MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
53.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, Waziri Mkuu
atawajibika kwa Rais kuhusu utekelezaji wa madaraka yake.
(2) Serikali ya Jamhuri ya Muungano, chini ya mamlaka ya
Rais, ndiyo itakuwa na uwezo wa kufanya maamuzi juu ya sera ya
Serikali kwa jumla, na Mawaziri, chini ya uongozi wa Waziri Mkuu,
watawajibika kwa pamoja Bungeni kuhusu utekelezaji wa shughuli
za Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
53A.-(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ya 51 ya Katiba hii,
Bunge linaweza kupitisha azimio la kura ya kutokuwa na imani na
Waziri Mkuu endapo itatolewa hoja kupendekeza hivyo na
ikapitishwa kwa mujibuwa wa masharti ya ibara hii.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja
yoyote ya kutaka kupitisha kura ya kutokuwa na imani na Waziri
Mkuu haitatolewa Bungeni endapo-
(a) haina uhusiano na utekelezaji wa majukumu ya Waziri
Mkuu kwa mujibu wa ibara ya 52 ya Katiba hii, wala
hakuna madai kwamba Waziri Mkuu amevunja Sheria
ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
(b) haijapita miezi sita tangu alipoteuliwa;
(c) haijapita miezi tisa tangu hoja ya namna hiyo
ilipotolewa Bungeni na Bunge likakataa kuipitisha.
(3) Hoja ya kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu
haitapitishwa na Bunge isipokuwa tu kama-
(a) taarifa ya maandishi, iliyotiwa sahihi na kuungwa
mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya
Wabunge wote itatolewa kwa Spika, siku angalau kumi
na nne kabla ya siku inapokusudiwa kuwasilishwa
Bungeni;
(b) Spika atajiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili
ya kuleta hoja yametimizwa.
(4) Hoja iliyotimiza masharti ya ibara hii itawasilishwa Bungeni
mapema iwezekanavyo kwa mujibu wa Kanuni za Bunge.
(5) Hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu itapitishwa tu
iwapo inaungwa mkono na Wabunge walio wengi.
(6) Endapo hoja ya kura ya kutokuwa na imani kwa Waziri
Mkuu itaungwa mkono na Wabunge wengi, Spika atawasilisha
azimio hilo kwa Rais, na mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote
vile ndani ya siku mbili tangu Bunge lilipopitisha azimio la hoja ya
kura ya kutokuwa na imani kwa Waziri Mkuu, Waziri Mkuu
atatakiwa ajiuzulu, na Rais atamteua Mbunge mwingine kuwa
Waziri Mkuu.
atawajibika kwa Rais kuhusu utekelezaji wa madaraka yake.
(2) Serikali ya Jamhuri ya Muungano, chini ya mamlaka ya
Rais, ndiyo itakuwa na uwezo wa kufanya maamuzi juu ya sera ya
Serikali kwa jumla, na Mawaziri, chini ya uongozi wa Waziri Mkuu,
watawajibika kwa pamoja Bungeni kuhusu utekelezaji wa shughuli
za Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
53A.-(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ya 51 ya Katiba hii,
Bunge linaweza kupitisha azimio la kura ya kutokuwa na imani na
Waziri Mkuu endapo itatolewa hoja kupendekeza hivyo na
ikapitishwa kwa mujibuwa wa masharti ya ibara hii.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja
yoyote ya kutaka kupitisha kura ya kutokuwa na imani na Waziri
Mkuu haitatolewa Bungeni endapo-
(a) haina uhusiano na utekelezaji wa majukumu ya Waziri
Mkuu kwa mujibu wa ibara ya 52 ya Katiba hii, wala
hakuna madai kwamba Waziri Mkuu amevunja Sheria
ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
(b) haijapita miezi sita tangu alipoteuliwa;
(c) haijapita miezi tisa tangu hoja ya namna hiyo
ilipotolewa Bungeni na Bunge likakataa kuipitisha.
(3) Hoja ya kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu
haitapitishwa na Bunge isipokuwa tu kama-
(a) taarifa ya maandishi, iliyotiwa sahihi na kuungwa
mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya
Wabunge wote itatolewa kwa Spika, siku angalau kumi
na nne kabla ya siku inapokusudiwa kuwasilishwa
Bungeni;
(b) Spika atajiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili
ya kuleta hoja yametimizwa.
(4) Hoja iliyotimiza masharti ya ibara hii itawasilishwa Bungeni
mapema iwezekanavyo kwa mujibu wa Kanuni za Bunge.
(5) Hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu itapitishwa tu
iwapo inaungwa mkono na Wabunge walio wengi.
(6) Endapo hoja ya kura ya kutokuwa na imani kwa Waziri
Mkuu itaungwa mkono na Wabunge wengi, Spika atawasilisha
azimio hilo kwa Rais, na mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote
vile ndani ya siku mbili tangu Bunge lilipopitisha azimio la hoja ya
kura ya kutokuwa na imani kwa Waziri Mkuu, Waziri Mkuu
atatakiwa ajiuzulu, na Rais atamteua Mbunge mwingine kuwa
Waziri Mkuu.