Kuna hatari ya kuibuka makundi ndani ya CHADEMA/UKAWA?

Mphamvu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
10,702
3,288
Hatua kubwa imechukuliwa na CHADEMA, kwa mwamvuli wa UKAWA, kumkaribisha kubwa la maadui awe miongoni mwao, na hatua hiyo imeshagawanya wafuasi wa chama hicho kifikra.

Wapo walioungana na kauli za kishujaa kuwa "Kwenye Siasa hakuna adui wala rafiki wa kudumu" na "Adui wa adui yako ni Rafiki yako" na wapo ambao wamepinga waziwazi hatua hiyo, wengine wakitishia kujiondoa kushabikia siasa.

Ukweli ni kuwa kubwa la maadui bado ana cheo chake cha jambazi kuu, maana mawaa yaliyomfanya awe na cheo hicho bado anayo na waliompachika mawaa hayo ndio hao anaojiunga nao.

Kama tulivyoona kwenye vyama vingine, kwenye vilabu vya soka na kadhalika kuwa maamuzi makubwa huibua makundi, wapo akina 'Asilia', 'Masilahi' na hata kwenye Klabu ya Simba kuliwahi kuwa na kundi la Mashabiki liliojiia UKAWA kutokana na historia ya wanachama wake.

Tetesi ni kuwa Kubwa la Maadui anakubalika kwa kuwa ana nguvu ya fedha, kwa hiyo maslahi ndiyo yaliyowafanya wamkubali japo kwa taabu. Mjadala wa 'magamba', 'masilahi' na 'asili' ndani ya Chama cha Mapinduzi uliwahi kutokea kipindi cha nyuma, na Kubwa la Maadui alihusika kiasi fulani.

Je, kunaweza kuibuka kundi pinzani ndani ya upinzani ambalo licha ya kutokubaliana na hatua hii linataka kubakia ndani ya chama na Muungano wake? Tufahamu wazi kuwa, licha ya kutokubaliana na viongozi, mwanachama ana haki ya kuendelea kuwa mwanachama na akalindwa na katiba ya chama.

Tunaweza kushuhudia makundi ndani ya CHADEMA au UKAWA kutokana na msimamo huu?


 
Kumbuka hata Marekani ilimtumia gaidi Osama Bin Laden kuisambaratisha Urusi. Iwapo Lowassa ana uwezo wa kuisambaratisha CCM ni lazima CDM wamtumie! Lengo ni kuing'oa CCM madarakani!

Siasa ni strategy na hii ni fursa nzuri ya CCM kufa hata kama ni kwa mbinu chafu! Mengine baadae!
 
ccm mwaka huu mnalo kila dakika mnaanzisha tread

Mkuu lazima tukubali uhalisia, kitaa kuna watu wamefadhaishwa sana na huu uamuzi wa CHADEMA na wasipojipanga hii inaweza kuwa ajenda baina ya wanachama na ajenda ya chama tawala dhidi ya upinzani.

Binafsi haikuwa karata nzuri kucheza na haikuwa na umuhimu kulingana na muda na uhalisia. Kitendo cha wapinzani kuungana tu dhidi ya chama tawala ilikuwa strategy nzuri sana kuelekea safari ya mafanikio lakini sasa tunaletewa unnecessary panic.
 
Makundi kwa kawaida yanasababishwa na viongozi. Kama viongozi wako pamoja hakuna litakaloharibika!!

Ndiyo maana Viongozi wote wa UKAWA wamekutana pamoja kuonyesha umoja wao.

Hao unaowadhania wewe kama kweli watajitokeza, watapita kama USHUZI tu.....!!!!
 
Hatuna shida ya Lowassa kuhamia CHADEMA na hata kugombea uraisi kupitia Ukawa, sisi tunataka mdadavue au adadavue yeye mwenyewe Lowassa kuhusu kashfa ya Richmond.

Atueleze mwazo mwisho wa sakata lenyewe, alihusika vipi na hakuhusika vipi, mana bado tunawalakini juu yako, tuna mashaka na tuna wasiwasi.

Tunaomba tafadhali utuaminshe sisi ambao bado fikra zetu zinakutambua wewe ni fisadi, mwizi na mla rushwa, hao ndipo tutakuelewa.

Hatuna mashaka na wewe kama tuu ukiweka mambo wazi, kama ulihusika utuombe radhi na kama hukuhusika, utuambie aliyehusika, na kwanini iwe wewe.

Unataka urais kwa gharama yoyote, kwanini umepania hivyo, wataka kutufanyia nini, kwanini siyo Mgombea mwezako Magufuli au hata huko ulipojiunga Chadema kwanini asiwe Slaa?

Tafadhali tunaomba yote haya utupe majibu, tukuelewe tuweze kuungana nawe. Baada ya hapo, tutakuwa pamoja na tutakua na imani na wewe.

Tunasubiri,

Shost.
 
Sasa ni wazi kuwa Chadema imewathibitishia watanzania kuwa iko tayari (kwa gharama zozote zile hata ikimaanisha ku-compromise sera za chama) kuongoza nchi kwa misingi ya kifisadi ambayo kwa sasa CCM wanapambana kuondokana nayo.

Je? Watanzania wako tayari kumkabidhi Lowassa funguo za Magogoni dhidi ya Dk. Magufuli?

Tukiwaweka Lowassa na Magufuli kwenye "uwanja" sawa (pasipo kutumia ushawishi wa pesa) na kuwaacha watanzania watoe hukumu kwa kutumia record zao za utendaji, nani ataibuka kidedea?

Wastaarabu wote karibuni mezani tuvutane kwa hoja.
 
Sasa ni wazi kuwa Chadema imewathibitishia watanzania kuwa iko tayari (kwa gharama zozote zile hata ikimaanisha ku-compromise sera za chama) kuongoza nchi kwa misingi ya kifisadi ambayo kwa sasa CCM wanapambana kuondokana nayo.

Je? Watanzania wako tayari kumkabidhi Lowassa funguo za Magogoni dhidi ya Dk. Magufuli?

Tukiwaweka Lowassa na Magufuli kwenye "uwanja" sawa (pasipo kutumia ushawishi wa pesa) na kuwaacha watanzania watoe hukumu kwa kutumia record zao za utendaji, nani ataibuka kidedea?

Wastaarabu wote karibuni mezani tuvutane kwa hoja.

Kma LOWASA ni fisad alpo jiuzulu ufisad imepngua au umezid
 
China kuna ndiko kuliko na sheria kali ya madawa ya kulevya lkn mbona bado wananchi wa china ndio wanaofanya hii biashara? Ukawa acheni ujinga wenu huyo tumeshamkata kama mnaasili ya ufisadi mchukueni tuu atawafaa ninyi lkn xy ikulu
 
Agenda yangu kwasasa nk kuhamasisha wananchi wasiachie pesa za huyo fisadi...zitafuneni lakini kwenye sanduku ya kura fanyeni maamuzi sahihi kwa ajili ya hiki kizazi na cha baadae...nadhani nimeeleweka.
 
China kuna ndiko kuliko na sheria kali ya madawa ya kulevya lkn mbona bado wananchi wa china ndio wanaofanya hii biashara? Ukawa acheni ujinga wenu huyo tumeshamkata kama mnaasili ya ufisadi mchukueni tuu atawafaa ninyi lkn xy ikulu

Nakuunga mkono mkuu..Lowassa atabaki rais wa UKAWA
 
kwan issue ya Escrow ilipoibuliwa EL alikuwepo madarakani? Twiga waliokuwa wanasafirishwa kwa ndege nje ya nchi Lowassa alikuwepo? Shehena za pembe za ndovu zilizo kamatwa zilikuwa na mkono waLowassa?....
 
Mimi hapa nmechanganyikiwa kabisa, sielewi ukawa kumchukua Lowasa is a big mistake CCM watapata agenda za kusema sana Mimi nasema Hapana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom