Habari za jioni wanabodi.
Ni utaratibu uliokithiri kwenye jamii nyingi bila kuangalia dini zao ama makabila yao, unakuta kwenye msiba mtu amefariki anazikwa na suti,vito vya thamani kama cheni na pete, smartphone.
kwa maoni yangu huu ni upotevu mkubwa wa mali ukizingatia vitu anavyozikwa navyo vilitengenezwa kwa ajili ya walio hai sasa mtu aliyekufa pete ya zahabu ama smartphone anaenda kuitumia wapi?
Mi naona hizi tamaduni zingine ni za kumkufuru mungu tu hazina maana yeyote, eti unakuta mtu anazikwa na gitaa kwa kuwa alikuwa mwanamuziki, nani amesema mungu anataka apigiwe gitaa na binadamu.
Naomba tuangalie hali halisi na uhalali wa mtu kuzikwa na vitu vya thamani, kama kuna mdau ana mwongozo wa vitabu vya dini auelete hapa uweze kutusaidia malengo hasa ya zahabu inayotafutwa kwa hali na mali kisha kuvishwa binadamu aliyekufa na kurudishwa ardhini tena?
Ni utaratibu uliokithiri kwenye jamii nyingi bila kuangalia dini zao ama makabila yao, unakuta kwenye msiba mtu amefariki anazikwa na suti,vito vya thamani kama cheni na pete, smartphone.
kwa maoni yangu huu ni upotevu mkubwa wa mali ukizingatia vitu anavyozikwa navyo vilitengenezwa kwa ajili ya walio hai sasa mtu aliyekufa pete ya zahabu ama smartphone anaenda kuitumia wapi?
Mi naona hizi tamaduni zingine ni za kumkufuru mungu tu hazina maana yeyote, eti unakuta mtu anazikwa na gitaa kwa kuwa alikuwa mwanamuziki, nani amesema mungu anataka apigiwe gitaa na binadamu.
Naomba tuangalie hali halisi na uhalali wa mtu kuzikwa na vitu vya thamani, kama kuna mdau ana mwongozo wa vitabu vya dini auelete hapa uweze kutusaidia malengo hasa ya zahabu inayotafutwa kwa hali na mali kisha kuvishwa binadamu aliyekufa na kurudishwa ardhini tena?