Kumsaidia mkeo kazi za ndani si ujinga hata kidogo

Bernard bakari

JF-Expert Member
Mar 30, 2016
407
780
Kuna maisha yamejengeka katika jamii kuwa mwanamke ndiye anatakiwa afanye kazi zote za ndani kama vile kufua, kupika, kuosha vyombo, kufanya usafi na kazi zingine nyingi za kifamilia.

Kuna wakati unaona kabisa mwanamke anachoka yeye apige deki nyumba, akimaliza akapike chai, akafue nguo akimaliza achote maji aanze kuandaa chakula cha mchana mwanaume amekaa tu anasubiri chai kisha anashinda na Tv anasubiri chakula cha mchana kisha anaangalia mpira anasubiri chakula cha usiku. Maisha hayo yamepitwa na wakati wanaume tubadilike Mwanamke si mtumwa.

Mwanamke anatakiwa kusaidiwa kazi wakati yeye anapiga deki mwanaume anza kujaza maji kwenye vyombo kama nyumba yako ina mfumo wa maji kila sehemu ni vyema ukaanza kuosha vyombo akimaliza wakati anapika chai chukua nguo anza kufua atakuja kukusaidia chai ikiwa tayari kisha mnamaliza kwa mda mfupi mnakunywa chai mtajikuta kazi zinaisha mapema naye anapata mda wa kupumzika na kuandaa chakula cha mchana pole pole kwa furaha.

Maisha ya sasa ni ya kusaidiana tusiwafanye wake zetu kama watumwa. Mwanamke anayohaki ya kupumzika na anastahili kusaidiwa kazi. Niwatakie jumatatu njema
 
Tatizo wanaume wa kiafrika tume wageuza wake zetu kama wafanyakazi wa ndani... utakuta mke katoka kazi kama ww kachoka kama ww lakini mkifika nyumbani yeye ndio afanye kazi zote peke yake
Huu sio ustaarabu hata kidogo..
 
Tatizo wanaume wa kiafrika tume wageuza wake zetu kama wafanyakazi wa ndani... utakuta mke katoka kazi kama ww kachoka kama ww lakini mkifika nyumbani yeye ndio afanye kazi zote peke yake
Huu sio ustaarabu hata kidogo..
Ndio maana hatutaki wafanye kazi, wakae nyumbani ebo
 
Kama wewe ni great thinker huwezi kumuachia mkeo kazi zote, achana na mila za zamani, ukifika nyumbani gawaneni kazi zikiisha angalieni TV pamoja
 
Kuna maisha yamejengeka katika jamii kuwa mwanamke ndiye anatakiwa afanye kazi zote za ndani kama vile kufua, kupika, kuosha vyombo, kufanya usafi na kazi zingine nyingi za kifamilia.

Kuna wakati unaona kabisa mwanamke anachoka yeye apige deki nyumba, akimaliza akapike chai, akafue nguo akimaliza achote maji aanze kuandaa chakula cha mchana mwanaume amekaa tu anasubiri chai kisha anashinda na Tv anasubiri chakula cha mchana kisha anaangalia mpira anasubiri chakula cha usiku. Maisha hayo yamepitwa na wakati wanaume tubadilike Mwanamke si mtumwa.

Mwanamke anatakiwa kusaidiwa kazi wakati yeye anapiga deki mwanaume anza kujaza maji kwenye vyombo kama nyumba yako ina mfumo wa maji kila sehemu ni vyema ukaanza kuosha vyombo akimaliza wakati anapika chai chukua nguo anza kufua atakuja kukusaidia chai ikiwa tayari kisha mnamaliza kwa mda mfupi mnakunywa chai mtajikuta kazi zinaisha mapema naye anapata mda wa kupumzika na kuandaa chakula cha mchana pole pole kwa furaha.

Maisha ya sasa ni ya kusaidiana tusiwafanye wake zetu kama watumwa. Mwanamke anayohaki ya kupumzika na anastahili kusaidiwa kazi. Niwatakie jumatatu njema
Nyie ndo nasema mpo duniani kupita. Badilisha mawazo bwana mkubwa. Inatakiwa uishi

Ninaposema uishi, namaanisha uwe na mawazo chanya ya kuibadilisha dunia.

Wenzako wanahangaika kila siku waweze kurahisisha mambo. Yaani kila kitu kifanywe na mashine. Badala ya wewe kuelekeza mawazo yako ya nini wanaume cha kufanya wakati mwanamke anafanya kazi ambazo hazinaga mwisho, wewe unawarudisha nyuma wenzako.

Labda nikupe mfano, kipindi mama chanja akiwa mjamzito, nilikua najituma sana kusombelezea maji kutoka kwa nyumba ya jifani. Kuna siku nikawa nimechoka sana na Maji hayakuwepo ndani. Ilinibidi nikachote kwa kujilazimisha. Ndipo nilipoanza kujiuliza, hivi kubeba maji kwaajili ya mke wangu ndo upendo au kujitesa?
Nikajiuliza pia, kwani wanaoweka mfumo wa maji ndani ya nyumba ni wazembe?
Ndipo nilipogundua kuwa kwamba kumpenda mke wako ni kuhakikiaha unapata pesa za kutosha ili umuwekee kila kitu ndani.

Tafakari sana
 
Kuna maisha yamejengeka katika jamii kuwa mwanamke ndiye anatakiwa afanye kazi zote za ndani kama vile kufua, kupika, kuosha vyombo, kufanya usafi na kazi zingine nyingi za kifamilia.

Kuna wakati unaona kabisa mwanamke anachoka yeye apige deki nyumba, akimaliza akapike chai, akafue nguo akimaliza achote maji aanze kuandaa chakula cha mchana mwanaume amekaa tu anasubiri chai kisha anashinda na Tv anasubiri chakula cha mchana kisha anaangalia mpira anasubiri chakula cha usiku. Maisha hayo yamepitwa na wakati wanaume tubadilike Mwanamke si mtumwa.

Mwanamke anatakiwa kusaidiwa kazi wakati yeye anapiga deki mwanaume anza kujaza maji kwenye vyombo kama nyumba yako ina mfumo wa maji kila sehemu ni vyema ukaanza kuosha vyombo akimaliza wakati anapika chai chukua nguo anza kufua atakuja kukusaidia chai ikiwa tayari kisha mnamaliza kwa mda mfupi mnakunywa chai mtajikuta kazi zinaisha mapema naye anapata mda wa kupumzika na kuandaa chakula cha mchana pole pole kwa furaha.

Maisha ya sasa ni ya kusaidiana tusiwafanye wake zetu kama watumwa. Mwanamke anayohaki ya kupumzika na anastahili kusaidiwa kazi. Niwatakie jumatatu njema
Wewe mkeo huwa unamfanyia haya au umecopy mahali?
 
Hayo nitafanya kipindi cha weekend labda na kipindi cha dharura mfano ugonjwa, ujauzito, labda kama ameumia n.k ila siku nyingine atanisamehe...nitoke kazini nimefanya kazi huko nimechoka na nyumbani tena niwe na zamu ya kudeki, kuosha vyombo na kufua?? HELL NO!!
 
Naunga mkono hoja,ila kumsaidia mkeo kukuna nazi...hapana kwa kweli!!
 
Kuna wakati unaona kabisa mwanamke anachoka yeye apige deki nyumba, akimaliza akapike chai, akafue nguo akimaliza achote maji aanze kuandaa chakula cha mchana mwanaume amekaa tu anasubiri chai kisha anashinda na Tv anasubiri chakula cha mchana kisha anaangalia mpira anasubiri chakula cha usiku. Maisha hayo yamepitwa na wakati wanaume tubadilike Mwanamke si mtumwa.
Hii haikubaliki, sio sawa!
 
unaweza kutenga siku moja ktk wk....home duty.......unaandaa bf lunch even dinner,,,,kunyoosha nguo zenu za wk nzima...sio mbaya.....bali isiwe kwa lazima hiyari
 
  • Thanks
Reactions: BAK
hakuna ubaya kumsaidia mm binafsi huwa namsaidia sana mkewangu huwa anafurahi sana endapo nikimsaidia japo nakaa dsm yeye yupo moro kwa kikazi huwa naenda kila baada ya wiki na msaidia kuanzia kupika kudeki mpaka kufua na sion tatizo zaidi ya kuongeza furaha
 
Hayo nitafanya kipindi cha weekend labda na kipindi cha dharura mfano ugonjwa, ujauzito, labda kama ameumia n.k ila siku nyingine atanisamehe...nitoke kazini nimefanya kazi huko nimechoka na nyumbani tena niwe na zamu ya kudeki, kuosha vyombo na kufua?? HELL NO!!
Vipi na yeye kama anafanya kazi?
 
Back
Top Bottom