Kumekucha Jimbo katoliki Moshi na Arusha

LAMBOFGOD

JF-Expert Member
Aug 12, 2016
1,561
1,315
Jimbo katolik Moshi na Arusha laazimia kuondoa kikwazo cha mahali kwa vijana wengi wanaoshindwa kufunga ndoa zao kwa kutozwa mahali kubwa kubwa na wazazi wa mabinti hivyo kuwafanya wawili hao kuendelea kuwa wachumba sugu na wazinzi wazoefu aidha waumini wametakiwa kuondokana na mila zilizopitwa na wakati za kuwatoza mahali vijana wanapotaka kuanzisha familia kwani huo ndio wito wa kwanza mwanadamu kuitwa kule bustanini eden, kwani kufanya hivyo ni kukatili mpango wa Mungu wa kuzaa na kuongezeka. Waumini wametakiwa kutokuchukulia maanani swala la mahali kwani haiwafanyi wapendanao hao kudumu katika upendo wao kwenye maisha ya ndoa yaliyojaa njia panda zinazohitaji maamuzi na machaguzi sahihi ili kuzivuka kwani yule mwovu huvizia katika dhoruba za njia panda kuwatia vishawishini. Mahali kwa wazazi imetakiwa kuchukuliwa kama zawadi za kawaida kabisa kulinganisha na udugu huo mpya unaoanzishwa

Mengi tu yalizungumuzwa ila haya machache nimewafikishia.

Karibuni kuoa/kuolewa moshi na arusha kwani sisi hatuangalii tena mahali ila kuwasaidia kudumu katika ndoa zenu ambazo ni paradise ndogo hapa duniani wala si ndoano kama wengi wanavyozichukulia

NAWASILISHA
 
Ila mahari nyingi zinaishia kwenye sherehe za kitchen party na sendoff
 
Hata hivyo wanasema kuwa mahari huwa haiishi.
Wachaga wamezid hasa ukute familia bora halaf ndio bint kapitapta shule anakabachelor ndio kabisa utapigwa 8M na ndoa haifungwi mpka ulipe 4M... Hiyo uliobak utamalizia mbele ya safar... Ukijiumauma unaambiwa kama umeshindwa kulipa mahar kama hyo utawezaje kumtunza mtoto wao????

Ndio maana wengne wanajichukulia maamuz tu ya sogea tuishi mkishazaa mtoto ndio mnaanza process wakileta magumash mnabarik ndoa then life linasonga
 
Mahari ni lazima iwepo kwanini asante kwa walezi sema naitizama pale asante inavyopangwa na anayepewa. Mwacheni mtoa asante atoe asante yake kwa kadiri ya atakavyoona yeye inamfaa, msitake asante asante na mkampangia mtoaji atoeje na asante haiwezi kuwa lazima kwani ikifanywa na ka ulazima "automatically" inakosa maana ya asante.
 
Mkuu hata tuliooa kwahiyo tunaruhusiwa kuoa tena?
Yah, sie wanaume kwanza tunajiwekea vimasharti tu, kama manabii waliweza kuoa wanawake wengi ni kwanini leo sie tuzuiwe jambo jema hivyo? Kwani manabii waliokuwa wanatenda dhambi walivyokuwa wakioa wake wengi?
 
Ni jambo zuri sana wamefanya...ikifaa na majimbo mengine yauchukue mpango huu ili vijana waweze kufunga ndoa kuepukana na uzinzi.
 
Kwa waafrica suala la mahari ni lazima.. akili imegota hapo..
Jamii ikiamua mbona inawezekana?may be kama familia husika itamfanya binti husika kuwa kitegauchumi chao ila kama sio hivyo hili linawezekana.nilivyoelewa mimi unaweza kuambiwa mahari toa 100,000/= or 50,000/= sio mtu unaambiwa 2,000,000/=ambazo ni mtaji kabisa wa biashara.
 
Back
Top Bottom