huyo utakayedhani unampenda, yeye hakupendi kihivyo..., haya mambo ndivyo yalivyo!!

Ushauri wa bure ni kama uko tayari kuoa, na kama huyu usiyempenda hana kasoro zozote zilizo bayana na ambazo unadhani hutaweza kuzimudu, OA along the way utampenda tu! Ukija kuchunguza ndoa (union) nyingi ziko composed na watu wa namna hii unayoizungumzia. Kunakuwa na mmoja anampenda sana mwenzie lakini mwingine si saaana kihivyo....
 
Foolish! unataka uchakachue hadi ukishatosheka ndo umuache, kama siyo hivyo mwambie mapemaaaa.
Hivi binadamu kama binadamu unachakachua nn na ni nn unatosheka kwa kuchakachua huko! Kumbuka anayeweza kuchakaza binadamu ni shetani anapopata nafasi tu. Hapa issue ni mahusiano yenye lengo la kuoana lkn mmoja anaona hawezi kufanya hivyo so ni kumuongoza afanye nn basi!!
 
Bora kumuacha mapema kuliko kuendelea naye maana mwisho utakua mbaya kuliko mwanzo...ila inabidi hekima itumike vinginevyo hawachelewagi kujinaniliu...kisa mapenzi....
 
Huu mwaka huu....watu ni kupendana tuu.....haya bwana ukishatosheka kufanya yako muombe na 0713 ili utosheke kabisa..nyambaaf
 
hebu acha ujinga,km ulikuwa humpendi kihivyo uliwezaje kukaa nae mwaka mzima....yaan wanaume wa siku hz kwakweli sijui mmelogwa nashindwa ht kuwaelewa.
 
Dah...Haya ni maandalizi ya Valentine....Wa ukweli watajulikana na wanaopotezeana muda watadhihirika tu...sinema inaendelea!
 
Aaaaaaaaaaah! Wapi! Ukute na yeye anakulia timing tu! Mujini humu siku hizi wote manunda tu! Dont feel so gulity!

You can never miss the water untill the wells are dry!!!!!!!!!!
 
Kuna msichana anainipenda kweli na kila siku haachi kuniambia kuwa ananipenda na anataka nimuoe ila ukweli ni kwamba simpendi kama anavyo nipenda yeye na sina mpango wa kumuoa na nimekuwa kwenye mahusiano nae kwa takribani mwaka nimejaribu kuwa na furaha nikiwa nae ila sina furaha... Naogopa kumuacha kwani naona nitakuwa nime muumiza sana

Acha kumpotezea muda mrembo wa watu bora umwambie ukweli.
 
Kuna msichana anainipenda kweli na kila siku haachi kuniambia kuwa ananipenda na anataka nimuoe ila ukweli ni kwamba simpendi kama anavyo nipenda yeye na sina mpango wa kumuoa na nimekuwa kwenye mahusiano nae kwa takribani mwaka nimejaribu kuwa na furaha nikiwa nae ila sina furaha... Naogopa kumuacha kwani naona nitakuwa nime muumiza sana

ukishamuacha umlipe na "dumping fee"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom