Kuna Dalili Nchi ikakumbwa na Ukame?

Kuna Dalili Nchi ikakumbwa na Ukame?

Mchochezi

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
11,449
Reaction score
9,748
Wakuu habari zenu,

Kwasasa hali ya mvua hapa nchini si nzuri. Kuna baadhi ya maeneo mvua huanza kunyesha mapema tu mwishoni mwa mwezi wa pili na mwanzoni mwa mwezi wa tatu lakini kwasasa hayo maeneo ni makavu na sasa tunaelekea mwisho wa mwezi March, hali ya mvua ni ya wasiwasi.

Nini kitatokea kama mvua haitonyesha? Ni ukame na kuadimika kwa vyakula pamoja na kupanda kwa bei za vyakula.

Nini kifanyike endapo nchi itakumbwa na ukame? Ilihali tunaelewa kabisa hakuna mashamba ya serikali? Yaani hakuna chakula cha msaada? Nini kifanyike wakuu?
 
Mikoa inayolisha Nchi hii ni Mbeya, Iringa, Rukwa, Ruvuma, Songwe na Njombe. Kote Huko walipata mvua za kutosha na tarajieni mazao tele. Ukiachia mkoa wa Ruvuma, Huko upinzani umeshika kasi, hii inaashiria Mungu yuko against CCM, Dodoma kukame, watu wamekaukiwa hadi mate
Watu wamekaukiwa hadi mate !!!!!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wala usiwe na wasiwasi na hilo, Joto mwezi huu ndio mahala pake. Kwa ukanda wa pwani, mvua zitanyesha kuanzia wiki ya kwanza ya mwezi wa nne hadi tutaomba jua liwake tena.... Mozambique juzi tu mafuriko yamefanya kitu ambacho hakijawahi kutokea.. watu 1000 wameishafariki hadi sasa. Gharika iliyotokea Mozambique mwaka 1996 matokeo yake tuliyaona hata sisi, Tujiandae tu.
 
Mikoa inayolisha Nchi hii ni Mbeya, Iringa, Rukwa, Ruvuma, Songwe na Njombe. Kote Huko walipata mvua za kutosha na tarajieni mazao tele. Ukiachia mkoa wa Ruvuma, Huko upinzani umeshika kasi, hii inaashiria Mungu yuko against CCM, Dodoma kukame, watu wamekaukiwa hadi mate
Dodoma lini wakawa na hali nzuri ya hewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mikoa inayolisha Nchi hii ni Mbeya, Iringa, Rukwa, Ruvuma, Songwe na Njombe. Kote Huko walipata mvua za kutosha na tarajieni mazao tele. Ukiachia mkoa wa Ruvuma, Huko upinzani umeshika kasi, hii inaashiria Mungu yuko against CCM, Dodoma kukame, watu wamekaukiwa hadi mate
Ni kweli mie niko ruvuma ila mvua mwaka huu imekata kabisa kwa mfano songea ina week sasa haijanyesha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom