Uchaguzi 2020 Kuna alichojifunza mzee baba hadi sasa?

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,826
35,827
Mabibi na mabwana heshima kwenu.

Siku ya 9 leo tangu kampeni zianze, hali ya upepo nchini kwa ujumla tayari inatoa picha kuhusiana na uchaguzi mkuu ujao.

Magufuli alidhani anakubalika kwa 100%. Alidhani wapinzani hawatakuwa na hoja na eti labda wangekuwa wanamfanyia yeye kampeni tu.

La haula! Hali si hivyo.

Upepo umebadilisha ile minya minya yote ya habari. Wanapodhibiti radio na Tvs, ndiyo kwanza inawahamasisha zaidi wananchi kwenda mikutanoni.

Ukweli mchungu ni kuwa pana kundi kubwa la watu wenye chuki na hata hasira na mkuu huyu.

Yote kheri, kwa vile kuishi kwingi ni kuona mengi bila shaka huu utakuwa ni wasaa mzuri kwake kuweza kujitafakari.

Kwanini kama binadamu uchukiwe kiasi tunachokiona? Nini alichowakwaza hivi wamchukiao? Afanye nini kuubadili upepo huu?

Leo tu wazima hakuna ajuaye yajayo. Katangulia mzee Mkapa (rip) mema yake mengi yalisomwa.

Hala hala mtu unaweza somewa maovu kimzaha mzaha hivi hivi.

Ilikuwa vyema kuelezana wakati tungali hai na katika hali ya amani. Pana na kesho na keshokutwa pia.

Mbona kina mzee ruksa, mzee kikwette na wengine wapo wanadunda mtaani na amani zao zote za moyo?

Hali isije kuwa tofauti kwa Mzee baba kwani hao wengine hawakuwahi kuchukiwa kwa kiwango cha wazi hivi.

Misahafu inasema heri ya wapatanishi.

Kwa pamoja tuwasaidie watia nia wetu kukubalika kwa wananchi

Bandugu halipo neno mantashari kama tuhoye (kisukuma), rajunah (Italiano), rejoice (English), yaani maridhiano (kiswahili).

Hala hala kabla ya hatari.

Tahadhari inaponya!
 
FB_IMG_1599228588465.jpg
 
Mkuu!

Acheni kushinda mitandaoni njooni huku mitaani jamani huku ndio kura zilipo.

Yani kwa jinsi hali ilivyo huku ni kama vile watu walishajitayarisha kumpitisha Magu.

Sioni upinznai mtatokea wapi mwaka huu

Hivi unadhani huku mitandaoni ni nje ya nchi, au ukiingia mitandaoni basi huwezi kukaa mtaani? Narudia tena, chini ya Magufuli hakuna uchaguzi, bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
Hivi unadhani huku mitandaoni ni nje ya nchi, au ukiingia mitandaoni basi huwezi kukaa mtaani? Narudia tena, chini ya Magufuli hakuna uchaguzi, bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
Sawa mkuu mwambieni basi Lisu ajitoe!
 
Mkuu!

Acheni kushinda mitandaoni njooni huku mitaani jamani huku ndio kura zilipo.

Yani kwa jinsi hali ilivyo huku ni kama vile watu walishajitayarisha kumpitisha Magu.

Sioni upinznai mtatokea wapi mwaka huu
Ccm ni wajinga kiasi gani ninyi?
Watu wakiwa wengi kwenye mikutano ya Lissu mnasema siyo wapiga kura, hawana kadi, hawajajiandikisha, wapiga kura wapo mtaaani.

Watu wakiwa wengi kwenye mikutano ya ccm(maanna huwa wanakuwa wengi waje kuona tamasha la mziki na wapiga mitama) huwa mnasema hao ndo wapigga kura na kuwa jiwe anakubalika.

Huu upuuzi wenu huu mnajidanganya sana, mnajitekenya kisha mnacheka wenyewe, ukweli mnaujua wenyewe, jiwe hakubaliki, ameshapoteza mvuto!
 
Back
Top Bottom