luhala
JF-Expert Member
- Feb 25, 2012
- 412
- 142
Kuna taarifa kwamba wanajeshi wa Nigeria sasa wanawastukia makamanda wao wanaoshukiwa kuwa na uswahiba na Boko Haram na kumkosakosa mmoja wa makamanda wanafiki. Wananchi pia wameanzisha vikundi vyao vya kujihami dhidi ya majambazi hawa.
Habari zaidi zinasema wananchi wa vijiji vitatu hivi karibuni "waliwachangamkia" maharamia hawa na kuangamiza 200 kati yao.
Kama habari hii ni kweli basi mapambano dhidi ya wahalifu hawa ni magumu kutokana na ukweli kwamba kundi hili haramu limejipenyeza hadi ndani ya Jeshi la nchi hiyo na mbaya zaidi hadi ndani ya safu ya viongozi waandamizi wanaoonekana kuvuruga mipango ya Jeshi katika kupambana nao.
Haiingii akilini kabisa kuona Jeshi la nchi hiyo limeshindwa kuua idadi hiyo ya magaidi hawa wakati wanavijiji tu wameweza! Kama hili ni sahihi siku za Boko Haram kuendelea "kutanua" zinahesabika kwani hakuna nguvu zinazoweza kuushinda umma ulioungana.
================================================
Sent from my iPhone using JamiiForums
Habari zaidi zinasema wananchi wa vijiji vitatu hivi karibuni "waliwachangamkia" maharamia hawa na kuangamiza 200 kati yao.
Kama habari hii ni kweli basi mapambano dhidi ya wahalifu hawa ni magumu kutokana na ukweli kwamba kundi hili haramu limejipenyeza hadi ndani ya Jeshi la nchi hiyo na mbaya zaidi hadi ndani ya safu ya viongozi waandamizi wanaoonekana kuvuruga mipango ya Jeshi katika kupambana nao.
Haiingii akilini kabisa kuona Jeshi la nchi hiyo limeshindwa kuua idadi hiyo ya magaidi hawa wakati wanavijiji tu wameweza! Kama hili ni sahihi siku za Boko Haram kuendelea "kutanua" zinahesabika kwani hakuna nguvu zinazoweza kuushinda umma ulioungana.
================================================
Wanajeshi nchini Nigeria, wamemfyatulia risasi kamanda wao mkuu katika mji wa Maiduguri Kaskazini Mashariki mwa nchi.
Hata hivyo Meja Jenerali, Ahmed Mohammed alinusurika kifo. Shambulizi lilifanywa dhidi ya gari lake katika kambi ya jeshi ya Maimalari .
![]()
Wanajeshi hao walimlaumu kamanda kwa mauaji ya wanajeshi wenzao walioshambuliwa na kundi la Boko Haram na kuuawa.
Wakati huohuo, Rais wa Goodluck Jonathan amesema hayuko tayari kubadilishana wasichana miambili waliotekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram wanaozuiliwa katika magereza ya Nigeria.
![]()
Wazazi wa wasichana waliotekwa nyara na Boko Haram
Waziri wa serikali awali alikuwa amesema kuwa maafisa wa utawala walikuwa tayari kwa mazungumzo na Boko Haram lakini Rais Goodluck Jonathan amesisitiza kwamba swala hilo halitazungumziwa.
"Amesisitiza kwamba hataongea na Boko Haram kuhusu kubadilishana wasichana waliotekwa na wapiganaji wa kundi hilo wanaozuiliwa nchini humo," alisema mwakilishi wa serikali ya Uingereza Mark Simmonds baada ya kukutana na Rais Jonathan kujadili namna ya kuwanusuru wasichana hao.
Hatua ya kutekwa nyara kwa wasichana hao katika jimbo la Borno tarehe 14 Aprili, imesababisha kero kubwa kwa jamii ya kimataifa kiasi cha kulazimisha baadhi ya nchi za kutoa wataalamu kusaidia serikali ya Nigeria kuwatafuta wasichana hao.
Sent from my iPhone using JamiiForums