Kuna haja ya kusherehekea mwaka mpya?

Kuna haja ya kusherehekea mwaka mpya?

Ngonepi

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2013
Posts
1,872
Reaction score
1,212
Wana Cc, kuna kitu nakiona katika maisha yetu ya kila siku na kwangu nimeshindwa kukielewa kabisa.
Hivi ni lazima wote tusherehekee mwaka mpya? Huku uswazi ninakoishi nakutanaga na watu ambao mpaka hupata majeraha kwa namna wanavyoshehekea mwaka mpya.
Kwa mawazo yangu naona kama ingefaa zaidi kwa wale waliofanikiwa malengo yao kwa mwaka unaoisha ndio wangesherehekeamwaka mpya.

Unasherehekeaje mwaka mpya hali huna ulichokifanya mwaka unaoisha, na wala huna mipango yoyote kwa mwaka unaofuatia!

Hii kwangu kwa kweli sioni haja ya kufurahia mwaka mpy maana yake ikiwa sina mipango yeyote wala mwaka niumalizao hakuna nilichokifanya
nawakilisha.
 
Basi waache waliopata mafanikio mwaka uliopita na wenye mipango endelevu kwa mwaka huu mpya washerehekee.....
 
Mi niko kivingine!
As a matter of fact ! Kusheherekea mwaka mpya ni kusheherekea kifo!
Kwa maana ya kila mtu aelewe kila Saa , Siku , Wiki , Mwezi , Mwaka , Muongo , vikipita hua havirejei tena na kila vikipita jua ndiyo inavyopelekea umri wako wa kuishi kusogea na kila usugeapo ndiyo safari ya ahera! (Ahera moja)
 
Kushehekea mwaka mpya bila kuwa na malengo yoyote ni ujinga, sijui hata huwa wanashangilia nini aisee!
 
Mie huwa naungana na wadau wengine kusherehekea ingawa sijui huwa tunasherehekea nini..!?
 
Mie huwa naungana na wadau wengine kusherehekea ingawa sijui huwa tunasherehekea nini..!?

Na wengi hizi ndio zao, yaani mtu anashrehekea utadhani labda ni kitu gani sijui, mpaka anajisababishia majeraha au kuamka akiwa hana hata senti tano kisa mwaka mpya.

Sasa ukiangalia kinchomfurahisha hakionekani kabisa, au anasherehekea kuwa hai! mbona siku zote alikuwa hai na hajawahi kusherehekea hivyo!!
inashangaza kwa kweli!
 
Aise hata mimi sijui kama unaweza kuserebuka kama hujafanya chochote cha maana;
Daaah mwaka 2013 ni kama sikufanya kitu cha maana sana, ila naomba sana Mungu
hii 2014 nitimize malengo yangu mawili tu.
 
Be transparency at your goals !
May be God spotted someone to direct you to a certain achievement !
 
Aise hata mimi sijui kama unaweza kuserebuka kama hujafanya chochote cha maana;
Daaah mwaka 2013 ni kama sikufanya kitu cha maana sana, ila naomba sana Mungu
hii 2014 nitimize malengo yangu mawili tu.
M/mungu atakufanyia wepesi.
Nalog off
 
Back
Top Bottom