Kuna Kushinda na Kushindwa; CCM Inaposhindwa Iliposhinda...

Kwa ujumla, anafurahia mauaji. Mnakumbuka maelekezo aliyoyatoa kwa makamanda wa vyombo vya ulinzi?

''Mimi nashangaa sana. Eti wananchi wasio na hata na silaha yoyote wanaandamana kwenda kuzingira kituo cha polisi. Na nyie mna silaha, kwa nini hamuwalazi chini? Pale Chato kuna wakati wananchi walizingira kituo cha polisi. Kama ningefika pale, nikakuta watu wamelazwa chini, hata wangekuwemo ndugu zangu, ningempandisha cheo mkuu wa kituo'' -- JPM akiwahutubia makamanda. Kwa hiyo polisi wanaoua wanasubiria kupandishwa vyeo.

Huyu ndiye kiongozi tuliye naye. Ndiye tunayemtegemea, kwa kutumia vyombo alivyo navyo, atulinde sisi sote!!!
Halafu Mwanakijiji anasema tusimnyoshee kidole polisi wanatekeleza amri ya nani kama sio yake maana yake nini kauli kama hizi?Je hizi ni kauli za kiongozi wa nchi?
 
huu ni wakati wa watu wote bila kujali tofauti zetu huko nyuma kuyapinga haya yanayotokea nchini mwetu,uwe ccm,ukawa,tlp,cuf lipumba,nk wakati ndo huu tudai demokrasia ya kweli,pia hii tume ya uchaguzi NEC ni takataka tupu itupiliwe mbali kabisa
 
Inashangaza mno. Hata kipindi wengine tulichoona CCM imebeba ajenda muhimu awali kabisa baada ya kushinda 2015 inaamua kutumia mabavu mengi kuumaliza upinzani. Upinzani walishapoteana mapema kabisa ....CCM wakawapa ajenda zingine kizembe kabisa ....hata ambao tuliona 2020 ni nyepesi kwa CCM kuliko wakati wowote inageuka kwa kasi ....tena si kwa mbinu za wapinzani ....bali CCM wenyewe ....usajili wa akina Msando wengine tulijua labda wameamua kutengeneza team ya kushindana kwa hoja .....lakini mbinu zinatumika zile zile kama CCM ile ya JK ambayo hata mtu kuvaa gwanda lao alikuwa anaona aibu .....
 
Hivi nyie akina Mbowe na Nassari na viongozi wengine wa upinzani kile kifaa mlichotumia kumnasaa mnyeti kule Arumeru kwanini msingechukua kwa yule mkurugenzi wa TAKUKURU mkatumia kwenye huu uchaguzi?

Najua mnaushahidi wa kutosha ila kuna baadhi ya sehemu watu/mawakala hawakuruhiswa hata kupiga picha
 
Kuwa mstaarabu angalau kwa kukiri kwamba ulifanya makosa KUISAPOTI CCM na KUMSAPOTI MAGUFULI, ikiwa ni hasira zako kwa kile kilichofanywa na CHADEMA. kwa sababu kama ulivyosema kwamba hakuna jipya, kwamba kama ni wizi ulishafanyika tokea zamani, kama ni fujo tokea zamani, sasa kama ulijua yote hayo, na bado ukashabikia CCM na Magufuli wake kuanzia 2015, na sasa ndio unakumbuka shuka kumekucha, angalau uwe mkweli na muungwana ukiri kwamba ulikosea. Namna nyingine huna moral authority ya kuandika haya uliyoandika, hasa kwa mtu wa kaliba yako
 
Inashangaza mno. Hata kipindi wengine tulichoona CCM imebeba ajenda muhimu awali kabisa baada ya kushinda 2015 inaamua kutumia mabavu mengi kuumaliza upinzani. Upinzani walishapoteana mapema kabisa ....CCM wakawapa ajenda zingine kizembe kabisa ....hata ambao tuliona 2020 ni nyepesi kwa CCM kuliko wakati wowote inageuka kwa kasi ....tena si kwa mbinu za wapinzani ....bali CCM wenyewe ....usajili wa akina Msando wengine tulijua labda wameamua kutengeneza team ya kushindana kwa hoja .....lakini mbinu zinatumika zile zile kama CCM ile ya JK ambayo hata mtu kuvaa gwanda lao alikuwa anaona aibu .....
Umepiga U TURN kaka????
 
mzee umefilisika since uliamua kubong'oa mbele ya watawala.

CCM imemwaga damu kwasababu inajua haiwezi kushinda kwenye sanduku la kura kihalali.
 
Mwanakijiji -----Yaani kumpongeza Mtoto aliyefaulu kwa Kuiba Mitihani? Eti Kisa kwasababu kafaulu?Huyu Mtoto ameshirikiana na Baraza la Mitihani kuiba na ameshirikiana na wasimamizi wa mitihani kuiba na walinzi wa vituo vya mithani na mimi eti kama mzazi nimpongeze.
Mkuu sio tu kuiba mtihani,mana kuiba wanaiba wengi,Hili toto limeiba pepa,likahonga wasimamizi wa mitihani,likahonga mpaka wasahihishaji mbaya zaidi likatembeza kipigo na mikwara kwa watahiniwa wenzake,mbaya zaidi linabebwa na NECTA.
 
hajawahi kuacha kuwa mkweli! wewe jaribu kuwa na brain huru na ndio lengo la jukwaa hili

hamtakagi kweli na ndio mnaona upinzani unakufa mkiambiwa fanyeni hili hamtaki!!!

aibu, chutama
Upinzani unakufa sababu ya kukosa ubunge?!

Upinzani unajua tafsiri yake ni kuwa na wabunge wa upinzani ndani ya bunge pekee?!
 
Kitendo cha mchezaji au timu kucheza bila kumuumiza, kumdhalilisha au kumpigisha magoti mshindani au mpinzani wake kinaitwa “good sportsmanship” yaani “uanamichezo mzuri”.
Hiyo ni sawa kama huyo mshindani au mpinzani wako naye anayo sifa hiyo ya "good sportsmanship". Mshindani anayekutolea maneno machafu na matusi ya kila aina mnapokuwa kwenye mchezo hana sifa hiyo ya sportsmanship na kamwe hastahili kuonewa huruma. Lazima utamshikisha adabu kwa kumtandika hata bao 30 kwa nunge!
 
Hivi, ni ugumu gani uliopo kwa CCM kushinda vizuri tu bila Watanzania kuona kama ni lazima kila mtu apige magoti na kutoa sadaka kwenye madhabahu ya CCM na asiyefanya hivyo basi ni Mtanzania nusu na asiye na mapenzi na Taifa lake? Tunawafundisha nini watoto wetu na vijana wetu kuhusu ushindani katika siasa?
Nimesoma vizuri tu bandiko lako lakini hiki unachouliza hapo ni kujichanganya wewe mwenyewe hapo juu umesema ccm wana mbinu nyingi halali za kushinda ni zipi hizo hebu fafanua?kinyume chake ccm hawana mbinu zozote halali za kushinda uchaguzi wowote huru na haki na hilo ccm wanalijua vizuri,Polepole mwenyewe akiwa kwenye tume ya katiba alishasema uchaguzi ukiwa huru na haki ccm haiwezi kushinda.kununua madiwani na wabunge,kutumia nguvu kubwa ya jeshi la polisi,wakurugenzi wa uchaguzi makada wa ccm,kuuwawa kwa viongozi wa vyama pinzani n.k mabavu yote ya nini kama chama kinakubalika?
 
Back
Top Bottom