Kuna Baadhi ya wanasiasa wakistaafu siasa; Taifa litapumua

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
37,545
47,194
Kwakweli kuna baadhi ya wanasiasa wanaturudisha nyuma kutokana na kupoteza muda kujadili mambo yao ambayo kwa kiasi kikubwa yamelipatia Taifa hili hasara tu.

Ukijaribu kufuatilia kila jambo ambalo limekua kikwazo kwa namna moja au nyingine wameshiriki.

Naona kwakua tunatumia muda mwingi sana kuwajadili ni bora tu wakastaafu siasa kwa manufaa ya uma ile tuweze kupumua na makando kando yao.

Naamini kabisa pindi wakiamua kwenda kupumzika majumbani mwao, tutawasahau na tutaendelea na kulijenga taifa letu. Naamini kabisa mambo waliyoyafanya pia tutayasahau, na tunaahidi kuwasamehe kabisa, mradi tu wakubali kutupumzisha.

Asanteni wazee wangu.
 
Kuna wale wako kwenye payroll ya Egypt, kutwa kucha kuhakikisha wanapambana ili wakazi WA kando ya Lake Victoria hawanufahiki na hiyo resources.
 
Kwakweli kuna baadhi ya wanasiasa wanaturudisha nyuma kutokana na kupoteza muda kujadili mambo yao ambayo kwa kiasi kikubwa yamelipatia Taifa hili hasara tu.

Ukijaribu kufuatilia kila jambo ambalo limekua kikwazo kwa namna moja au nyingine wameshiriki.

Naona kwakua tunatumia muda mwingi sana kuwajadili ni bora tu wakastaafu siasa kwa manufaa ya uma ile tuweze kupumua na makando kando yao.

Naamini kabisa pindi wakiamua kwenda kupumzika majumbani mwao, tutawasahau na tutaendelea na kulijenga taifa letu. Naamini kabisa mambo waliyoyafanya pia tutayasahau, na tunaahidi kuwasamehe kabisa, mradi tu wakubali kutupumzisha.

Asanteni wazee wangu.

Apumzike Bashite!!!
 
Kwa bahati mbaya wale wazee wa awamu zilizopita wamekwisha pandikiza watoto na ndugu zao kila sehemu muhimu. Itachukua muda mrefu sana mambo kubadilika
 
Kama hayo makando-kando yao yanahusu ufisadi wapelekeni kwenye mahakama ya mafisadi ili muwapumzishe gerezani kama kweli wamewabana pumzi.
 
Hawawezi kupumzika kwan wanajua kusoma na kuandika tu. Wakipumzika watakula nini?
 
Kwakweli Rais alimuumbua waziri mkuu aliposema wafanyakazi hewa na vyeti feki mawaziri waliopita hawakuona?? Wakati huo Katelefoni mjaliwa alikuwa Tamisemi!! Lakini naye wizarayake ilikuwa na mahewa sema nyani haonagi 'kungu' lake!!
 
kwa uchache tu; Lowasa; lipumba ; maalim; sumaye na kingunge; hawa wachukue mfano kwa wenzao kina Pinda na prof
tapatalk_1493580467619.jpeg
 
Back
Top Bottom