Kuna mchezo unachezwa TANESCO

Kuna mchezo unachezwa TANESCO

Mapigo Saba

Senior Member
Joined
Dec 11, 2014
Posts
129
Reaction score
28
Bill ya umeme ya mwezi wa Kwanza ambayo imekuja mwanzoni mwa mwezi huu wa pili imewaacha watu hoi na nilidhani matumizi ya nyumbani kwangu ndo yamekuwa makubwa na kuanza kuwafokea watoto, kumbe ni kila kona ni kilio, kila mwezi bili yangu ya umeme ilikuwa inarange 5000-5500, LAKINI cha kushangaza bill imekuja 85,600/= nikajaribu kuuliza wenzangu kwa maana ya majiarani wakasema na wao imekuja kubwa sana, mmoja imekuja 94,650/= na mwingine 59,700/-

Huu ni uhuni wa serikali kwa Tanesco, yawezekana pesa ya uchaguzi inatafutwa sana hapa, au, kwa kuwa pesa ya kununulia vifaa vya BVR kits haipo na serikali imefirisika sasa inajaribu kufa na wananchi wake.

Acheni huu mchezo.
 
hapo ni sehem ambayo mafisad wa ccm wamewekeza raia wa kawaida utalia na kusaga meno mpaka utakapo amua kuchagua viongoz walio bora sio akina pinda wanaongoza nchi kwa kudhan!!
 
go to tanesco
Halafu kama bado upo analogia kuwa na utaratibu wa kuandika units kila mwezi
 
Ndugu yangu Mapigo Saba,moja ya MIRIJA mikubwa inayotumiwa na watawala wetu kufanya WIZI, ni kupitia NISHATI.
 
wandugu hata mie na wife tuu kipindi cha nyuma tulikuwa tuna tumia unit 1 kwa siku now hadi unit 2 na hakuna tulichoingeza ndio kwanza friji tunaliwasha kwa masaaa.huu mchezo nilihisi wanacheza na units za luku zinaliwa haraka tukanunue tena wapate za uchaguzi.
 
Bill ya umeme ya mwezi wa Kwanza ambayo imekuja mwanzoni mwa mwezi huu wa pili imewaacha watu hoi na nilidhani matumizi ya nyumbani kwangu ndo yamekuwa makubwa na kuanza kuwafokea watoto, kumbe ni kila kona ni kilio, kila mwezi bili yangu ya umeme ilikuwa inarange 5000-5500, LAKINI cha kushangaza bill imekuja 85,600/= nikajaribu kuuliza wenzangu kwa maana ya majiarani wakasema na wao imekuja kubwa sana, mmoja imekuja 94,650/= na mwingine 59,700/-

Huu ni uhuni wa serikali kwa Tanesco, yawezekana pesa ya uchaguzi inatafutwa sana hapa, au, kwa kuwa pesa ya kununulia vifaa vya BVR kits haipo na serikali imefirisika sasa inajaribu kufa na wananchi wake.

Acheni huu mchezo.
Kwanza Nitangulize pole Sana, Hizi ndio sign za serekali na chama chake cha mafisadi kinavyokufa. Tushirikiane kukiondoa ccm Madarakani

Chadema Kwanza
 
bill ya 5000 kwa mwezi inatia mashaka makubwa kuwa inawezekana tataizo liko kwako.

wengi tunatumia mbinu za vishoka kuunganisha umeme au kuchezea mita na matokeo ni kulipa kidogo.

hivyo kabla ya kulalamika hakikisha uko msafi kwa maana wateja wanaojua walikuwa wakifanya wizi na shirika linapoziba mianya ya kuiba badala ya kunyamaza na kujua wamenigundua wanaanza kupiga kelele kama wameibiwa wao. hao kazi ni kuwapiga faini mpaka nyumba zao zikauzwa kwa maana wanaiba kwa kiburi.

gharama za umeme zitazidi kupanda tu iwapo kuna wateja wataendelea kuiba umeme kwa maana wale wanaolipa itabidi kuongezewa bei ili kufidia umeme unaotumiwa na wezi au shirika kukosa mapato na matokeo yake ni huduma hafifu.


hivyo kama unajijua ni mwizi basi bora unyamaze na ulipe hiyo halali, ila kama una taa kidogo tena energy saving, hautumii pasi wala friji hapo pengine unaweza kulalamika.

Bill ya umeme ya mwezi wa Kwanza ambayo imekuja mwanzoni mwa mwezi huu wa pili imewaacha watu hoi na nilidhani matumizi ya nyumbani kwangu ndo yamekuwa makubwa na kuanza kuwafokea watoto, kumbe ni kila kona ni kilio, kila mwezi bili yangu ya umeme ilikuwa inarange 5000-5500, LAKINI cha kushangaza bill imekuja 85,600/= nikajaribu kuuliza wenzangu kwa maana ya majiarani wakasema na wao imekuja kubwa sana, mmoja imekuja 94,650/= na mwingine 59,700/-

Huu ni uhuni wa serikali kwa Tanesco, yawezekana pesa ya uchaguzi inatafutwa sana hapa, au, kwa kuwa pesa ya kununulia vifaa vya BVR kits haipo na serikali imefirisika sasa inajaribu kufa na wananchi wake.

Acheni huu mchezo.
 
watanzania tulio wengi tunaibiwa na bei za umeme,tulio wengi tumefungiwa mita za viwanda vidogo,ambapo umeme wa kiwanda kidogo ni 370 kwa unit,lko makaz ya kawaida unatakiwa ulipe chn ya 200,kwa umeme usiozd unit 75 kwa mwez.halaf wanaleta punguzo la sh8 kweli!! 8 mara ngapi ili upate unit 1 ambyo utahisi punguzo umelifaidi? Viongozi ubnafsi utawaumbua siku moja
 
Hayo matumizi yako kwa mwezi kiboko!

mimi situmii Luku natumia mita tu, hayo maluku ni wizi wakuu, kwani bila kuwa na kuanzia na 10000 hupati umeme, lakini mita hata 4000 umeme unao.
 
  • Thanks
Reactions: rpg
mimi situmii Luku natumia mita tu, hayo maluku ni wizi wakuu, kwani bila kuwa na kuanzia na 10000 hupati umeme, lakini mita hata 4000 umeme unao.
Unachoongea siyo kweli. Mimi natumia Luku name huwa nanunua hata wa ellfu 1
 
Mie wamekuja nyumbani mafundi wakapachika kiwaya kwenye luku na kumlazimisha h/girl asaini na kupiga picha meta na H/girl eti tumeiba umeme. mimi najiuliza huo waya ameweka nani? anayenunua umeme ni mimi sasa iweje mtu aweke waya ili matumizi yapungue? na kama ni hivyo mbona matumizi hayajapungua wakati natumia pia mkaa na jiko la gasi. halafu wamenidai 1.2 eti nimechezea luku. Mimi naona ni ujanja wanatafuta pesa kwa nguvu. nasema hivi " Mungu wa Mbinguni ameona".
 
Unachoongea siyo kweli. Mimi natumia Luku name huwa nanunua hata wa ellfu 1
anachoongea ni cha kweli. ni kama wamepandisha bei ya umeme vile. umeme sasaivi ni garama sana sana. jamani tanesco wapunguze kidogo kwa kweli. mimi nilijua kwangu tu, kumbe na kwa wenzangu. na jinari zangu fulani wapangaji niliwakuta wanagombana hadi wanasachiana wanafikiri labda mwenzao anatumia vitu vinavyokula umeme zaidi.
 
Back
Top Bottom