Kuna mgomo wa wauza mafuta?

Kuna mgomo wa wauza mafuta?

Mgongano wa maslahi, wanaotakiwa kusimamia sheria na kukemea hali hii tete wana hisa kubwa kwenye biashara hii ya mafuta. Watanganyika tuamke hakuna atakaye kuja kutukomboa ni sisi wenyewe.
 
Nguvu ya umma hata sisi tunayo,hujakatazwa kusema ila umekatazwa kuropoka

Define kuropoka, then from there we will have a common base to debate. Mbona mwoga wewe wakati hakuna kosa lililotendeka. Au una ndugu zako serikalini ndio maana unakuwa mtetezi mkubwa.
 
mimi nilishasema nchi hii haina serikali tena ila tumebakiza police wa kukandamiza raia wake,kuwapiga,kuua na kubambikiza kesi zisizo na maana yoyote.

Hivi waagiza mafuta wanaweza kufanya ujinga huu wa kutotoa mafuta kwa Kamanda kagame /rwanda? au enzi za mwalimu wangejaribu kweli? ila tatizo tunalijua kuna conflict of interest maana na wakuu wa nchi wanafanya hii biashara ya mafuta.
 
Hivi UGOMVI wa JAIRO na MASEBU hauwezi kuwa unachangia hili tatizo?
 
Ni saa la pili sasa nimepanga foleni ya kusubiri mafuta ya petrol. Hivi hii nchi ina uongozi? Jk,pinda, bilali wapo wapi ? Hawaoni mateso ya watanzania. Ni njia gani rahisi ya kuhama nchi?

** Lol! Jiunge na Al-shabab..... free ticket out.
 
Kwenye luku mnaongeza mia mia tunanunua kwenye mafuta tunanunua lita 3000 tunalipa jamani jamani mbona hivi jamani???
 
Tukazanie bunge wafute sheria ya kutangaza bei ya mafuta kila baada ya wiki mbili. Ewura wanahujumu wananchi pamoja na nchi,kwa sababu wafanyabiashara sasa wanajua trend ya ewura katika kupandisha na kupunguza bei ya mafuta.Wiki hii bei inishuka automatically wiki itakayofuata itapanda. Kwa hiyo kwa vile biashara ni kununua kwa bei ndogo na kuuza kwa bei kubwa,wafanyabiashara wananunua mafuta mengi bei ishukapo, na kutunza kuyatuinza wakisubiri bei ipande ili wauze kwa bei kubwa ili wapate faida KUBWA.Ewura mtu anayeumia most ni mlaji wa mwisho,hivyo nawaombeni.
Formula ya uchumi iko wazi bidhaa inapokuwa adimu,bei lazima ipande na bidhaa inapokuwa ya kumwaga bei inashuka.
 
Yote haya yanatokana na serikali yetu kuwa legelege. wameshindwa kuwa control matajiri.

Ingelikuwa bei ya mafuta imepanda saa hiyo hiyo wangepandisha na wao, lakini kwakuwa ni bei imeshuka eti wanagoma kisa wana stock kubwa ya mafuta. mbona bei ikishushwa wasisema wana stock kubwa?
Najuuuuuuuuuuuuuuuta!
 
Back
Top Bottom