Kumekucha Marekani angalia Picha Jinsi Waandamanaji wakikabiliana na polisi

Econometrician

JF-Expert Member
Oct 25, 2013
15,797
28,460
160710083212__us_protest_624x351_getty.jpg
Image copyrightGETTY
Image captionWaandamana kupinga mauaji ya weusi Marekani

Polisi katika jimbo la Louisiana Marekani wamemkamata mwanaharakati wa kupigania haki za weusi katika makabiliano na waandamanaji katika mji wa Baton Rouge.

160709075843_us_protest_640x360_ap_nocredit.jpg
Image copyrightAP
Image captionDeRay McKesson alikuwa mmoja wa waandamanaji waliokamatwa
DeRay McKesson alikuwa mmoja wa waandamanaji waliokamatwa na polisi wakipinga mauaji ya weusi wawili mikononi mwa polisi.

160710083542__us_protest_624x351_ap.jpg
Image copyrightAP
Image captionMapema rais Obama alikana kuwa Marekani imetumbukia katika ubaguzi wa rangi wa miaka 60.
Kamata hiyo ya polisi ilitokea huku maandamano ya kupinga mauaji yanayofanywa na polisi dhidi ya watu weusi yakiendelea katika miji kote nchini Marekani licha ya wito kutoka kwa rais Barack Obama kulitaka taifa kuungana baada ya kuuawa kwa polisi 5 katika mji wa Dallas.

160710083803__us_protest_624x351_epa.jpg
Image copyrightEPA
Image captionMaandamano mengi yalikuwa ya amani.
Maandamano mengi yalikuwa ya amani.

Lakini katika maeneo ya Baton Rouge huko Louisiana na St Paul katika jimbo la Minnesota, maeneo ambapo wanaume wawili weusi waliuawa juma lililopita, kulishuhudiwa makabiliano kati ya polisi na waandamaji.

Mapema rais Obama alikana kuwa Marekani imetumbukia katika ubaguzi wa rangi wa miaka 60.

160710083445__us_protest_624x351_ap.jpg
Image copyrightAP
Image captionPolisi katika jimbo la Louisiana Marekani wamemkamata mwanaharakati wa kupigania haki za weusi
Huko Baton Rouge waandamanaji walikuwa na kibwagizo cha 'no justice, no peace', yaani ''bila ya haki kutendeka hakutakuwa na amani''

160709075927_us_protest_kids_624x351_ap_nocredit.jpg
Image copyrightAP
Image caption"black lives matter" na "hands up, don't shoot" vilirindima kote
Vibwagizo hivyo pamoja na "black lives matter" na "hands up, don't shoot" vilirindima kote katika maeneo hayo ya hivi punde zaidi kuathirika na mauaji ya weusi.

chanzo:BBC masaa 2 yaliyopita
 
Back
Top Bottom