Munawavuruga Watanganyika.
Sasa hiyo yenu ni rasimu ya ngapi?
Kwani Kuna rasmu ngapi?
1. Ya JK
2. Ya Warioba
3. Ya Ukawa
4. Tanzania Kwanza
5. ........
ongezeeni hapo.
By The way Hilo tamko mumeandikiwa na CCM na hapo kunawatu wamekuwa Millionairs.
Pesa zinazotumika kupotosha ukweli wakat wananchi wanajua, zingepelekwa mahosptalini ningeshukuru kweli
Juzi nimeenda AMANA HOSPT nilitamani kulia yani wamama wamelala chini kabisa na mimba zao, wengine na watoto niliumia sanaaaa nikajiuliza hapa ni mjini tena city center kabisa je huko nachingwea vijiji vip
Inauma sana, mzee maliza vizuri uende msonga ataingia chizi zaidi yako utapata tabu sanaaaa.
lililululululuuuuuuuuuluuuu wapigaji vigelegele mjengoni!!!!!!!! Hapo ndipo huwa mnaniacha hoi, mnapiga vigelegele utadhani mko kwenye harusi au kitchen party!!! Kuweni serious bwana nyie wajumbe wa bunge katiba. Au ndo mmeishaanza kupewa vibahasha mahotelini eh! ili muanze kutoa matamko ya kujiweka sawa kukubali yale ya wachache.
Kingunge ameishawapa muongozo, tunataka katiba itayotuletea maendeleo kama katiba za wenzetu walioendelea na siyo kwenda kutafuta posho na ipad huko.