Kuna haja ya Rais kuchunguza mchakato wa CRDB kushinda tenda ya kulipa mishahara ya serikali

Kweli tutafika?muda wa kufanya kazi kwa bidii na sio kuanzisha majungu 24/7!Tuache majungu tupige kazi kwa bidii na sio kutumia watu nyuma ya mgongo kuchafua benki nyingine!

Majungu trna! Mm nilidhani tunafunua kila kitanda tuue kunguni wote.....Okay kama yanalipa tutayapika tu!
 
Najifunza vitu kadhaa kutokana na uzi huu:

1. Uzi umekuja baada ya kusoma Andiko kwamba CRDB wamepunguza kasi ya kutoa mikopo ili kuangalia na kutathmini stability ya hali ya uchumi nchini kisha watoe mikopo kwa wakopaji wa sekta inayoonesha viashiria vya kukua,

2. Waweza kuwa uzi uliotolewa na jamii ya Watu wasiopenda mawazo mbadala na walio hatari kuwa Washauri wa Rais kwani ni rahisi sana kumdanganya Rais kwa kutompatia alternative ideas against and towards situations,

3. Waweza kuwa uzi wa watu wanaopenda ukiritimba i.e monopoly kwani sijambo la kushadidiwa kwa watumishi wote wa umma nchini kuhudumiwa na NMB peke yake ktk kusambaza mishahara yao ya kila mwezi,

4. Waweza kuwa ni uzi wa watu ambao hawajawa na taarifa za kina kwamba NMB haikunyang'anywa kabisa tenda bali ilitolewa ktk kuwa sole distributor wa mishahara kwa watumishi wote wa umma nchini,

5. Waweza kuwa ni uzi wa watu waficha maovu kwani inaonekana kabisa kuna jambo ovu ulikuwa unalidhania kuwepo na kutendwa na crdb ktk kupata hiyo tenda lkn ukawa kimya mpaka pale ambapo crdb walipotoa kauli ambayo imekuudhi. Jamii kama hii haimsaidii Rais,

6. Mtazamo wa CRDB kama kweli ndiyo huo unapaswa kuwa changamoto kwa Wizara ya Fedha na Mipango kurejea hali ya uchumi wa taifa kwa sasa kwa ujumla wake na kwa kaya (the homestead economic survey) ili tuone hali yetu kiuchumi ki Per Capita na ki GDP ili tuje na Mikakati inayoimarisha ukuaji wa vitu vyote hivi,

7. Tumuombee JPM asizungukwe na Wanafiki ili juhudi zake, nia yake na malengo yake yazae taifa jipya lenye watu wenye kuaminiana, wenye kupenda kufanya kazi na kulipenda taifa lao, waadilifu, makini na wenye kupenda ushindani wa kimaendeleo.

mkuu hiyo namba saba "tuombe Mungu, Magu asizungukwe na human satanic gates" wanaotaka kumpotosha na kutomwambia ukweli
 
Ni vizur kukaa na kuwaza nifanye nn kujikwamua kiuchumi lakini sio kuwachukia au kuwafanyia fitna wale wenye mafanikio kiuchumi; Hii ni itakufanya uzidi kupoteza nafasi ya mafanikio. Benki ya CRDB inajina kubwa pia inamafanikio makubwa ukitafta mbinu ya kuichafua utapoteza nafasi zaidi ya kuifikia.
 
Harakati za kuponda bila hoja zimeendelea kuwa big deal Tanzania yetu. Badala ya benki iliyokosa tenda ikaze ili next time ishinde, inakaza kwenye kuponda na kupotosha. Namna hii mshindi atabaki kuwa mshindi. Haya ndio mambo ya Debe tupu !!
 
Tukiendelea kutumia mda wetu kufanya watu waamini upuuzi soon tutakuwa wapuuzi. Huwezi kuhoji CRDB kushinda tenda. Na juzi kati umethibitishiwa ni benki bora Afrika na hakuna benki yoyote Tanzania ilowahi kupata hio tuzo but CRDB. so from which angle wasishinde tenda? try to be logical japo kwa kulazimisha!!
 
mkuu hiyo namba saba "tuombe Mungu, Magu asizungukwe na human satanic gates" wanaotaka kumpotosha na kutomwambia ukweli
Uaninifu hauji kiujanja ujanja ni kwakuwa wazi wenye kufanya kwa faida ya wote. Tatizo letu kubwa we do not want change hasa kama zina gusa comfort zones zetu. Na pale maslahi yetu yanapoguswa hatupotayari kuangalia in a posituve eyes ni vipi kweli sisi ni vikwazo kwenye jamii. Hii yote ina chagizwa na selfish attitudes zilizojijenga kwa muda mrefu na kudhania vibaya wengine hata pale wanapoangalia maslahi mapana ya nchi.

Hivi lro hii tuamini kuwa hii comfort zone ya less than 10% inapoondolewa ndiyo nchi uchumi wake una dondoka? Watu wanashindwa kujua wakati tukijitapa uchumi upo imara more than 60% ya raia walikuwa wana ishi kwa mlo mmoja what do say about those in relation to uchumi imara tunao brag nao?
Hapa leo kinachoongelewa kwenye mada hii ni watu wanapendekeza ichunguzi ufanyike kama kuna un wanted ways zilifanyika mtu objective unathubutu kusema wanafiki? Nani huyo kati ya wewe na wale wanaotaka uchubguzi? Tena mm ningeona hii ingrijengea bank credibility zaidi kwakua uchunguzi ndiyo ungewaonyesha watu intension zao kama zilikuwa mbaya dhidi ya bank!

Dhambi huwa zinatakiwa kutubu siyo ki cover....na toba ya kweli ni kugeuka na kuacha....Uaminifu wa kweli hupatikana pale kila mmoja anaporidhika na game of rules na siyo kufanya usanii.

Hakuna anayeichukia vank yeyotr na pale mtu anapoona kuna tatizo anahaki ya ku raise banner kama wewe ni safi unatoa tu ushirikiano with positive mind ili kuondoa huko kutoaminiana!
 
Wadau,

Baada ya kuona mzee wa watu (Magufuli) anaandamwa na watu ambao walipaswa kumsaidia kuinua hali ya uchumi wa Taifa hili, watu ambao wanajua fika kwamba kupitia taasisi zao wamechangia katika kulirudisha Taifa hili nyuma kwa miongo kadhaa, watu ambao hawana shukrani kiasi ya kuombea mabaya kila kukicha, watu ambao elimu zao za uchumi hazisaidii Taifa kwa mawazo chanya, ......Nimeamua nimshauri mzee wangu JPM.

Ikumbukwe kuwa mwaka uliopita , benki ya CRDB ilishinda tenda ya usambazaji wa mishahara ya serikali, kwa maoni yangu binafsi na maoni ya watu wengi waliolitazama jambo lile kwa jicho la tatu walijiuliza iweje NMB yenye mtandao mpana wa huduma hadi vijijini, benki ambayo serikali ina hisa, benki ambayo ni mkombozi kwa walalahoi inyang'anywe tenda ile wakati ina sifa za ziada kuliko CRDB ambayo hata baadhi ya wilaya nchini haijafika?? Kwa nini tenda ile ipewe CRDB ambayo ina kiasi kidogo sana cha wafanyakazi wa serikali ambao wanapitishia mishahara yao kule?

Nani alisaidia CRDB kushinda tenda ile!!!! kitendo ambacho kimeongeza gharama za kuhamisha pesa kutoka benki ya CRDB kwenda benki nyengine ambazo idadi kubwa ya wafanyakazi wa serikali wana akaunti za mishahara? ni kwa faida ya nani?

Nichukue nafasi hii kumuomba Rais wetu mpendwa Ndugu, Dkt John Joseph Pombe Magufuli auchunguze ule mchakato wote ulioipatia benki ya CRDB tenda ya kusambaza Mishahara iliyopelekea kuongezeka kwa gharama za "inter-banking transaction" tofauti na ilivyokuwa awali.


Update: 19-08-16
Nasikia "Kimei" kakanusha taarifa zilizonukuliwa na magazeti kupitia mkurugenzi wa masoko.....Niwahakikishieni tu kuwa, "Kimei" ni lazima atambue kuwa JPM hajaribiwi.

Ni hayo tu.

Tume ya Katiba

Mcheza pool table Maarufu.
This is a very bias news is
 
Harakati za kuponda bila hoja zimeendelea kuwa big deal Tanzania yetu. Badala ya benki iliyokosa tenda ikaze ili next time ishinde, inakaza kwenye kuponda na kupotosha. Namna hii mshindi atabaki kuwa mshindi. Haya ndio mambo ya Debe tupu !!
 
This is a very bias news is
Yaani ukisoma toka mwanzo unaona the way mko bias ... pia kama mnaisakama CRDB Bank for no reason . Nadhani mna yenu sio Bure. Ila mwenye macho haambiwi tazama . Na wenye macho wanaona u bora wa Benki ya CRDB . Hebu tafuteni mada za msingi acheni umbea wa bila malipo ........
 
Harakati za kuponda bila hoja zimeendelea kuwa big deal Tanzania yetu. Badala ya benki iliyokosa tenda ikaze ili next time ishinde, inakaza kwenye kuponda na kupotosha. Namna hii mshindi atabaki kuwa mshindi. Haya ndio mambo ya Debe tupu !!
 
Tulijua tu mtakuja ambao mmekosa pumba baada ya Kimei kuongea ukweli kuhusu hali ya kiuchumi ilivyo..na bado mtaendelea kuumbuka kizazi hichi siyo kile cha danganya toto..ulivyo mjinga katika hoja zako unadiliki kusema kwanini walishinda tenda ilihali wana wafanyakazi wengi,una akili kweli wewe? Kwahiyo kigezo chako kuwa wafanyakazi wakiwa wengi ufanisi wa kazi unakuwa mkubwa?

Hoja ni kuwa NMB ni benki nyenye matawi kila wilaya na serikali ina hisa nyingi humo. Kwa nini hizo bank charges za kuhudumia mishahara ya wafanyakazi wa serikali zisibaki NMB ili ipate faida zaidi na serikali ipate gawio kubwa kwenye faida ya benki? Mambo ya Kimei yanahusika nini?
 
JPM anaimba kila siku kuwa msemakweli ni mpenzi wa Mungu. Iweje Dr. Kimei kwa kusema ukweli aanze kuandamwa? JPM ameshasema kuwa hata watalii wapungue kufikia laki tano hatishiki, sasa CRDB na mabenki mengine wakiaacha kutoa mikopo kwenye sekta ya utalii watakosea? Ndio maana wenye maono tunasema, JPM apime madhara ya kauli zake kwa uchumi wa nchi. Amri na matamshi tata majukwaani haviendani na uchumi, haswa unaomilikiwa na sekta binafsi.
 
Jana nilisema Kimei atazingirwa, sasa naona ametangulia huyu upande wake akisubiri na wenzake waje kujipanga wamzingire
 
Wadau,

Baada ya kuona mzee wa watu (Magufuli) anaandamwa na watu ambao walipaswa kumsaidia kuinua hali ya uchumi wa Taifa hili, watu ambao wanajua fika kwamba kupitia taasisi zao wamechangia katika kulirudisha Taifa hili nyuma kwa miongo kadhaa, watu ambao hawana shukrani kiasi ya kuombea mabaya kila kukicha, watu ambao elimu zao za uchumi hazisaidii Taifa kwa mawazo chanya, ......Nimeamua nimshauri mzee wangu JPM.

Ikumbukwe kuwa mwaka uliopita , benki ya CRDB ilishinda tenda ya usambazaji wa mishahara ya serikali, kwa maoni yangu binafsi na maoni ya watu wengi waliolitazama jambo lile kwa jicho la tatu walijiuliza iweje NMB yenye mtandao mpana wa huduma hadi vijijini, benki ambayo serikali ina hisa, benki ambayo ni mkombozi kwa walalahoi inyang'anywe tenda ile wakati ina sifa za ziada kuliko CRDB ambayo hata baadhi ya wilaya nchini haijafika?? Kwa nini tenda ile ipewe CRDB ambayo ina kiasi kidogo sana cha wafanyakazi wa serikali ambao wanapitishia mishahara yao kule?

Nani alisaidia CRDB kushinda tenda ile!!!! kitendo ambacho kimeongeza gharama za kuhamisha pesa kutoka benki ya CRDB kwenda benki nyengine ambazo idadi kubwa ya wafanyakazi wa serikali wana akaunti za mishahara? ni kwa faida ya nani?

Nichukue nafasi hii kumuomba Rais wetu mpendwa Ndugu, Dkt John Joseph Pombe Magufuli auchunguze ule mchakato wote ulioipatia benki ya CRDB tenda ya kusambaza Mishahara iliyopelekea kuongezeka kwa gharama za "inter-banking transaction" tofauti na ilivyokuwa awali.


Update: 19-08-16
Nasikia "Kimei" kakanusha taarifa zilizonukuliwa na magazeti kupitia mkurugenzi wa masoko.....Niwahakikishieni tu kuwa, "Kimei" ni lazima atambue kuwa JPM hajaribiwi.

Ni hayo tu.

Tume ya Katiba

Mcheza pool table Maarufu.

Mtoa mada yaonyesha umetumwa na NMB na wamekununua kwa bei rahisi sana. Mafanikio ambayo Dr Kimei ameyafanya kwenye nchi hii ni makubwa sana na ameonyesha uzalendo na mapenzi kwa nchi yake. Hivi karibuni Benki ya CRDB imepewa tuzo ya kuwa Benki namba moja Tanzania na Kusini mwa jangwa la sahara kuwa una uwezo mkubwa wa kuhimili madeni yake na kuwa rated kwa daraja la B1. Isitoshe miradi mikubwa yote ya nchi hii CRDB ndio wametoa fedha mfano. Ujenzi wa Terminal 3 JNIA, Soko la Mwanjelwa, Miradi ya barabara, Viwanda nk. Haya ni mafanikio ya Dr Kimei. Kuhusu hili suala la kuhudumia Halmashauri za Serikali, mchakato ulikuwa wazi kazi. Mabenki yalipewa fursa ya kwenda kufanya presentation kwenye Halmashauri zote , na baada ya hapo Halmashauri wao wenyewe wakaamua benki ipi iwahudumie, hapo hujuma ipo wapi ?. Hii yaonyesha umetumwa na unatumika na NMB na huujui mchakato jinsi ulivyo kwenda mpaka CRDB kuchaguliwa.
 
Hoja ni kuwa NMB ni benki nyenye matawi kila wilaya na serikali ina hisa nyingi humo. Kwa nini hizo bank charges za kuhudumia mishahara ya wafanyakazi wa serikali zisibaki NMB ili ipate faida zaidi na
serikali ipate gawio kubwa kwenye faida ya benki? Mambo ya Kimei yanahusika nini?
Kwa akili yako CRDB haina matawi kila wilaya? Usipende kukurupukia mambo ambayo huyajui
 
Back
Top Bottom